Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 15,101
- 56,054
Kwenu wana CCM mnaojitambua, wenye mapenzi mema na chama na mustakbali mwema wa nchi hii.
Hicho mlichofanyiwa Dodoma ni uhuni mtupu, hakipo ndani ya kanuni, taratibu wala culture ya chama.
Inakuwaje mnakubali genge dogo la watu wachache wanakaa chemba ili waje wawastukize kwa jambo nyeti kama hilo la kupata mgombea wa nafasi za Urais wa JMT na ZNZ?.
Kwa nini mgeuke rubber stamp tu ya maamuzi ya genge dogo lililokwepa taratibu za chama zilizozoeka?
Hebu jiulizeni, huyo anayekwepa mchakato wa kawaida wa kugombea anaogopa nini, kawakosea nini wana CCM hadi aruke vikao vya maamuzi vya chama kama mwanga arukavyo kwenye ungo?.
Ndugu wana CCM, mkikubaliana na uhuni huu maanq yake mnatengeneza precedence ya UHUNI mkubwa zaidi kufanyika ndani ya chama.
Aliyewahi kuwa katibu mkuu mwenezi wa CCM bwana Polepole amewahi kusema kuwa ndani ya CCM kuna WAHUNI na bila shaka mmethibitisha wenye hili jambo kwa UHUNI usio na chembe ya haya wala aibu, kwa kuletewa mgombea kwa mlango wa nyuma bila ngazi tofauti za chama na taratibu zake kufuatwa.
Najua bado mna hyesteria ya mkutano, wengine posho zimewatia upofu, Pengine mastarehe ya muda mfupi yaendayo na mkutano bado mna hangover nayo. Lakini Jiulizeni hiki kilichofanyika ni sawasawa.
Hebu simameni sasa muanze kukataa uhuni huu wa watu wachache kupika mambo sirini halafu wanakuja kuwastukiza kama mmekamatwa ugoni vile.
Msikubali kuwa pawns au kete za kutumika tu katika hii chess ya mustakbali wa chama na nchi. Anzeni kuonyesha hisia zenu waziwazi.
Hii siyo CCM ya Nyerere, hii ni CCM ya kihuni.
Hicho mlichofanyiwa Dodoma ni uhuni mtupu, hakipo ndani ya kanuni, taratibu wala culture ya chama.
Inakuwaje mnakubali genge dogo la watu wachache wanakaa chemba ili waje wawastukize kwa jambo nyeti kama hilo la kupata mgombea wa nafasi za Urais wa JMT na ZNZ?.
Kwa nini mgeuke rubber stamp tu ya maamuzi ya genge dogo lililokwepa taratibu za chama zilizozoeka?
Hebu jiulizeni, huyo anayekwepa mchakato wa kawaida wa kugombea anaogopa nini, kawakosea nini wana CCM hadi aruke vikao vya maamuzi vya chama kama mwanga arukavyo kwenye ungo?.
Ndugu wana CCM, mkikubaliana na uhuni huu maanq yake mnatengeneza precedence ya UHUNI mkubwa zaidi kufanyika ndani ya chama.
Aliyewahi kuwa katibu mkuu mwenezi wa CCM bwana Polepole amewahi kusema kuwa ndani ya CCM kuna WAHUNI na bila shaka mmethibitisha wenye hili jambo kwa UHUNI usio na chembe ya haya wala aibu, kwa kuletewa mgombea kwa mlango wa nyuma bila ngazi tofauti za chama na taratibu zake kufuatwa.
Najua bado mna hyesteria ya mkutano, wengine posho zimewatia upofu, Pengine mastarehe ya muda mfupi yaendayo na mkutano bado mna hangover nayo. Lakini Jiulizeni hiki kilichofanyika ni sawasawa.
Hebu simameni sasa muanze kukataa uhuni huu wa watu wachache kupika mambo sirini halafu wanakuja kuwastukiza kama mmekamatwa ugoni vile.
Msikubali kuwa pawns au kete za kutumika tu katika hii chess ya mustakbali wa chama na nchi. Anzeni kuonyesha hisia zenu waziwazi.
Hii siyo CCM ya Nyerere, hii ni CCM ya kihuni.