Wana CCM tuambieni Tanzania ilipata uhuru tarehe, mwezi na mwaka gani?

Wana CCM tuambieni Tanzania ilipata uhuru tarehe, mwezi na mwaka gani?

Imekuwa kawaida viongozi wamekuwa wakiiambia Dunia kwamba Tanzania ilipata uhuru tarehe 09/12/1961.
Tarehe 9/12/1961

Kwa muktadha huo ni ukweli kwamba Tarehe 09/12/1961 ni Siku ya Tanganyika kupata Uhuru.
Nawatakia mapumziko mema ya kumbukumbu ya siku uhuru na jamhuri ya nchi iliyokuwa Tanganyika sasa Tanzania。Tarehe 9 Desemba 1961 Tanganyika ilipata uhuru toka kwa mkoloni Mwingereza,9 Desemba 1962 ikawa jamhuri。 Tarehe 26 April 1964 ikaungana na Zanzibar na kubadili jina na kuwa Tanzania,hivyo leo tunapoadhimisha siku hii,ile Tanganyika iliyopata uhuru wake siku hii sasa haipo tena,iliyopo ni Tanzania hivyo kumbukumbu ndio ya Tanganyika lakini maadhimisho ni ya Tanzania。
Heri ya Uhuru na Jamhuri。
P。
 
Nawatakia mapumziko mema ya kumbukumbu ya siku uhuru na jamhuri ya nchi iliyokuwa Tanganyika sasa Tanzania。Tarehe 9 Desemba 1961 Tanganyika ilipata uhuru toka kwa mkoloni Mwingereza,9 Desemba 1962 ikawa jamhuri。 Tarehe 26 April 1964 ikaungana na Zanzibar na kubadili jina na kuwa Tanzania,hivyo leo tunapoadhimisha siku hii,ile Tanganyika iliyopata uhuru wake siku hii sasa haipo tena,iliyopo ni Tanzania hivyo kumbukumbu ndio ya Tanganyika lakini maadhimisho ni ya Tanzania。
Heri ya Uhuru na Jamhuri。
P。
Mbona Zanzibar mapinduzi day haiitwi "Mapinduzi ya Tanzania Visiwani"!? Tanganyika ipo ( ambayo ni Tanzania isiyo na Zanzibar) na Zanzibar ipo ( ambayo ni Tanzania isiyo na Tanganyika) . Ccm jaribuni kuachana na huu upumbavu wa kujifanya kuwa Tanganyika haipo. Tanganyika hakuna sehemu iliwahi badili jina. Hakuna. Sema TU Kuna nchi ambayo inaitwa Tanzania ambayo ni Muungano wa Tanganyika Na Zanzibar.
 
Mdogo wangu Paschal nimeona unaungana na hoja ya Uhuru wa Tanzania SIYO Tanganyika. Naomba utusaidie kujua mambo yafutayo;
1. 9/12/1961 kulikuwepo na Tanzania?
2. Je Tanganyika au Tanzania Bara imewahi kubadili jina ikajiita Tanzania? If yes,lini na kwa hati gani?
3. Tukisema Uhuru wa Tanzania tunamaanisha hata Zanzibar walipata Uhuru wao 9/12/1961?
4. Kama Zanzibar inatarehe yake yakupata Uhuru ambayo naamini ni siku ya Mapinduzi, tunasemaje Tanzania ilipata Uhuru mwaka 1961 tukijua kilichopata Uhuru ni sehemu tu ya Tanzania ambayo ni Tanganyika?
5. Kwa uelewa wako Mapinduzi ya Zanzibar yanaweza kutambua kama siku ya Uhuru ya Zanzibar?
6. Hoja Yako ya kusherekea ya Sasa ( present) umeitoa kwenye nyaraka gani?

Nauliza haya baada ya kuona mada zako zote zimeacha lakuna kwenye maeneo hayo: Nikutakie siku njema ya Uhuru wa Watanganyika
Haya maswali atayajibu kweli?
 
Back
Top Bottom