Wana CCM tusiwe makeyboard warriors: Tuingie mabarabarani kupinga kodi na tozo zisizohalali, kulalamika kwenye whatsapp group hakutasaidia

Wana CCM tusiwe makeyboard warriors: Tuingie mabarabarani kupinga kodi na tozo zisizohalali, kulalamika kwenye whatsapp group hakutasaidia

Rasterman

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2015
Posts
33,894
Reaction score
44,117
Habari za Muda huu wana Jfs.

Ni muda sasa wa takribani mwezi kumekuwa na introduction ya kile kinachoitwa tozo ambapo kwa mujibu wa Mh Rais Samia kupitia Waziri Wake Dr Mwigulu nchemba na wabunge wake wanadai ni kwa ajili ya solidarity funds ili kusaidia miradi mbali mbali ya kijamii kama elimu na afya.

Baada ya watanzania wengi kulalamikia njia hiyo iliyokinyume na sheria za kodi Dr Mwigulu Nchemba aliwataka wananchi kuungana kwa pamoja kufanikisha jambo hili. Na kwamba yeyote anayeona kero kuchangua maendeleo ya nchi yake ni bora aanze mapema ahamie Burundi.

Haikuishia hapo zikaja tozo za simu na miamala, wanaccm wengi kwenye mitandao ya kijamii whatsapp, twitter, instagram, facebook na telegram wamelalamika sana kupita maelezo kiasi cha kuanza kutukana mamlaka zilizoko madarakani huku wakilinganisha na mamlaka ya awamu ya tano. Kilio cha kufa na kupona kimeanza baada ya kuongeza tozo kupitia mfumo wa kununua umeme wa LUKU hapa ndio wakazidi kuchanganyikiwa.

Msingi wa kuchanganyikiwa kwao ni kwa sababu

1. Moja hawakutarajia serikali yao ambayo 90% ya viongozi wao walipita bila kupingwa kuwafanyia unyama huu.

2. Waliamini Mama ni sawa na Mwendazake hivyo ataendelea kuwadekeza

3. Waliaminishwa uchumi wa nchi uko vizuri sasa wanashangaa matozo ya nini.

4. Wanaamini mfumo ulioko madarakani sasa una lengo la kurudisha ufisadi wa wazi ( ikumbukwe ufisadi wa magufuli ulikuwa mkubwa na wa kificho sana).

Wito kwa wanaccm popote mlipo badala ya kutupigia kelele sisi ambao ni wazalendi kweli kweli na tuko tayari kuchangia maendeleo ya nchi ni vema mkapinga kwa vitendo ikiwemo kuingia mabarabarani kuonesha hisia zenu Ni haki yenu kikatiba kupinga pale haki zenu mnapohisi zinavunjwa.

Ukweli daima, unafiki kwangu mwiko. Tudumishe itikadi hii.
 
Serikali iliyopita ilitumia pesa vibaya nchi haina pesa lazma sisi wenyewe tufunge mkanda kujenga nchi yetu.
Mleta mada shauri tupate wapi pesa !? Vinginevyo funga domo nchi ijengwe.
 
Serikali iliyopita ilitumia pesa vibaya nchi haina pesa lazma sisi wenyewe tufunge mkanda kujenga nchi yetu.
Mleta mada shauri tupate wapi pesa !? Vinginevyo funga domo nchi ijengwe.
Pesa nyingi zilitumika kweny uchaguzi. Tume ya Uchaguzi ilikula pesa nyingi plus loop holes za maded
 
Serikali iliyopita ilitumia pesa vibaya nchi haina pesa lazma sisi wenyewe tufunge mkanda kujenga nchi yetu.
Mleta mada shauri tupate wapi pesa !? Vinginevyo funga domo nchi ijengwe.
Huyu alisema yeye na mwendazake ni kitu kimoja
Sasa na yeye si atatumia hiyo hela vibaya tu?
 
Wanalalamika sana mpaka tumechoka sasa. huko mitandaoni Wamefura kila mahali
Umesoma vizur heading ya uzi wAKO?

Inavoonekana umejipa mamlaka ya kuwasemea wanacccm wakati wewe sio mwanaccm.

Sasa,
Tukikwambia una kiherehere,

Au unawashwa washwa tutakua tumekukosea heshima?
 
Umesoma vizur heading ya uzi wAKO?

Inavoonekana umejipa mamlaka ya kuwasemea wanacccm wakati wewe sio mwanaccm.

Sasa,
Tukikwambia una kiherehere,

Au unawashwa washwa tutakua tumekukosea heshima?
nawashauri tu baada ya kuona malalamiko yamezidi wakati serikali ni yao
 
Habari za Muda huu wana Jfs.

Ni muda sasa wa takribani mwezi kumekuwa na introduction ya kile kinachoitwa tozo ambapo kwa mujibu wa Mh Rais Samia kupitia Waziri Wake Dr Mwigulu nchemba na wabunge wake wanadai ni kwa ajili ya solidarity funds ili kusaidia miradi mbali mbali ya kijamii kama elimu na afya
vp na yale mabadiliko ya kwenye simu waliyotaka kufanya wakahairisha, walisema mpaka tarehe ngapi vile? au ndo hayahaya mambo yao ya tozo?

Hivi hizi pesa zote wanapelekaga wapi? mbona kila kukicha nchi ni ileile haikaribii hata south africa?
 
vp na yale mabadiliko ya kwenye simu waliyotaka kufanya wakahairisha, walisema mpaka tarehe ngapi vile? au ndo hayahaya mambo yao ya tozo?

Hivi hizi pesa zote wanapelekaga wapi? mbona kila kukicha nchi ni ileile haikaribii hata south africa?
Tunasubiri wazalendo tutatoa tu hakuna namna
 
Serikali iliyopita ilitumia pesa vibaya nchi haina pesa lazma sisi wenyewe tufunge mkanda kujenga nchi yetu.
Mleta mada shauri tupate wapi pesa !? Vinginevyo funga domo nchi ijengwe.
Nchi hii itaendelea kulipa gharama ya utawala mbovu wa magufuli kwa miongo kadhaa
 
Back
Top Bottom