wana JF ARUSHA Mliokwisha Kuoa/kuolewa; Ombi Langu la dhati kwenu

mimi nipo dar ila naeza kuja kukusaidia sijaolewa lakini. si umepata wa kiume? nitasimama nae au?

Bebii,
Nilishasema kule juu kuwa hakuna sharti katika ndoa linalosema msimamizi lazima awe ameoa au ameolewa...so kama upo tayari kumsaidia jamaa we m-PM tu ili ujue atakupokea vipi.
 
Bebii,
Nilishasema kule juu kuwa hakuna sharti katika ndoa linalosema msimamizi lazima awe ameoa au ameolewa...so kama upo tayari kumsaidia jamaa we m-PM tu ili ujue atakupokea vipi.
huyo msimamizi wa kiume ana mvuto?
 

Mkeshaji naomba nitofautiane na wewe kidogo
Msimamizi wa ndoa sio show off wala sio suala la kuchukua mtu ambaye hajaoa au hajaolewa
Sio suala la kwenda kuchukua mtu ambaye haijui ndoa wala hajawahi kuwemo kwenye ndoa kuwa msimamizi wa ndoa yako
Sio suala la kuchukua mtu ni mtu hata mnayetofautiana madhehebu kuwa msimamizi wa ndoa
Msimamizi sio anatakiwa tuu asimame pale mbele aonekane kwa kuvaa suti na gauni zuri kwa kuwa ni mpambe wa bwana na bibi arusi
Nenda kwa watu wanaojua thamani na kazi za msimamizi wa ndoa watakuambia ni nini kazi na thamani ya msimamizi wako wa ndoa
Ana majukumu zaidi ya unavyofikiria na sio kusimama pale mbele ya wafunga ndoa tuu kushuhudia ndoa yako ila ni zaidi ya hapo
Ana jukumu kwanza la kuw amsiri maana yeye ndie atakayepelekewa matatizo yote ya ndoa iwapo yatatokea. Atakuwa msuluhishi wa migogoro yote ya ndoa yenu. Kuna mambo ambayo yakitokea ndani ya nyumba mke anaweza kwenda kumweleza mzimamizi wake wa ndoa au mume kwenda kumweleza msimamizi wake wa ndoa sasa kama hata hawaishi pamoja au haawajui hata ndoa ni nini hapo watakupa ushauri gani
Mnasema wasimamizi wawe hata hawajaoa sasa watu ambao hawajaoa unategemea wawashauri nini watu ambao wanaingia kwenye ndoa
Sipingi kwamba ambao hawajaoa wanaweza kutoa ushauri ila tuangalie na taasisi ya ndoa ina mambo mengi ambayo yanatakiwa yasuluhishwe na watu ambao washaingia kwenye ndoa
Na inashauriwa hata wasimamizi wa ndoa wawe ni watu ambao wamefunga ndoa muda mrefu kiasi sio wale ambao ndoa zao ni changa
 
kwa iyo sifai?
 

Mkuu,
ukisoma vizuri post yangu hicho ndicho nilichokiandika,
Niliposema kuwa hayo mengine ni "show" sikumaanisha kuwa watu wakafanye show, lakini nilimaanisha kwa mfano kijana ni mweupe anapolazimisha kutafuta msimamizi mweupe na mrefu mathalani kama yeye bila kujali vigezo vya msingi kama ulivyoelezea hapo juu.....hiyo ndo show niliyomaanisha. Na tukubali, tukatae ndoa za vijana wa sasa ndo ziko hivo.
 

mkuu nimekupata
Wanasahau maana nzima ya msimamizi wa ndoa wanangalia morphology ni mrefu au mwembamba au mnene au ni mzuri kupita wakati hio sio dhana nzima ya msimamizi
Msimamizi ni mtu wa muhimu sana kwenye ndoa na sio hizi show off tunazoziona sasa
Na ndo maana ndoa nyingi zinatetereka kwa sababu hawana hata watu wa kuwashhauri
Imagine mzimamizi wako wa ndoa ni mtu ambaye hana ndoa atakushauri lipi kama sio kukuambia achana na huyo mwanamke au mwanaume tukale raha tena anakuambia kuwa single ni bora acha kufungwa fungwa na ndoa
 

nashukuru mkuu nimejaribu hili mara kadhaa,but wengi wa niliowaomba msaada wamekuwa na wakati mgumu kupata ridhaa ya mume kutokana na sababu ambazo ziko nje ya uwezo wangu..but nitazdi kujaribu
 
pole kwa mtihani mkuu...nakushauri ukae na familia yako mlijadili hili kwani nina imani watakupa mawazo ya nani asimamie ndoa yako kutoka kwenye familia/ukoo wenu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…