Cha msingi kwenye stori ni ONYO tu. Hii stori ilikuwepo around the street but ishapuuzwa kitambo.Kawaida hapa SAUT mtu akipotea ama kufariki uongozi unahusika kusafirisha maiti ama kutoa taarifa za upotevu kwa jeshi la polisi ili kushirikiana katika kumtafuta lakini kwenye stori hii hakuna kitu kama hicho.Uongozi ulifanya initiation ya kufanya utafiti lakini hakuna mtu mwenye fact. Pia uongozi ulitoa muda kwa waliokuwa wanamfahamu mtu huyo,kutoa taarifa ili kama ni kweli ndugu zake waambiwe,Je hata waliokuwa wanakaa nae hostel wasingeripoti suala la rafiki yao kutojulikana alipo? Suala la kutokujulikana kozi aliyokuwa anasoma its illogical na hata muda huu ukienda kwa Dean of Student (Mama Nasania) haamini suala hilo.Kama mwenye uzi hana shaka,namwomba azilete upya taarifa hizo pamoja na huyo binti aliyemwambia kwani naamini alimjua japo kwa jina moja tu.Vinginevyo wanajf tuendelee kumwombea Kaka Ulimboka.