Wana macho lakini hawaoni, wana masikio lakini hawasikii. CHADEMA wana macho? Je, wawasamehe Wabunge 19 wabarikiwe, au wakomae nao walaaniwe?

Kwani wakisamehewa Chama kitakuwa kimepoteza kitu gani kikubwa ??!

Makamanda walikipigania sana chama chao before that evil took place !!

Duniani hakuna mkamilifu !!
Muwasamehe tu nanyi mutasamehewa na mutabarikiwa !! 🙏🙏
 
Mhaini hasamehewi kumsamehe ni sawa na kukaribisha uhaini zaidi au kuwambia kuna watu ni bora au wana nguvu kuliko chama. Mtu akifanya uhaini, haijalishi ni nani ni afadhali aondoke
 
Kwani wakisamehewa Chama kitakuwa kimepoteza kitu gani kikubwa ??!

Makamanda walikipigania sana chama chao before that evil took place !!

Duniani hakuna mkamilifu !!
Muwasamehe tu nanyi mutasamehewa na mutabarikiwa !! 🙏🙏
Kumsamehe mhaini ni kumwambia yeye ni mkubwa kuliko chama na ni untouchable. Hii itasababisha uhaini mwingine huko mbeleni. Hata CCM haiwezi kulikbali hili. Ni afadhali liwalo na liwe ila wasiwasamehe.
 
Anyway mimi nilikuwa rafiki wa late kaka yake Mbowe wakianzia Splendid na mzee Mbowe kabla ya kuuza eneo na kuhamia huko.
Turudi kwenye mada, "Rafiki wa leo ni adui wa kesho", Mbowe alipofutiwa kesi wewe mwanasheria msomi bado ulishikilia hoja ya Mwanza eti unaushahidi wa ugaidi wa Mbowe! What a friend!
 

Nimesoma andiko lako. Ila naomba nikushauri Jambo moja. Usipende kila mara kumuhusisha Mungu kwenye mambo ya kijinga.
 


kwa makini nimesema nini kuhusu mimi na Freeman
View: https://youtu.be/fxDX_gk

Jitahidi%20kutokuwa%20bias%20itakusaidia%20sana.
 
Jamaa ni kada wa Ccm na mmoja wa watia nia wa ubunge na nafasi nyingine za kisiasa, hivyo lazima ajitengenezee mazingira ya kuonekana hayupo nyuma sana kwenye kuunanga Upinzani Chadema hasa hasa kama makada wenzake.

Hivyo zoea tu haya mabandiko yake.
 
Ila sometimes majina yana special attachment na mwenye jina. Mayalla maana yake njaa. Kwa hivyo tusimlaumu sana Mzee Mayalla itakuwa njaa inamsumbua sana
 
1. Of course, kupigania au kutetea haki za watu ni jambo muhimu kiongozi. Hata mimi napenda iwe hivyo. In fact, ndiyo matakwa ya kila mtu mwenye mapenzi mema - haki itendeke - kila upande utende haki na utimize wajibu wake.
2. Lakini kwa hili suala la Chadema na ex-wanachama wao inabidi kuliangalia vizuri bila kuwa 'biased'.
3. Hao akina dada nilipenda sana michango yao na hata baada ya kuwa kwenye hili tatizo waliendelea kutoa michango mizuri bungeni.
4. Hata mimi nilisikitika sana nilipoona kwamba pande zote mbili zilishindwa kukutana/kupata mwafaka maana nilitamani wabaki upande huu ili serikali iendelee kupata mchango mzuri kutoka upande wao kama chama.
5. Kwa upande mwingine, kama ni kweli waligushi barua na sahihi ili waapishwe as if wamependekezwa na Chadema katika kipindi ambacho walitakiwa kusimama pamoja siwezi kuona kama kosa lao ni dogo na la Chadema kutowasamehe ndilo kubwa zaidi. Hata kama tungewapima kwa kutumia kanuni ya kusema ni upande gani tunaweza kusema walichokifanya ni 'lesser evil' sidhani kama upande wao una merit hiyo 'lesser evil' kwa sababu Chadema waliamua kama walivyoamua kutokana na kuona kwamba "wamesalitiwa" na in this case usaliti unaharibu kanuni zote (kama kweli walisaliti).
6. Kama Chadema waliwapa hizo barua na kuzisaini na kubariki uteuzi wao kama Chama na baadaye wakatudanganya kwamba hawajawahi kufanya kitu kama hicho, hapo Chadema ni wa kulaumiwa muda wote mpaka watakapokuja tena hadharani na kutuomba radhi kwamba walitudanganya.
7. Otherwise, bado kwa maoni yangu natoa the benefit of the doubt kwa pande zote, ila kama kuna upande unatudanganya unatukosea sana. Kama pande zote ziko sahihi, then ni muhimu kupata reconciliation sehemu ambayo kumetokea misunderstandings.
8. Kwa vile sina chama na sina upande wa kuegemea, hata mimi nasema napenda kutetea haki ambayo pia inaambatana na wajibu.
 
Tumia uamuzi wa haki, mahakama. Tukumbuke kuna wakati baadhi yao waliomba watoke mahakamani ili wajadiliane na kuomba msamaha lakini kuna wanaojiona viongozi wao waliendelea kuwachuuza wasio na sauti.
 
Tumia uamuzi wa haki, mahakama. Tukumbuke kuna wakati baadhi yao waliomba watoke mahakamani ili wajadiliane na kuomba msamaha lakini kuna wanaojiona viongozi wao waliendelea kuwachuuza wasio na sauti.
Mbona mahakama ilisema uamuzi wa kamati kuu wa kuwafukuza ulikuwa sawa au mahakama haikuwatendea haki?
 
Nimeandika hivyo kutokana na wewe kuwapa 50 50 kwenye shauri lao, mahakama ilitoa 100 kwa Chadema.
Mimi nimesema sina upande ninaoegemea, hivyo siwezi kuegemea upande wa X dhidi ya Y. Lakini kwa vile kuna tuhuma kwamba waligushi barua na sahihi, ndiyo maana nikasema kama hiyo ni kweli, hawawezi kustahili kanuni ya 'lesser evil' na kuona Chadema ndio hawakutenda haki. Kwa sababu tatizo la jambo hili kwa maoni yangu chanzo siyo Chadema, bali ni kuapishwa kwa hao wabunge waliodai walipata baraka zote kutoka kwa chama chao, wakati chama chao kinadai hakijawahi kufanya kitu kama hicho. So, 50:50 ni katika mkutadha kwamba kama madai ya kila upande hayajapatiwa ufumbuzi. Lakini kama kuna upande uligushi na kutuaminisha kwamba walichokifanya kilikuwa na baraka za chama wakati siyo kweli, kwa kutumia the principle of double effect, "the lesser evil" iko upande wa Chadema (kama kuna eneo Chadema walikosea). In this case, kosa lao (kama lipo) kwa maoni yangu ni dogo sana ukilinganisha na kosa la upande wa hao 'ex-members' 19 walilolifanya. Anyway, sipendi kujadili mambo ya vyama kwa sababu siyo mzoefu sana katika hayo na nimejikuta nafanya hivi baada ya kutoa maoni yangu kwa maoni aliyoyatoa ndugu Paskali Mayala. Asante.
 
Figure of speech in quotation marks. Some kind of reward au mere gratification of the soul.

Nimesoma mada zako nyingi kuhusu CHADEMA na sijashawishika kuwa zinaandikwa na mtu mwenye nia njema kuhusu hicho chama na upinzani kwa ujumla. Ni kama mtu anaye-celebrate ubabe wa chama dola kwa wapinzani na wananchi kwa ujumla.

Kwanza, maelezo yako mengi huonyesha kuwa CHADEMA ina viongozi, wanachama na wafuasi wasiojitambua, wanaojisikia sana, wasiosikia mawazo mbadala, wabishi na wasio na mikakati ya maana. Na hiyo ni kero kubwa sana kwako. Umetoa tishio la karma kwao mara kwa mara.

Pili unawaaminisha kuwa “njia ya kwenda Ikulu” na kuondoa CCM i wazi kwao endapo watashirikiana na wapinzani wengine including some dubious characters. Pia wakimezea na kusamehe baadhi ya maovu hata uvunjifu wa katiba na ukiukaji wa sheria unaofanywa na dola.

Sihitaji kugusia kuhusu illegality ya masuala ya hao wabunge 19 waliofutwa uanachama na CDM wala illegality ya kesi ya ugaidi na
“msamaha” kwa Mbowe. Mitazamo yako ni questionable.

Sote pamoja na wewe tunajua kuwa CCM haina mpango wa kuruhusu uchaguzi huru na wa haki. Hizo bla bla kuhusu mkakati wa CDM kuingia Ikulu hazina mantiki yoyote. Kinachoonekana dhahiri ni janja ya kutaka kushusha kiwango cha brand ya CDM. Mienendo ya vyama vingine vya upinzani na viongozi wake inajulikana. Pendekezo la ushirikiano linaacha maswali. Hii kukubaliana moja kwa moja na mambo ya ovyo yanayofanywa na serikali ndio mwanzo wa viongozi wa CDM kuonekana “wamelambishwa asali”. Hata “maridhiano” wengi hatuyafurahii ingawa tunayaelewa kiasi fulani.

Kilicho dhahiri pia ni kuwa dola inachokoza kijanja (provoke) wapinzani ili wahamaki ipate fursa ya kuwagonga kwa kisingizio cha kulinda amani. Zile kamati na mahubiri mtiririko ya amani majukwaani na kwenye nyumba za ibada ni maandalizi ya kimkakati. Hatuna illusion kuwa eti CCM inaweza kuondoka madarakani kwa kura (vikaratasi) wala katiba (kijitabu). Hivyo tunaposoma mada za kuhimiza CDM ikubaliane na “nusu shari” ili iishi hata kwenda Ikulu tunajiuliza dhamira ya mwandishi ni ipi hasa?

Kitu pekee unachoweza kuisikitikia (CDM), kama kweli unajali, ni mtihani mgumu ilio nao wa kuingia kwenye uchaguzi mkuu katika mazingira yasiyokubalika kabisa. You may wish to put a word on that.

Mwisho kabisa sina shaka unajua vizuri sana kuwa mabandiko marefu yenye cross-references kibao ndio kile kinachoitwa “stringing people along”. Tutaendelea kukusoma hadi tufike huko unakotupeleka. Have a good day, Sir.
 
Naomba uheshimu hukumu ya mahakama kwamba walifukuzwa kihalali, huo ndiyo ulikuwa mwisho wa utata wa kufukuzwa kwao.
 
Naomba uheshimu hukumu ya mahakama kwamba walifukuzwa kihalali, huo ndiyo ulikuwa mwisho wa utata wa kufukuzwa kwao.
Si ndivyo nilivyosema au wewe unataka nisemeje? Soma vizuri tangu nilipoanza ku'post' hii post labda hapo utaelewa ninachokisema. In fact, nilitofautiana na Paskali Mayala anayeona Chadema hawakuwatendea haki. Nikamuuliza kama anaona kugushi barua na sahihi kwamba walipendekezwa na kupewa baraka za chama ni sahihi. Hoja imeanzia hapo. Sasa unaniambia nini, mkuu? Soma tangu mwanzo utaona ninasema nini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…