Hawa viongozi waliopo lazima wabadilishwe, ili uingie uongozi mwingine lakini sio timu akabidhiwe Dewji kama kampuni. Simba ni zaidi ya kampuni, inaweza kujiendesha kwa kutumia michango ya wanachama tu.
Tusijaribu kujifananisha na timu za ulaya kwani wao wana misingi ya uwazi sana kuliko sisi. Huyo Dewji atatumia simba kujinufaisha kibiashara, kama anapenda maendeleo ya simba agombee urais muda ukifika. Sio kumiliki timu na kama anapenda maendeleo ya soka, hizo bilioni 20 anaweza kuanzisha timu kama mwenzie bakhresa alivyofanya.