Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
nyie ndio wale makomandoo wa getini?Hapanaaa
Hawa viongozi waliopo lazima wabadilishwe, ili uingie uongozi mwingine lakini sio timu akabidhiwe Dewji kama kampuni. Simba ni zaidi ya kampuni, inaweza kujiendesha kwa kutumia michango ya wanachama tu.
Tusijaribu kujifananisha na timu za ulaya kwani wao wana misingi ya uwazi sana kuliko sisi. Huyo Dewji atatumia simba kujinufaisha kibiashara, kama anapenda maendeleo ya simba agombee urais muda ukifika. Sio kumiliki timu na kama anapenda maendeleo ya soka, hizo bilioni 20 anaweza kuanzisha timu kama mwenzie bakhresa alivyofanya.
Boss tupo kwenye MICHEZO mbona unatupeleka kwenye SIASA ! Wewe ni mbaguzi na hiyo ni dhambi kubwa sana Umesha leta ubaguzi kwamba SIMBA ni upinzani Ushindwe kwa jina Yesu .Simba timu ya upinzani hawezi kuuziwa uyo kada wa ccm mbunge mstaafu.
Wahenguzi walishanena.. "Ya Ngoswe Muachie Ngoswe"Mimi siyo mwanachama wala mshabiki wa timu ya Simba, lakini ukweli lazima usemwe.