Nasikitika kukuambia kuwa unashindwa kunielewa..lakni pia unashindwa kuelewa maana halisi ya kadi hizi za uawanachama..kwa jinsi navyoelewa hadi kufikia hatua ya kuwa unania ya kupata kadi inamaana uko tayari kwa lolote,,yani unakuwa miongoni mwa jamii husika..
Inapotokea timu inacheza ,,kama kweli wewe ni mwanasimba na unakadi hutaacha kwenda uwanjani kutazama chama lako ..labda uwe unaumwa ama upo nnje ya eneo kikazi..
Tofauti na shabiki..shabiki ni kama wale wanaobishana na kutoa maoni kama hivi tunavyofanya hapa kwamba nani aachwe nani asajiliwe..shabiki yeye kazi yake ni hiyo tu basi,,anaishia kuwaona wachezaji kwenye tv au magazeti,,sasa mtu kama huyu ni sawa na KUPE tu..
Wapo kweli mashabiki wanaojitoa kwa timu..timu hata iende wapi nao wapo ..timu hata iwe mbovu kaisi gani lakini yeye uwanjani lazima awepo ..mtu kama huyu ukichunguza kwa makini anakadi yake ya uanachama na anailipi kila mwaka..ndio maana anaona uchungu...
leo kama ni shabhi hapa utaona kuna wanaojiita mashabiki wa Simba hapa wanasema mtu kama Kotei eti aachwe,,ukimuuliza kwa nini sababu yao etu amechoka...?sasa unajiuliza yeye Kotei asichoke amaekuwa mashine au roboti?hao ndio mashabiki maandazi kazi yao ni kufuata upepo na hawana faida kwenye timu .
hao ni kupiga porojo ambao inatakaiwa ifie mahali mfumo uwateme