Wana Simba wenzangu zoezi la kuchangia uwanja Kama limekufa hivi

Wana Simba wenzangu zoezi la kuchangia uwanja Kama limekufa hivi

Nyuma ya michango Simba inamipango mikubwa sana ya kufanikisha hili jambo.
 
Itifak imezingatiwa,

Hili Jambo mbona Kama limekufa kibudu ,mitandaoni sioni hamasa yenye makali kabisa , Simba ilivyo na nguvu mitandaoni inashindwa Nini kutumia nguvu ya ushawishi ili hili jambo uwe Kama wimbo Taifa.

Au ndio wanatusahaurisha pole pole na pesa imeenda kwenye usajiri.

Haki niongee hapa Waz Waz kama hili Jambo halitafanikiwa viongozi wajiandae kunirudishia 50k yangu maana huu utakua Ni uhuni wa kutukuka.

Uzuri sms sijawahi kifuta ,haiwezekan watu tumeamua kujitoa Ila viongozi wanapooza hili swala yaan wanaliongea kwa kudokoa dokoa tu alafu wanakaa Kimya.

Viongozi kuweni serious msije tukwaza mashabik kwa hili Jambo weken msisitizo Kama mnavyoweka msisitizo kwenye mambo ya usajir .
Leo naishia hapa Ila hili swala naliona Waz kuwa tumepigwa na kitu kizito kichwan kwa mwendo huu wa Kobe hakuna uwanja hapa.
Swala la kujenga uwanja kwa staili kama ile halitafanikiwa..lipo kishabiki na sio kitaalam.
 
Ukweli mchungu ila mashabiki wa Simba na Yanga mchango wao ni kwenda uwanjani kuangalia mpira basi,mengine hawana mpango nayo.

Misimu miwili mlianzisha kadi kama za Yanga, huku mkishirikiana na DTB bank, gharama ilikuwa 19000 na kila mwaka mwanachama alipie 14000 sijui zoezi liliishia wapi. Hili la uwanja labda MO na baba yake wajikamue.
 
Back
Top Bottom