Wana Yanga SC muanze Kujiandaa 'Kisaikolojia' kwani huenda 'Viongozi' wenu baadhi wakayaanza Maisha mapya Jela Segerea

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
BENARD MORRISON KUMALIZA 'MASINEMA' YAKE NA YANGA

Shirikisho la kabumbu nchini Tanzania (TFF) limesema hukumu ya madai ya kughushi saini ya mchezaji Bernard Morrison itatolewa Agosti 10 baada ya kazi ya uchunguzi iliyofanywa na Jeshi la Polisi kumalizika.

Kiungo huyo mshambuliaji kutoka nchini Ghana aliishitaki Young Africans kwa TFF, akidai kuwa saini yake imefaniwa fojari katika mkataba wa miaka miwili, ambao klabu hiyo yenye maskani yake kwenye makutano ta mitaa ya Twiga na Jangwani jijini Dar es salaam, imeuwasilisha TFF na Shirikisho la kandanda duniani (FIFA).

Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF, Elias Mwanjala amesema kwa sasa wapo katika hatua za mwisho za uchunguzi wa suala hilo na hawana haja ya kuwa na papara ili kupata majibu sahihi.

Mwanjala amesema awali walipanga kutoa uamuzi wa suala hilo mwishoni mwa mwezi Julai na baadaye kupeleka mwanzoni mwa mwezi huu, lakini walishindwa kufanya hivyo kutokana na sababu mbalimbali zilizo nje ya uwezo wao.

globalpublishers

Kuna Watu walidhani ule 'Uhuni' wao waliokuwa wakiufanya wakati JK Yanga Mwenzao akiwa Madarakani basi na kwa JPM huyu watauendeleza tu.
 
Kama simba wamefanya uchunguzi ndiyo maana mnahukumu moja kwa moja lakin km siyo simba mtulie mbumbumbu fc ile tff ilete mrejeshooooo
 
ndio maana walitumia polisi kutaka kumnyang'anya simu yake ili wapandikize vitu vya uongo kumbe Morison mwenyewe mjanja
 
Mbumbumbu fc Porojo haziwasaidii, nyinyi mmemshawishi Morrison ajiunge na timu yenu bila kuwasiliana na yanga,mnakwenda kulipa gharama bila chenga na Morrison ataendelea Kubaki jangwani mpango wenu umefeli mjiandae kulipia gharama za umbumbumbu wenu.
 
Baada ya majibu kutoka manyani fc sijui tutawaita jina gani maana kila siku wanapata majina mapya
 
Swala la huyu mwamba Morrison, nshaanza kuhisi harufu yakufikishwa kunako FIFA..
 
Swala la huyu mwamba Morrison, nshaanza kuhisi harufu yakufikishwa kunako FIFA..

Nani sasa Yeye Mkweli Morrison au 'Wahuni' Viongozi wa Yanga SC 'waliofoji' saini yake? Wewe hujiulizi tu kuwa kwanini Mchezaji anajiamini hivi?
 
Nani sasa Yeye Mkweli Morrison au 'Wahuni' Viongozi wa Yanga SC 'waliofoji' saini yake? Wewe hujiulizi tu kuwa kwanini Mchezaji anajiamini hivi?
Mkuu Gentamycine thus why nmesema hivyo na hata swala la yeye kujiamini hivi nalo niliishaliona kwamba kuna kitu may be hakipo sawa au kipo sawa kwa pande zote au kwa upande mmoja,na ninachokiona hapa hao Yanga sidhan kama watakubaliana na maamuzi negative ndo maana nmejaribu kuhisi hiyo harufu,but kama kweli Yanga walighushi sahihi itakuwa si kitu cha kiungwana hata kidogo mchezoni.
 
Takukuru wameanza kuwachunguza Gsm kwa utakatishaji wa fedha kwa kudai wamelipa mamilioni kwa Morison kumbe wamefoji sahihi na mkataba series bado inaendelea
 
Mbumbumbu fc Porojo haziwasaidii, nyinyi mmemshawishi Morrison ajiunge na timu yenu bila kuwasiliana na yanga,mnakwenda kulipa gharama bila chenga na Morrison ataendelea Kubaki jangwani mpango wenu umefeli mjiandae kulipia gharama za umbumbumbu wenu.
Minyani fc bhana mchezaji hatak kuendelea na nyie mnamng'ang'ania. Aibu sana. HEBU CHEKI ILE DHARAU YA KUBADILISHWA PALE UWABJANI
 

Kwani Wewe hii tabia ya 'Kihuni' ya Yanga SC Kufanya hivi ndiyo umeanza Kuijua leo Mkuu? JK katika 'Utawala' wake aliwaharibu mno hawa Yanga.
 
Takukuru wameanza kuwachunguza Gsm kwa utakatishaji wa fedha kwa kufai wamelipa mamilioni kwa Morison kumbe wamefoji sahihi na mkataba series bado inaendelea

Kesho kuna Watu huenda ( nasisitiza tena neno huenda nikiwa sina uhakika wa 100% ) hasa baadhi ya Viongozi wa Yanga wakalala Lupango Dar.
 
Morrison alikamatwa na polisi juzikati na kupelekwa kituoni kwa mahojiano, baada ya kuandikishwa maelezo kutia sain ya kuyakubali maelezo yake pale tayari kilakitu kilipatikana. Tayari sain yake itakwenda kulinganishwa na ile aliyo mwagika katika mkataba wa GSM. Mbumbumbu mkiambiwa Yanga ni Taasisi kubwa hamwamin Sasa subirini. Waalimu wa Morrison apa Tanzania ni Mbumbumbu fc ambao hawajui wanancho kifanya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…