Pre GE2025 Wanachama wa ACT Wazalendo wakamatwa kwa kufanya fujo kwenye Vituo vya Uandikishaji Zanzibar

Pre GE2025 Wanachama wa ACT Wazalendo wakamatwa kwa kufanya fujo kwenye Vituo vya Uandikishaji Zanzibar

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Kama ambavyo niliwapa habari awali juu ya zoezi la Uandikishaji kwenye Daftari la wapiga kura Mkoa wa Kusini Unguja kuanzia tarehe 08/03/2025 hadi tarehe 13/03/2025; zoezi ambalo Jeshi la Polisi lilikuwa na dhamana ya ulinzi na Usalama wa vifaa, watendaji wa Tume, mawakala wa vyama, wananchi ambao ndio walengwa walipewa fursa kwa mujibu wa sheria kujiandikisha/kuhakiki taarifa zao tayari kwa ajili ya kutimiza haki yao ya kikatiba kuwachagua viongozi wao akiwepo Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wah. Wawakilishi wa Baraza la wawakilishi na Wah. Madiwani: nilitoa tahadhari kwa Umma wasijitokeze watu ama kikundi cha watu kuvuruga zoezi hilo muhimu kwa taifa letu.

Leo nimewaita kuwapa taarifa juu ya hali ya Usalama katika zoezi hilo kama ifuatavyo;-

Kwa ujumla zoezi zima lilikuwa salama wananchi wenye sifa walipata fursa ya kujiandikisha katika Daftari la wapiga kura kupitia vituo vilivyoainishwa katika shehia zao.

WILAYA YA KATI UNGUJA.
Katika Wilaya ya Kati zoezi hili lilifanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 08/03/2025 hadi tarehe 10/03/2025 na hapakuwa na changamoto za kiusalama zilizojitokeza na zoezi lilienda vizuri.

WILAYA YA KUSINI UNGUJA.
Katika Wilaya ya Kusini zoezi lilifanyika kwa siku tatu kuanizia tarehe 11/03/2025 hadi tarehe 13/03/2025. Katika Wilaya hii kwa ujumla wake lilifanyika kwa utulivu na amani ingawa kuna matukio machache yaliyoripotiwa katika vituo vya Polisi kama ifuatavyo:-
  • KUZUIA WATU WASIJIANDIKISHE.
  • Tarehe 11/03/2025 majira ya saa 4:30 asubuhi huko Jambiani Kibigija wanachama watatu wa ACT WAZALENDO walisimama kwenye njia ya kuingia kwenye kituo cha kujiandikisha na kuwazuia wasijiandikishe kwa madai kuwa watu hao wana asili ya Tanzania Bara huko wakijua kuwa hawana mamlaka ya kufanya hivyo watu hao ni:-
  • RAMADHAN HASSAN RAJABU, 58 yrs, Mshirazi, Mvuvi wa Jambiani Mzuri.
  • MOHAMED PANDU VUAI, 43 yrs, Mshirazi, Mvuvi wa Jambiani Mzuri.
  • AMEIR KISHAJI AMEIR, 60 yrs, Mshirazi, Fundi Mwasi, Mkazi wa Jambiani Mzuri.
Watuhumiwa wote watatu walikamatwa na kuhojiwa na kukiri kufanya hivyo wakiamini kuwa watu waliokuwa wakiwakamata na kuzuia wasiingie kujiandikisha walikuwa hawana sifa.
  • KUWANYANG’ANYA WANANCHI VITAMBULISHO.
  • Mnamo tarehe 11/03/2025 majira ya saa 03:30 asubuhi huko Nganani Makunduchi katika eneo la uandikishaji wapiga kura, wanachama wa ACT WAZALENDO waliwakamata watu wawili na kuwanyang’anya vitambulisho vya Mzanzibar watu hao wanatafutwa na Jeshi la Polisi ili wakahojiwe juu ya kitendo hicho ambacho lengo lake ni kuvuruga zoezi la uandikishaji; walionyang’anya vitambulisho ni EMMANUEL KINYAJA SAPILI, 42 yrs, Mkazi wa Nganani Makunduchi na Mkewe ELIZABETH KULWA, 21 yrs

  • KUZUIA WATU WASIJIANDIKISHE.
  • Mnamo Tarehe 11/03/2025 majira ya saa 3:30 asubuhi huko Muyuni ’A’, mwanachama mmoja wa ACT WAZALENDO aitwaye KHAMIS HAJI JUMA, 56 yrs, Mshirazi WA Muyuni ’A’ bila mamlaka aliwazuia wafanyakazi wake kwenda kujiandikisha kitendo ambacho ni kuwanyima haki yao ya kikatiba: Wafanyakazi hao ni;- EMASON ARIN YINGA, 25 yrs, Muha, Mkazi wa Muyuni na mwenzake ISSAYA s/o WILBERT ZINJIBAR, 37 yrs, Muha, Mkazi wa Muyuni ’A’. Mtuhumiwa amekamatwa na kuhojiwa.

  • KUFANYA FUJO KWENYE KITUO CHA KUANDIKISHA WAPIGA KURA.
  • Mnamo tarehe 11/03/2025 najira ya saa 05:30 asubuhi huko kituo cha kuandikishia TASAN mwanachama ALLI s/o ABDALLA MKWENDE alifanya vurugu kwa kutoa lugha za vitisho na kuwapiga picha watendaji wa kituo hicho kitendo ambacho kililenga kuvuruga zoezi la uandikishaji. Mtuhumiwa alikamatwa na kuhojiwa.
Hali ya ulinzi kwa ujumla imeimarishwa na leo tunahitimisha zoezi hili katika Mkoa wa Kusini Unguja.

Imetolewa na:-
Daniel E. Shillah-SACP,
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Kusini Unguja.
 
Hao ex-CUF members fujo za nini huko zenj? Watulif hilo zoezi la uandikishaji likamilike. ACT WAZALENDO wa bara hawana munkari
 
Back
Top Bottom