Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
- Thread starter
-
- #21
Stalin...Huwa ni makusudi au niaje?
Theme moja ila ina maandiko zaidi ya 50+......
Ushaiandikia kitabu, Umeshaiandikia Journals na mabandiko kibao.
Je Tanganyika na Tanzania zilikoma baada ya Hapo.
Kama lengo ni kupeana historia, kuna theme Nyingi za kuzungumza, vitu vingi vya kuzungumza.
Lakini hujataka kufanya hivyo, kwa umri wango ungeweza hata kutusaidia Historia Nyingine, kama Vita ya Kagera, kuingia kwa vyama Vingi, privatization etc.
Ila umekomaa na Theme moja kila siku, haielimishi Tena, its annoying.
Karne,Kwa nini majina ya Sykes na hao wazee wengine akina Chamwenyewe hayapo tena kwenye siasa na uongozi wa nchi hii.
Finally umekubali kwa mdomo wako, umebobea katika uislamu na Siasa.Stalin...
Kwani hairuhusiwi kwa mtu kuwa na "specialisation?"
Au hujui umuhimu wa mtu kuwa bingwa katika somo moja?
Ikiwa huu uzamivu wangu katika Uislam na Siasa unakuudhi acha kusoma.
It is this simple.
Asante kushukuru, but why iwe kwa kusema waislamu na si Watanganyika wenzake bila kujinasibisha na mrengo wa dini, the fact Tanganyika ilikuwa na watu wa dini tofauti na geographically it happened Colonial master's had established head quarterly in DSM where slave trade descendants had settled, most slaves came from the interior, very often am skeptical of being ego with religions because of the devastating past history.Wad....
Ahsante sana.
Maneno hayo yako aliyasema Jonathon Glassman wa Northwestern University, Evanston, Chicago alikonialika kuzungumza.
Katika neno la shukurani alisema kuna mengi hakubaliani na mimi lakini alichojifunza kutoka kwangu ni ukweli kuwa Nyerere alifika pale alipofika katika kupigania uhuru wa Tanganyika kwa msaada mkubwa wa Waislam.
Stalin...Finally umekubali kwa mdomo wako, umebobea katika uislamu na Siasa.
Na si historia kama unavyopenda kujipambanua.
Kuanzia sasa nikikusoma nitaelewa hii ni "persepective" ya Siasa ya kiislamu.
Na si historia.
Wad...Asante kushukuru, but why iwe kwa kusema waislamu na si Watanganyika wenzake bila kujinasibisha na mrengo wa dini, the fact Tanganyika ilikuwa na watu wa dini tofauti na geographically it happened Colonial master's had established head quarterly in DSM where slave trade descendants had settled, most slaves came from the interior, very often am skeptical of being ego with religions because of the devastating past history.
It was not good na bado ni vibaya kutokuwataja bayana na kuwaweka kwenye kumbukumbu sahihi wapigania uhuru wote kwanzia TAA, TANU, CCM katika ngazi mmoja mmoja, wilaya, mikoa, kata, vikundi, familia, na aina ya mchango wao, Kila aina ya historia, nafahamu religious aspect ni muhimu hasa kama dhana ya ukusudi wa kutengwa, ama kusalitiwa. But generally speaking uko vizuri sana [emoji120][emoji120][emoji120]
Lakini wewe ni mtaalamu wa siasa ya dini ?Stalin...
Lini nimekataa hilo?
Kitabu changu cha kwanza kuandika: "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," (1998).
Hii ni "political history.'
Ninachikataa ni kuwa naandika dini.
Nikikuwekea vitabu na paper zangu zote ni political history.
Ukipenda angalia catalogue ya Library of Congress (1998), "Dictionary of African Biography," (2011) wananielezaje au "Nyerere Biography," (2020) wanasema nini kuhusu Mohamed Said.
Stalin...Lakini wewe ni mtaalamu wa siasa ya dini ?
Unaweza rejea comment yako pale juu mzee wangu.Stalin...
Nimesoma Political Science sina elimu ya dini.
Stalin...Unaweza rejea comment yako pale juu mzee wangu.
Uliposema wewe una uzamivu katika Dini?
Labda sikukuelewa....Stalin...
Kwani hairuhusiwi kwa mtu kuwa na "specialisation?"
Au hujui umuhimu wa mtu kuwa bingwa katika somo moja?
Ikiwa huu uzamivu wangu katika Uislam na Siasa unakuudhi acha kusoma.
It is this simple.
Stalin....Labda sikukuelewa....
Ulimaanisha nini uliposema
"Uzamivu wangu katika siasa na Uislam"
Naomba nifahamishe kijana wako.
Naonekana kama narudia swali, ila si kweli.Stalin....
Mimi ni nani nini elimu yangu maswali haya nimeyajibu miaka 10 iliyopita.
Sielewi kwa nini hapa watu wanalazimisha kunipa sifa nisizokuwanazo.
Kwa kejeli wakiniita Mufti, Sheikh, Ustadh nk.
Nami nikiwajibu kuwa mimi ni mtu kama walivyo watu wengine JF.
Hawakutaka.
Sasa na wewe hili la elimu ya dini ambayo sikusoma umelipenda.
Nimesoma Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam (Political Science)na University of Wales, Cardiff (Maritime Studies).
Nimeandika vitabu kadhaa na kutiwa katika miradi mikubwa ya historia na wachapaji vitabu maarufu Oxford University Press Nairobi na New York nk.
Nimealikwa vyuoni kuzungumza Afrika, Ulaya na Marekani.
Sijapata kusimama kwenye membari ya msikiti wowote kuhubiri Uislam kwa kuwa mimi si sheikh.
Hapo chini picha yangu na hiyo ndiyo ilikuwa haiba yangu nyakati hizo.
Stalin...Naonekana kama narudia swali, ila si kweli.
Swali nalouliza sijibiwi.
Nilichouliza ni hichi.
Ulimaanisha nini uliposema
"Uzamivu wangu katika siasa na Uislam"...
nI hii maana tu ndio naihitaji.
Nadhani unafanya kusudi.....Stalin...
Historia ya uhuru wa Tanganyika ni historia ya wazee wangu na inaanza 1924.
Historia hii ni historia ya vipi Waislam walikuwa mstari wa mbele kupambana na ukoloni wa Mwingereza.
Wakaunda African Association 1929 kisha Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika 1933 wakahitimisha na TANU 1954.
Baada ya uhuru kupatikana 1961 ilipoandikwa historia ya Tanganyika historia yote ikawa anatajwa Julius Nyerere peke yake.
Si hili tu yakawa yapo na mengine yaliyowasibu Waislam.
Nikaamua kutafiti na kuandika historia hii ambayo leo mnaisoma ndani ya kitabu cha Abdul Sykes, ndani ya Cambridge Journal of African History na ndani ya Biography of African History na vitabu vingine nilivyoandika vinakaribia 10.
Stalin...Nadhani unafanya kusudi.....
Sikuhitaji kuskia habari za Tanganyika wala Sykes.
Nilichotaka kufahamu ni nini ulimaanisha uliposema.
" Uzamivu wangu katika Siasa na uislam "
Hichi pekee ndio nilichotaraji kuskia.
Kazi ipo....Stalin...
Kwa nini unaghabika?
Naamini uko hapa kwa mazungumzo si kwa ugomvi.
Mimi siwezi kujua nini unapenda kusiki kutoka kwangu na kipi hutaki kusikia.
Wala siwezi kukujibu kwa namna ya wewe ufurahi.
Labda unidokeze unataka kujua nini khasa kutoka kwangu.
Elewa kuwa niko hapa JF kwa zaidi ya miaka 10 najibu maswali ambayo mengine wewe kwa kuwa hunijui unyarejea kuniuliza.
Kuna waliokutangulia waliokataa kuwasikia Sykes katika historia ya Tanganyika 1962 leo baada ya miaka 60 wanasoma historia yake na imebadili historia yote ya uhuru wa Tanganyika.
Wengi wamepata kuniuliza: ''Imekuwaje TANU Card No. 3 ni ya Abdul Sykes, TANU Card No. 2 ni ya Ally Sykes na TANU Card No. 1 ni ya Julius Nyerere lakini historia hii ikawa haifahamiki imefutwa?''
NIngeweza kukueleza mengi lakini tusimame hapa kwa sasa.
Stalin...Kazi ipo....
Mohamed, ni kweli kuna vitu vingi unavifahamu, hisipokuwa una ugojwa wa Uislamu!! Mchango uliotolewa na mtu bila kujali ni Muislam au Mkiristo usiupeleke kwenye udini. Mchango huo ukitolewa kitaasis hapo una haki ya kuingiza huo Islam, lakini kama mtu binafsi hapana.Wad...
Historia ya Waislam na ukoloni wa Wajerumani na Waingereza ni wa kipekee.
Kipekee kama vile ilivyo historia ya Wakikuyu na ukoloni wa Waingereza.
Wakikuyu walikuja kwanza na Kenya African Union kisha wakaibuka na Mau Mau kisha KANU.
Waislam walianza na African Association kisha wakaibuka na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika kisha TANU.
Matukio haya yakawa "field of inquiry," kwa wasomi na wanafunzi wa African History.
Historia ya uhuru wa Kenya na Wakikuyu na Mau Mau imeandikwa sana.
Ila historia ya Tanganyika na Waislam na umoja wao kupambana na ukoloni haikuguswa.
Ndiyo sababu nilipotokea Mimi kuiandika ikapata umaarufu mkubwa katika vyuo vikuu vingi duniani.
Mbussi,Mohamed, ni kweli kuna vitu vingi unavifahamu, hisipokuwa una ugojwa wa Uislamu!! Mchango uliotolewa na mtu bila kujali ni Muislam au Mkiristo usiupeleke kwenye udini. Mchango huo ukitolewa kitaasis hapo una haki ya kuingiza huo Islam, lakini kama mtu binafsi hapana.