Wanachama wa Simba 'Aggy Simba' na Dkt. Mohammed wafungiwa kujihusisha na klabu kwa muda

Wanachama wa Simba 'Aggy Simba' na Dkt. Mohammed wafungiwa kujihusisha na klabu kwa muda

Kazi kweli kweli kwenye mambo ambao yanagusa ugali wa mtu basi sheria inafanya kazi ila sheria za kuwaondoa madakani kwa kuboronga hapo sheria hazionekani.Tusishangae mashabiki tukapewa kesi za kuwa sisi ndiyo tumesajili pia wachezaji wabovu.
Comrade, hii hoja ulitakiwa kuitoa siku ile ya mkutano wenu mkuu. Ila ndiyo hivyo tena; lile pilau la Mangungu na ule ujio wa Manzoki kama mshereheshaji mkuu wa mkutano! Ukawatoa kabisa kwenye reli.
 
IMG-20240614-WA0010.jpg
 
View attachment 3018243
Aggness Daniel (Aggy Simba)
View attachment 3018251
Dkt. Mohammed

Sekretarieti ya Klabu ya Simba imewafungia kujihusisha na masuala ya klabu Wanachama Mohamed Khamisi Mohamed maarufu Dr. Mohammed na Agnes M. Daniel maarufu Aggy Simba mpaka pale kamati ya maadili itakapoamua vinginevyo.

Sekretarieti imepokea malalamiko mengi ya kimaadili dhidi ya Wanafamilia hao wa klabu ya Simba ikiwemo kuitisha mikutano kinyume na taratibu na kuchochea migogoro ndani ya Klabu.

Sekretarieti itawafikisha Wanachama hao mbele ya Kamati ya maadili hivi karibuni.

Uamuzi huo umefikiwa kwa Mamlaka ya Sekretarieti iliyonayo chini ya Ibara ya 31(4)(g) ya katiba ya Simba ya klabu ya 2018 (kama ilivyofanyiwa mareke- bisho 2024), katika kuhakikisha Mahusiano ndani ya Klabu, Wanachama, na Mashabiki hayaathiriwi.

Sekretarieti inawakumbusha wanachama na mashabiki kuheshimu Katiba, Kanuni, na Miongozo iliyopo ndani ya Klabu.

Imetolewa na Sekretarieti, Simba Sports Club Juni 15, 2024


View attachment 3018081
Ngoja inyeshe.
 
Kuna taratibu za kuitisha mkutano wa dharula, swali je wanachama Hawa waliufata Kama hawakufata walikuwa na malengo gani? Huenda walikuwa wanatumiwa na watu kwa malengo yao Ila ngoja tusikilize na upande wa pili.
 
Sijawahi kumkubali Mangungu wala Salim ila huyo Mohamed naye anajikutaga kama msemaji wa timu, alitakiwa afungiwe siku nyingi sana au apewe onyo kuiongelea klabu kama vile ni msemaji wake.

Huyo Aggy naye alitakiwa awe amepewa onyo muda mrefu uliopita kwa tabia ya kuiba kila content ya Simba Instagram na kuiweka kwake bila kutoa credit.

Nasimama na kauli yangu ya muda mrefu kuwa itachukua muda mrefu sana Simba kuja kutulia tena na nina sababu zangu za msingi kusema hivyo. Hawa mashabiki wenye mvuto wote ni virusi tu, wananunulika na upande wowote kuyumbisha muelekeo sahihi wa timu.
 
Back
Top Bottom