Wanachama Yanga wachana na kuchoma magazeti ya Reginald Mengi!

Wanachama Yanga wachana na kuchoma magazeti ya Reginald Mengi!

Nilidhani wamewavamia wauza magazeti na kuyachoma,kumbe wameyanunua!!

Hili zoezi likiwa endelevu tena nchi nzima,Mengi atatengeneza pesa sana

Upumbavu ni kitu kibaya sana; hawa vilaza wanadhani kwa kuyanunua magazeti ya Mengi na kuyachoma ndio kumuadhibu, hawana uelewa kuwa kwa kfanya hivyo wanamuongezea mapato!!! Endeleeni na Manji wenu kununua Nipashe na Guardian kila siku na muwe mnayachoma!!
 
View attachment 349864
Wanachama wa Yanga wamecharuka na kufanya kitendo kinachoonyesha ni hasira kutokana na kuchana na kuchoma moto magazeti.
Wanachama hao wa Yanga, leo wamechoma moto magazeti ya Nipashena The Guardian katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye makao makuu ya klabu hiyo mtaa wa Jangwani na Twiga, Kariakoo jijini Dar es Salaam.


Wanachama hao wamefanya hivyo wakipinga Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji kusakamwa kw amakusudi na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi.
“Hii sasa imetosha, huyu Mengi na magazeti yake anamsakama Manji kila anapoona Yanga inafanya vizuri. Mara tu baada ya Yanga kutinga robo fainali hatua ya Kombe la Shirikisho, basi vyombo vyake vimeanza kuandika kwamba anatakiwa sijui kuondolewa Coco Beach.
“Hakuna asiyejua Manji amestaafu Quality Group, sasa anamtaja wa nini. Au anataka ashindwe kufanya kazi za Yanga kwa utulivu.


“Watuache, kweli tutatangaza watu wa Yanga waachane na kununua bidhaa zake,” alisema Abuu Chehekaheka.
Pamoja naye, wanachama wengine kama Edward Matiku, Clement Michael na Hashimu Mtanza nao walimuunga mkono pamoja na wengine waliokuwa pale kabla ya kuanza kuchoma moto magazeti hayo wakionyesha kuwa na jazba.

Hata walipoulizwa sababu kuu za kuchoma magazeti hayo yanayomilikiwa na Mengi, hakuna aliyetaka kujibu huku wakionyesha kuwa na jazba.

View attachment 349857View attachment 349858 View attachment 349859
Mkuu hebu tuwekee hapa uthobitisho wa gazeti la IPP linalo msakama Manji kuanzia January hadi May mwaka huu!
 
Huwa nikiona hivi namkumbuka mzee mmoja alikuwa anasisitiza sana ELIMU, ELIMU,ELIMU.....wanatumika vibaya
 
Back
Top Bottom