Wanachama Yanga wampigia magoti Yusuf Manji agombee tena uenyekiti

Wanachama Yanga wampigia magoti Yusuf Manji agombee tena uenyekiti

Lupweko

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2009
Posts
23,566
Reaction score
24,891
Katika mkutano wao mkuu, kilitokea kioja ambapo watu wazima walitokwa na aibu na kuamua kujidhalilisha hadharani kwa kuamua kupiga magoti na kumlilia YM ili kumuomba agombee tena uenyekiti. Bila shaka wamepiga mahesabu, mahela yote haya wameshindwa kulipa kisasi cha 5-0, badala yake wameendelea kupigwa tu 3-1, sasa je bila hela si zitakuwa 7-0 ??? Pia kuna maswali wanajiuliza, wamesajili mastaa kibao kutoka Simba kwa mikataba ya kuwalipa mishahara mikubwa mikubwa, sasa nani atakuwa anawalipa mishahara wachezaji? Watu wazima wenye watoto nyumbani wakaamua kumpigia magoti mtoto mdogo, lakini jamaa amegoma! Kazi kwenu Jangwani

attachment.php
 
Ndio tatizo la timu kushindwa kujiendesha zenyewe.
 
Ndio tatizo la timu kushindwa kujiendesha zenyewe.

ni kweli kabisa, hapa makomandoo walikua wanakula kilaini tu kwani mwenyekiti hana habari, ndio maana timu inaendeshwa kihasara
 
Mziray alishawaambia hizi timu zikijienda kuna watu watakufa njaa.
 
Mleta mada ni wa upande ule.
Usijadili mtu, jadili hoja. Je, si kweli kwamba watu wazima walipiga magoti kumuomba YM abadili uamuzi wake wa kutogombea tena uenyekiti?
 
Naomba uthibitisho wa hii habari kutoka kwa Makoye Matale na mandieta, maana huyo wa kushoto ni kama mmojawapo.

Hiyo ni dua ya kuiombea Yanga, sisi hatuendi kwa waganga kama Simba,tunapeleka shida zetu kwa Mungu wa mbinguni, ndiyo maana hata nilipoomba KCC iifunge Simba kamoja dua yangu iljibiwa. Habari ya mjini hii hapa: http://www.youngafricans.co.tz/news/localnews/5yan2simurqpik endelea pia kusoma hapa ili usije na maswali mengi: http://www.fifa.com/associations/association=aze/ranking/gender=m/ kisha linganisha na hapa: http://www.fifa.com/associations/association=tan/ranking/gender=m/
 
Usijadili mtu, jadili hoja. Je, si kweli kwamba watu wazima walipiga magoti kumuomba YM abadili uamuzi wake wa kutogombea tena uenyekiti?

Siwezi kumtenganisha MTU na HOJA yake kwa sababu ameiwasilisha kishabiki mno. Ungetaka tusikujadili wewe na tuijadili hoja ungekuwa OBJECTIVE otherwise wewe na hoja yako mtajadiliwa tu.
 
Duh!huwezi amini ndume nzima imempigia magoti mtoto mdogo ili tu agombee!Hivi kwani huko yanga ni YM tu ndiye mnamwamini?mbona licha ya jitihada zote na majigambo mengi bado kachezea 3-1?Hivi sasa wanatutishia Uturuki!subirini mje mwone jinsi mnavyobinuliwa tena maana bado mna ngebe sana

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
huyo maji kashitakiwa kwa kosa lajinai fail lipo kwa dpp anaonga asipelekwe kwani atopona zulumati katika mazingira ya kitapeli amebomoa nyumba kiwanja no 2474/5 seaview nyumba ilikuwa wanaishi mawaziri wakuu kama msuya na warioba atimaye aliuziwa waziri moja yeye akaibomoa na kujitwali hamezoea uwizi kama alivyotajwa kwenye epa anatoa ufadhili katika mali za dhuluma na uwizi
 
Muda umeongezwa, magoli hayajarudi!
 
Nasikia harufu kama kitu kinaungua vile kuna nn mliopo karbu na jangwan? hapana kuna kitu c bure
 
Back
Top Bottom