Wanachokifanya Marekani na NATO kwa ujumla dhidi ya Urusi ni sawa na kumbana paka kwenye kona; atakachokufanyia utakisimulia masha yako yote

Wanachokifanya Marekani na NATO kwa ujumla dhidi ya Urusi ni sawa na kumbana paka kwenye kona; atakachokufanyia utakisimulia masha yako yote

Haya waulize Walibya! Walidanganywa kuwa Gaddafi ni dikteta, anajilimbikizia Mali, mkimwondoa mtapata raha sana! Wakarubunika, wakamwasi Gaddafi na wakamwua!! Leo Walibya wanaishi maisha ya umaskini na marekani yuko pembeni akiwacheka! Wakti wa Gadafi maji na umeme vilikuwa bure, posho kubwa kwa kila asiye na ajira, ukioa unapata posho maalumu, pia kila ulipata mtoto unapata posho!! Leo vyote vimeota mbawa! Wanatamani Gaddafi angefufuka lakini haiwezekani! Hao ndio mabeberu!
Gaddafi Naye aliyataka mtu umestawi vizuri nchi yako halafu kuitwa chokochoko na marekani si utulie ule

Putin naye nchi ilikuwa iko vizuri kalala tu usiku kaota iko siku Ukraine itaishambulia Russia kaanzisha vita.Ona sasa vikwazo vinabomoa uchumi wa Russia kila kona kisa ndoto aliyoota Putin
 
Yaani mimi kiongozi wa nchi akishakuwa dikteta , mwenye tamaa ya madaraka akibadili katiba ili aongoze milele, na kuwaongoza wananchi wake kwa mkono wa chuma siwezi kumkubali kamwe! Na hicho ndicho kinatofautisha hao 'mabeberu ' na hao madikteta wanaoshabikiwa humu.

Watu wamejazana humu wanamshabikia Putin, Kim Jong Un, Xi Ji Ping na madikkteta wengine wakati jiwe aliwaonjesha moto kidogo tu ukawa mtafutano. Mswahili ni mtu wa ajabu sana!

Ubaya wa hao madikteta wanawaziba midomo raia wao, kwahiyo ukiwa buza au kyaka huwezi jua ni namna gani wanataabika. Leo hii tunawashangilia hatujui raia wao wanawasapoti ama wanawachukia kiasi gani, hakuna uhuru wa mawazo/maoni. Ndio maana hata umasikini uliowang'ang'ania hao wananchi wao hatuujui kwa sababu hakuna nafasi ya kuupata vema. Wengi wetu huma tunaamini hizo nchi zote ni tajiri sana. Niliwahi sikia kuwa North Korea hata umeme kukata ni kawaida sana, ila humu utasikia kiduku kiduku balaa!

Unapomshabikia dikteta imagine kwanza hata hali za raia wake chini ya msoto katika karne hii ya 21.

Wabongo tunapenda kuwashabikia madikteta wakiwa kwingine, ila udikteta ukiingia kwetu ndo tunaanza kuchambua takwimu za demokrasia. Kwa sasa tuna amani umesahau kabisa.

Ukiwachukia wa magharibi angalau kuwa neutral tu basi.View attachment 2148163

Sent using Jamii Forums mobile app
wewe ninani?
kwamba usichokipenda wewe wote wasikipende
VIVA PUTIN
 
Back
Top Bottom