Wanadamu tujifunze kuwa wastaarabu

Sijaona tatizo la huyo rafiki yako, kama ambavyo wewe ulikataa kununuliwa bia kwa sababu hukua na uhitaji, ndivyo hivyo hivyo ambavyo naye alikuwa hana kiu ya bia, alikunywa hiyo moja kwa kukuheshimu wewe tu, na hiyo moja iliyobakia, ulitaka aifanye nini ?, ulitaka aimwage ? au ulitaka aiache hapo wahudumu wa baa waichukue waiuze tena ?, aliona bora bora achukue hiyo hela imfae baadae, Na wewe kuwakashifu kabila zima kwa madhaifu ya mtu mmoja huo sio ustaarabu pia
 
Mtoa ofa katoa hela, aliyepewa ofa kagawa ofa, aliyedandia ofa kakubali ofa, kabadili ofa kuwa hela kasepa 😁.. Hicho ni kipaji cha kuishi mjini
 
Sijaona tatizo la huyo dada, huenda kiwango cha idadi bia ambazo huwa anatumia zilikuwa zimefikia. Sasa ulitaka aiache, me naona kama kawivu kamekushika hivi.
 
Hata hivyo kwenye uzi wangu nimesema nilikuwa sijihitaji bia kwa muda huo. hahahaahh
Kwa hiyo ndiyo mnaitana kunishambulia kisa kaswali kadogo chakari mtabari?

Uje nikununulie basi leo.
 
Hapana mkuu unaweza ukaenda kunywa whisk au wine sio lazima beer.

Kuna bar wanaoga kumbe.....asante kwa elimu.
hahahahahahahaahah, JF raha sana. Tumuombe Mungu atujalie tuuone mwaka 2020. hahahah
 
Kwa hiyo ndiyo mnaitana kunishambulia kisa kaswali kadogo chakari mtabari?

Uje nikununulie basi leo.
Siku hizi najiita Nakwede mkuu nilibadili ID,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…