Wanadiaspora wenzangu na Watanzania maisha ya majuu yana upweke sana. Tunaomba tutoe ushirikiano, mwenzetu ametutoka

Wanadiaspora wenzangu na Watanzania maisha ya majuu yana upweke sana. Tunaomba tutoe ushirikiano, mwenzetu ametutoka

Makonde plateu

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2022
Posts
1,443
Reaction score
3,480
Mtanzania Vivian Larsen aliyekuwa akiishi Nchini Denmark ameripotiwa kukutwa akiwa amefariki nyumbani kwake Nchini humo akiwa peke yake nyumbani huku ikiwa haijulikani ni lini umauti umemkuta wakati mume wake yupo safarini kikazi.

Juhudi za kuwasiliana na Polisi nchini kupata taarifa zaidi zimekwama kwa kuwa Polisi bado wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo chake.

Inadaiwa marehemu alikuwa anaishi Nchini Uhispania kabla hajaolewa na mume wake Brian Larsen mnamo mwaka 2016. Marehemu ana ndugu ambaye ni pacha wake anayeitwa Viola ambaye anaishi Mikocheni Dar es Salaam Tanzania.

Kama kuna Mtanzania yeyote aliyekuwa karibu na marehemu au kufahamiana naye enzi za uhai wake anaombwa kutoa ushirikiano wake, na familia ingefarijika sana.

Marehemu ana mtu mmoja wa familia alieoana na binamu yake Vivian anayeishi Denmark lakini naye alikuwa hajui kama Vivian yuko Denmark - Copenhagen. Taarifa alizokuwa anajua ni kwamba Vivian alikuwa anaishi Uhispania kama Mwanamitindo kwahiyo na yeye yuko kwenye masikitiko na mshangao wa kifo chake.
 
Pole kwa familia pamoja na ndugu wa marehemu.

Hili ni tatizo kubwa sana kwa Watz, tunasafiri BILA kutoa taarifa hata kwa watu wa karibu.

Fikiria, marehemu alikuwa na ndugu huko Denmark lkn hakuwah kumjulisha kuwa yupo hapo.
 
Daaah haya maisha haya bhana , poleni sana , Maisha ya Ulaya chenga sana , kuna dada mwingine alikutwa amekufa hvyo hvyo na ilichukua mwaka mzima kutambua amekufa , alifia kwenye sofa walikuta mifupa tuu , na mda huo Tv ilikuwa inaendelea kuwaka channel aliyokuwa ametune kabla ya kifo
IMG_20230322_084409.jpg


IMG_20230322_084234.jpg
 
Pole kwa familia pamoja na ndugu wa marehemu.

Hili ni tatizo kubwa sana kwa Watz, tunasafiri BILA kutoa taarifa hata kwa watu wa karibu.

Fikiria, marehemu alikuwa na ndugu huko Denmark lkn hakuwah kumjulisha kuwa yupo hapo.
Tatizo ukijukina upo nje omba omba wanakuwa wengi wakiamini una maisha mazuri sana huko. Pole kwa familia
 
Daaah haya maisha haya bhana , poleni sana , Maisha ya Ulaya chenga sana , kuna dada mwingine alikutwa amekufa hvyo hvyo na ilichukua mwaka mzima kutambua amekufa , alifia kwenye sofa walikuta mifupa tuu , na mda huo Tv ilikuwa inaendelea kuwaka channel aliyokuwa ametune kabla ya kifo
R.I.P Vivian.

Ni kweli, nchi za ulaya haswa hizi za Scandinavian upweke ni tatizo kubwa sana.

Unakuta una jirani yako kwenye 'flat' moja (milango inatizamana) lakini kama mnapishana saa za kuingia na kutoka, huyo mnaweza kukaa mwaka au zaidi bila kuonana.

Hakuna mtu anayejali kuwepo au kutokwepo kwako...hatari sana
 
Mume kasafiri, mke kakutwa amefia ndani, haijulikani kafa lini.

Si ni huyo huyo mume kahusika tu.

Huwezi safiri usiwe na ukaribu na mkeo wa mawasiliano mpaka watu baki washtukie.
 
Mume kasafiri, mke kakutwa amefia ndani, haijulikani kafa lini.

Si ni huyo huyo mume kahusika tu.

Huwezi safiri usiwe na ukaribu na mkeo wa mawasiliano mpaka watu baki washtukie.
Dada huko ulaya mambo hayaendi kihisia Kama ulivozoea Huku ndo maana wanafanya uchunguzi na ripoti watatoa kujua chanzo cha kifo, ahsante.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom