Wanafunzi 716,664 Kidato cha Kwanza hawajaripoti shuleni hadi sasa

Wanafunzi 716,664 Kidato cha Kwanza hawajaripoti shuleni hadi sasa

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Jumapili Januari 15, 2023 na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msingwa, wanafunzi 354,277 wakiwemo wenye ulemavu 697, ndiyo walioripoti hadi sasa kati ya wanafunzi 1,070,941 wanaotarajiwa kuingia kidato cha kwanza sawa na asilimia 33 ya matarajio.

Aidha amesema watoto walioandishwa kwa aajili ya kuanza darasa la kwanza ni 1,446,067 wakiwemo wenye ulemavu 2,942 sawa na asilimia 88.48 ya matarajio ya watoto 1,634,365.

Msigwa ametoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha watoto wote waliochaguliwa kwenda sekondari wanaripoti shuleni.

Amesema Serikali inagharamia elimu ya msingi na Sekondari kwa kutoa Sh 29 bilioni kila mwezi sambamba na kutoa maelekezo mahususi juu ya michango kwa wanafunzi wanaoingia shuleni lengo likiwa ni kuondoa vikwazo vya wanafunzi kujiunga na shule.

Vilevile amesema jumlanya wanafunzi 14,581 wameandikishwa katika Mpango wa Elimu ya Msingi kwa Walioikosa (MEMKWA) na kati ya hao 334 ni wenye mahitaji maalum.

MWANAHALISI ONLINE
 
Matokeo ya kidato cha pili na darasa la nne yaliyotoka juzijuzi yanasadifu kinachoendelea huko mashuleni.
 
Wazazi bado wanatafuta pesa michango ya kujiunga shuleni. mf, pesa ya dawati, mlinzi, limu, chakula cha mchana, walimu wa kujitolea nakaenikei. Si ndo maana ya elimu bure au?
 
So 33% hawajaripoti mpaka sasa, hebu watupe walau status ya kuripoti wanafunzi form one for the past 5 years tuone trend ikoje. Pia watupe status ya wanafunzi ambao wameenda private secondary schools kwa sababu inawezekana hiyo 33% inajumuisha walioenda shule binafsi.
 
Back
Top Bottom