Wanafunzi form one 2013 waanza mtihani wa kuchujwa leo

Wanafunzi form one 2013 waanza mtihani wa kuchujwa leo

Goodvision

JF-Expert Member
Joined
Apr 4, 2012
Posts
858
Reaction score
467
Wanafunzi wote wa kidato cha kwanza 2013 wameanza kufanya mtihani wa maarifa sehemu mbalimbali nchini kwa lengo la kuwabaini wale wote wasiojua kusoma,kuandika na kuhesabu.
Mtihani umegawanyika katika sehemu mbili na una jumla ya alama 50.
Taarifa kutoka kwa wakuu wa shule zinasema atakayepata chini ya alama 30 atachunguzwa kwa makini na ikiwezekana hataendelea na masomo ya kidato cha kwanza
source:mimi mwenyewe niko chumba cha mtihani
 
kama mitihan ndio kipmo cha uelewa bas mtihan wa darasa la saba hauna maana ni upotev wa hela tu.inakuwaje mtoto amefaulu alaf hajui kusoma na kuandika...
 
kama mitihan ndio kipmo cha uelewa bas mtihan wa darasa la saba hauna maana ni upotev wa hela tu.inakuwaje mtoto amefaulu alaf hajui kusoma na kuandika...

ni kweli,na waathirika wakubwa wa mfumo huu mbovu wa elimu ni watoto wa masikini,we need changes
 
Huo mtihani gani wa kumpima kidato cha kwanza eti 3*0= kulikuwa na maswali ya kijinga ya darasa la pili. Huu ni ujinga na matumizi mabaya ya hela. Na huu ni mradi wa mtu. Elimu washaiweka kapuni loooooo ndio inatokea kwa jk pekeeeee
 
kama mitihan ndio kipmo cha uelewa bas mtihan wa darasa la saba hauna maana ni upotev wa hela tu.inakuwaje mtoto amefaulu alaf hajui kusoma na kuandika...
inakuaje watanzania tunaangalia upuuzi huu!!jee mbona waziri hajaita waandishi wa habari kama vile siku ile alipotangaza matokeo kwa sifa eti KIWANGO CHA UFAULU KIMEONGEZEKA!!!hapa Jf kuna mtu alishatoa angalizo juu ya hali mbaya ya matokeo na govt kuamua kuchakachua sasa sijui aibu hii itaisha lini maana kwa kura hawataondoka
 
Njukaaaaa! umelalaaaaaa! sisi tuko machoooooo! Njukaaaaaaaa nikifika assembly kabla yenu mtadeki dinning kwa lesoooo! tena mje na hela zote mlizopewaaaaa ole wako uje bila helaaaaa! hii shule mlidhani benkiiiiii! Njukaaaaaaa unashangaa nini!!!!!
 
kila siku ubora wa elimu yetu unazidi kushuka,mara kuna form one hawajui kusoma,kuhesabu na kuandika,kesho utasikia kuna shule imekosa kabisa wanafunz waliofaulu kuingia kidato cha tatu,mara utasikia wastani wa form two umeshushwa ,mara mitaala feki,wazir na naibu wake mjiuzulu kuokoa taifa hili,hatuwataki kabisa
 
hv n kwel kwamba kizazi hik ni vilaza kiasi mim sitak kuamin kabsa.nakumbuka tulikuwa tunasoma wanafunzi 120 darasa moja lakin mbona wote tulfka darasa la pili tukiwa tunajua kusoma..hv serikal haitambui kwamba walimu wamegoma kmya kmya bila ya kubeba mabango...
 
Back
Top Bottom