Wanafunzi mliofeli kidato cha nne msikubali kutumika kisiasa

Wanafunzi mliofeli kidato cha nne msikubali kutumika kisiasa

Joined
Feb 8, 2012
Posts
92
Reaction score
9
Natoa rai kwa wote mliofeli mtihani wa kidato cha nne kuwa makini na wanasiasa wanaowachonganisha na serikali yetu tukufu ya Tanzania. Wanasiasa hao wamekuwa wakiwafanya muichukie serikali yenu kwa kutoa kauli mbalimbali mara baada ya kutangazwa matokeo ya kidato cha nne. Wanaweza kuwatumia kwa masilahi yao kisiasa.....kuna uwezekano mkubwa wakawaambia muandamane kupinga matokeo ya kidato cha nne. Kamwe msidanganyike. watawatumbukiza katika matatizo makubwa.

Ninajua wengi wenu mmepokea matokeo kwa masikitiko, hizi kauli za wanasiasa hazina mashiko...eti matokeo ya kidato cha nne yamekuwa mabaya kwa sababu zifuatazo hasa katika shule za serikali ;uhaba wa walimu, maslahi duni ya walimu, ukosefu wa maabara na zana za kufundishia, walimu kukata tamaa....sikubaliani na sababu hizi moja kwa moja...iweje shule za private kama Green Acres, Jitegemee, Makongo, Kenton zifanye vibaya ? kama sababu ndo hizo ?

Shule hizi zina kila kitu ;walimu wa kutosha wenye kulipwa vizuri, maabara na zana za kufundishia za kutosha, walimu wenye kujituma...na bado matokeo mabaya, ziro kibao...KUNA SABABU NYINGINE ZA MATOKEO MABAYA...Serikali haipaswi kulaumiwa...tusiwafanye walioshindwa mtihani waichukie serikali. Serikali inafanya kila juhudi kuboresha elimu ya nchi yetu...

Tusiyageuze matokeo ya kidato cha nne kama jukwaa la siasa uchwara.....naomba kuwasilisha.
 
Umechelewa.
Tayari wale 3 waliojinyonga weshatumika kisiasa.
.Wamesaundishwa na cdm hadi wameingia kwenye kamba pasipo shuruti na kujimaliza.
 
Mleta mada umeandika kwa kujihami sana.Mkuu watanzania wa leo wanajua adui yao vizuri sana.
 
mleta mada hebu tuambie tuwatumieje vijana wetu zaidi ya 350,000 waliofeli form 4. Otherwise GET BUSY.
 
Ni upuuzi kuilaumu serikali moja kwa moja. Nilisoma na mtoto wa Shein (kipindi Shein akiwa makamu wa Raisi wa Tanzania) na mtoto wake alifeli vibaya sana.

Huyo mtoto wa Shein alikuwa analetwa shule na kuja kuchukuliwa na gari kama mkurugenzi lakini alifeli vibaya sana na sisi watoto wa wakulima tukafaulu tena kwa alama za juu.

Kufaulu ni jitihada binafsi za mwanafunzi, hata kama serikali inahusika lakini siyo kivile kama mnavyoipamba hapa.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Sumu una akili saana...matokeo mabaya sababu kubwa ni wanafunzi wenyewe shule hawataki...ingawa kuna sababu nyingine....serikali haiwezi kumfuata kila mwanafunzi nyumbani kwake na kumbeba mgongoni aende shule....au serikali haiwezi kumfuata na kumchunga kila mwanafunzi atumie muda mwingi kujisomea badala ya facebook au kutumia muda mwingi kwenye disko na ngono zembe....
 
ndugu Sumu, kumbe Shein sasa and watoto 350,000? sipendi kuamini. I think we know better now, we're more knowledgeable, more conscious, more involved.
 
Umechelewa.
Tayari wale 3 waliojinyonga weshatumika kisiasa.
.Wamesaundishwa na cdm hadi wameingia kwenye kamba pasipo shuruti na kujimaliza.

Bado aisee. Usijeshangaa wale waliochora picha za Zombie, Messi, kulaumu Bunge, nk kukamatwa na kuhojiwa na polisi.
 
Natoa rai kwa wote mliofeli mtihani wa kidato cha nne kuwa makini na wanasiasa wanaowachonganisha na serikali yetu tukufu ya Tanzania. Wanasiasa hao wamekuwa wakiwafanya muichukie serikali yenu kwa kutoa kauli mbalimbali mara baada ya kutangazwa matokeo ya kidato cha nne. Wanaweza kuwatumia kwa masilahi yao kisiasa.....kuna uwezekano mkubwa wakawaambia muandamane kupinga matokeo ya kidato cha nne. Kamwe msidanganyike. watawatumbukiza katika matatizo makubwa.

Ninajua wengi wenu mmepokea matokeo kwa masikitiko, hizi kauli za wanasiasa hazina mashiko...eti matokeo ya kidato cha nne yamekuwa mabaya kwa sababu zifuatazo hasa katika shule za serikali ;uhaba wa walimu, maslahi duni ya walimu, ukosefu wa maabara na zana za kufundishia, walimu kukata tamaa....sikubaliani na sababu hizi moja kwa moja...iweje shule za private kama Green Acres, Jitegemee, Makongo, Kenton zifanye vibaya ? kama sababu ndo hizo ?

Shule hizi zina kila kitu ;walimu wa kutosha wenye kulipwa vizuri, maabara na zana za kufundishia za kutosha, walimu wenye kujituma...na bado matokeo mabaya, ziro kibao...KUNA SABABU NYINGINE ZA MATOKEO MABAYA...Serikali haipaswi kulaumiwa...tusiwafanye walioshindwa mtihani waichukie serikali. Serikali inafanya kila juhudi kuboresha elimu ya nchi yetu...

Tusiyageuze matokeo ya kidato cha nne kama jukwaa la siasa uchwara.....naomba kuwasilisha.

acha utani,umeamua kujibu thread yangu,nikweli wasitumike kisiasa,lakini walishatumiwa kisiasa pasipo kujua,sasa wanatakiwa wajue kuwa wanatumika,
 
Wewe umependa kilichotokea? Ni kweli wamefelishwa makusudi,nakupa sababu,1,,shule zote za vipaji wamefeli sana.2..shule za binafsi pia wamefeli tena sana,wao wana waalimu,maabara na fasilities zote,wamefeli kiwango sawa na vipaji,shule za kata nao wamefeli,wao hawana waalimu,madawati,maabara nk,nao kama wenzao binafsi,. Funga kazi ni hawa wa shule za dini,nao hakuna tofauti japo waalimu wapo hakuna wanachokosa,wao hawatumii facebok twitta wala nini, ukikutwa na simu kwenu,hamna kiduku, wala kata kei,, nao wamefeli hakuna tofauti kati ya izo scul,,,mtihani ni m1, wapo mambumbumbu sikatai,wapo walio pelekwa sec hawajui kusoma wala kuandika, mitihani ya mchujo fm 2 haupo,at the end fm4 wanafeli,hii ni siasa, ..
 
Natoa rai kwa wote mliofeli mtihani wa kidato cha nne kuwa makini na wanasiasa wanaowachonganisha na serikali yetu tukufu ya Tanzania. Wanasiasa hao wamekuwa wakiwafanya muichukie serikali yenu kwa kutoa kauli mbalimbali mara baada ya kutangazwa matokeo ya kidato cha nne. Wanaweza kuwatumia kwa masilahi yao kisiasa.....kuna uwezekano mkubwa wakawaambia muandamane kupinga matokeo ya kidato cha nne. Kamwe msidanganyike. watawatumbukiza katika matatizo makubwa.

Ninajua wengi wenu mmepokea matokeo kwa masikitiko, hizi kauli za wanasiasa hazina mashiko...eti matokeo ya kidato cha nne yamekuwa mabaya kwa sababu zifuatazo hasa katika shule za serikali ;uhaba wa walimu, maslahi duni ya walimu, ukosefu wa maabara na zana za kufundishia, walimu kukata tamaa....sikubaliani na sababu hizi moja kwa moja...iweje shule za private kama Green Acres, Jitegemee, Makongo, Kenton zifanye vibaya ? kama sababu ndo hizo ?

Shule hizi zina kila kitu ;walimu wa kutosha wenye kulipwa vizuri, maabara na zana za kufundishia za kutosha, walimu wenye kujituma...na bado matokeo mabaya, ziro kibao...KUNA SABABU NYINGINE ZA MATOKEO MABAYA...Serikali haipaswi kulaumiwa...tusiwafanye walioshindwa mtihani waichukie serikali. Serikali inafanya kila juhudi kuboresha elimu ya nchi yetu...

Tusiyageuze matokeo ya kidato cha nne kama jukwaa la siasa uchwara.....naomba kuwasilisha.

Ndio hizo ni private school Je waliosahihisha mtihani huo ni computer au ni walimu wenye matatizo kibao walonyimwa haki ya kugoma""akili za kuambiwa changanya na za kwako""_jk
 
Natoa rai kwa wote mliofeli mtihani wa kidato cha nne kuwa makini na wanasiasa wanaowachonganisha na serikali yetu tukufu ya Tanzania. Wanasiasa hao wamekuwa wakiwafanya muichukie serikali yenu kwa kutoa kauli mbalimbali mara baada ya kutangazwa matokeo ya kidato cha nne. Wanaweza kuwatumia kwa masilahi yao kisiasa.....kuna uwezekano mkubwa wakawaambia muandamane kupinga matokeo ya kidato cha nne. Kamwe msidanganyike. watawatumbukiza katika matatizo makubwa.

Ninajua wengi wenu mmepokea matokeo kwa masikitiko, hizi kauli za wanasiasa hazina mashiko...eti matokeo ya kidato cha nne yamekuwa mabaya kwa sababu zifuatazo hasa katika shule za serikali ;uhaba wa walimu, maslahi duni ya walimu, ukosefu wa maabara na zana za kufundishia, walimu kukata tamaa....sikubaliani na sababu hizi moja kwa moja...iweje shule za private kama Green Acres, Jitegemee, Makongo, Kenton zifanye vibaya ? kama sababu ndo hizo ?

Shule hizi zina kila kitu ;walimu wa kutosha wenye kulipwa vizuri, maabara na zana za kufundishia za kutosha, walimu wenye kujituma...na bado matokeo mabaya, ziro kibao...KUNA SABABU NYINGINE ZA MATOKEO MABAYA...Serikali haipaswi kulaumiwa...tusiwafanye walioshindwa mtihani waichukie serikali. Serikali inafanya kila juhudi kuboresha elimu ya nchi yetu...

Tusiyageuze matokeo ya kidato cha nne kama jukwaa la siasa uchwara.....naomba kuwasilisha.

Kum@n1n@ ! Humu ndani wengine tuna hasira msianzishe mazungumzo ya kutibuana na ninakuomba post yako ya kwanza iwe ya kufuta kauri yako ya kuiita serikali ya kina lowasa serikali tukufu. kikwete mwenyewe hajatamka hiyo kauli tangu mwaka uingie
how come serikali ya wezi(richmond,dowans,rada,epa,...., ....., ....,) Majasusi(matukio ya ulimboka,jerrymuro,kubenea,..., ......, ......, .....,) wauaji(arusha, mbeya iringa) leo kwa uhuru kabisa unasimama mbele ya uma kwenye zaidi ya watu 100,000 wenye majeraha ya migao ya umeme na matatizo kibao ya ugumu wa maisha unatamka eti serikali tukufu Daaaaah! nimekelekwa kweli kweli

Hiviiiiiiiiiiiiiiiiii unaanzaje kuzungumzia siasa kwenye hatma ya maisha ya maelfu ya vijana waliofelishwa kwa uzembe wa washenzi wachache!?
Hizi ndizo kati ya sababu tunazosema serikali yetu haina uwezo wa kuongoza hii nchi
Fikiria kama imeshindwa kucontrol angalau wakapata 50% ya watu waliofaulu kitu ambacho naamini ni jambo la kucheza na mahesabu kidogo tu hata wakimpa hiyo kazi Pro lipumba anaweza kuifanya wao wameshindwa hivi wataanzia wapi kupiga hesabu za watt za umeme zinazo hitajika kumaliza migao ya giza, watamaliza lini kiini macho cha mafoleni barabarani, Pata picha mahesabu ya madawati tu na mishahara ya walimu yamekuwa mitihani mpaka wanafelisha watoto wawatu je sayansi ya kushusha bei ya nyanya na kitunguu wataiweza?

USHAURI WANGU MIMI
Sio kwa waliofeli tuuuuu Bali wanafunzi wote wa shule za secondary Walio feli, waliofaulu na waliopo mashuleni, walimu Na wazazi wenye uchungu na Tanzania bora kwa ajili ya kizazi kijacho ni kuendesha mgomo mzito na maandamano makali Mitihani Irudiwe. la sivyo watakuja kuwa vibaka, makahaba, majambazi wakati tukilitafutia uvumbuzi jambo hili hao hao ni hazina kubwa sana kwa taifa. Wanafunzi wa vyuo vikuu wana jumuia zao walipoletewa longolongo walipigania haki zao mpaka kikaeleweka, Hawa vijana wa secondary Hawana chama wala jumuia inayowaunganisha iliwafanye uamuzi wa pamoja hivyo basi chama chochote mtu yoyote jumuia yoyote asasi au taasisi inaweza kuwashauri kufanya jambo sio kukaa kimya haitaeleweka wameridhika, wameonewa, wanaomba warudie, wanataka waende jeshini veta au vipi? ila kama wameonewa........ kama wameonewa basi pesa zetu za kodi hapo ndio zitumike sio zikawekwe uswizi halafu sisi tutajua cha kumfanya anaetutia hasara. Na wewe ndugu Opportunist kama ni wakala wa magamba najua wanaogopa sana maandamano rudi kawaambie sisi tunajua kuwa nyoka akijivua magamba habadiliki kuwa sungura tena hata kufanana hawatafanana sura wala harufu kwa hiyo tunachotaka ni kitu kimoja walivyotutia hasara na kutuibia vinatosha Watuachie nchi yetu.


 
Sikilizeni jamani mtuhumiwa wa kwanza hapa ni serikali, wakati wanatuombakula walisema ufaulu wawatoto wataongeza kwa asilimia 60 na 75 kufikia 2013. Walisema watalipa mishahara ya walimu na kuongeza fifaa vya kufundishia, mwaka 2008, 2009, 2010 2011 mpaka mwaka jana hadi watoto wasiojua kusoma na kuandika wamefaulu kuingia kidato cha kwanza

kuhusu mishahara ya walimu, walimu wameongea mpaka basi sasa hivi wamenyamaza sio kwamba yameisha ila ukweli ni kwamba wamesusa.

Ok tufike wakati tuachane na drama kwenye kupigania maendeleo ya nchi yetu, kwanini hawakusema kuwa uwezo wa kusimamia elimu hawana wakati wanaomba kuchaguliwa, na kuonesha serikali ilidhamiria na ilijua wapi inatupeleka kwenye swala la elimu presha na mstuko juu ya matokeo vipo normal, visingizio kibaoo

mimi naamini kama ikipatikana serikali makini kufeli asilimia 60% ya watahiniwa ni aibu kwa taifa na jambo lisilokubalika lililotakiwa liwe limezuiwa kwa namna yoyote na endapo linatokea basi mzembe lazima awajibishwe tena sio kwa kujiuzulu na kufunguliwa mashtaka.
 
Ni upuuzi kuilaumu serikali moja kwa moja. Nilisoma na mtoto wa Shein (kipindi Shein akiwa makamu wa Raisi wa Tanzania) na mtoto wake alifeli vibaya sana.

Huyo mtoto wa Shein alikuwa analetwa shule na kuja kuchukuliwa na gari kama mkurugenzi lakini alifeli vibaya sana na sisi watoto wa wakulima tukafaulu tena kwa alama za juu.

Kufaulu ni jitihada binafsi za mwanafunzi, hata kama serikali inahusika lakini siyo kivile kama mnavyoipamba hapa.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Na hizo shule ambazo hazina walimu nazo?
 
Na hizo shule ambazo hazina walimu nazo?

Ninakubali serikali inapaswa kulaumiwa kwenye haya matokeo lakini isiwe ndiyo kigezo cha kuacha kuangalia sababu nyingine zilizopelekea wanafunzi kufeli.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
mleta mada hebu tuambie tuwatumieje vijana wetu zaidi ya 350,000 waliofeli form 4. Otherwise GET BUSY.

Hii ni opportunity ya kuanzisha business management college kwa sie wajasiriamali
 
Mbunge analipwa sjilingi ngapi? Je walimu, hata wa private wapo kwenye mgomo mana wengi wa walimu wa shule hizo walipangwa porini wakachukia wakaondoka, wapo binafsi kwa machungu tuu.mitiani ilikuwa simple, ishu hizi wanazijua wanafunzi na walimu wao, den serikali, na wanasiass, hata wangefaulu masomo yao ni sanaa, yani sayansi ni ziro, mitaala duni, lugha ngumu ya kingereza, utandawaz, n.k
 
Ni upuuzi kuilaumu serikali moja kwa moja. Nilisoma na mtoto wa Shein (kipindi Shein akiwa makamu wa Raisi wa Tanzania) na mtoto wake alifeli vibaya sana.

Huyo mtoto wa Shein alikuwa analetwa shule na kuja kuchukuliwa na gari kama mkurugenzi lakini alifeli vibaya sana na sisi watoto wa wakulima tukafaulu tena kwa alama za juu.

Kufaulu ni jitihada binafsi za mwanafunzi, hata kama serikali inahusika lakini siyo kivile kama mnavyoipamba hapa.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Upo sawa kuna lakini mkuu serikali nayo inahusika,naamini serikali ingekuwa makini failures zingekwepo lakini si nyingi kama hizi,kuna watoto kibao nilikuwa nawaona wanajituma lakini mazingira yalikuwa ni hash kwao.Si kweli kabisa kuwa ni uzembe wa watoto moja kwa moja. Nina uhakika kama serikali ingekuwa makini kwa kiwango fulani atleast kila shule ingekuwa na division one,two vilevile three,japo majority nao wangekuwa four na zero.Mkuu matokeo ya sasa yanatisha.Nakubaliana nawe kwenye baadhi ya mambo kama descipline ya wanafunzi kushuka.LLakini kuan watoto wanajituma kwa bidii lakini wamekosa msaada.walimu wamekata tamaa,atoto wamekataa tamaa serikali inaendeleza propaganda unategemea atafaulu mtu hapo.
 
Back
Top Bottom