Wanafunzi UDSM Kuanza Mgomo Na Maandamano Yasiyokoma - Jumatatu, Tarehe 5 May

Wanafunzi UDSM Kuanza Mgomo Na Maandamano Yasiyokoma - Jumatatu, Tarehe 5 May

Kabwena

Senior Member
Joined
Jun 17, 2013
Posts
103
Reaction score
55
Kutokana na hali mbaya ya kiuchumi inayowakabili wanafunzi wa vyuo vikuu nchini ambao wanadhaminiwa na bodi ya mikopo huku hatma ya wanafunzi hao kupata fedha zao za kujikimu kwa awamu ya nne ikiwa haijulikani hatimaye wanafunzi wa chuo kikuu dar es salaam UDSM wameamua kuanza rasmi mgomo na maandamano yasiyokoma kesho Jumatatu ya tar. 5 Mei.

Maandamano hayo makubwa ya kushinikiza kupata malipo yao[boom] kwa awamu ya nne yanatarajia kuanza kesho saa moja kamili asubuhi katika eneo la chuo hicho linalojulikana kama REVOLUTION SQUARE na kisha kuelekea barabara ya Ubungo na kumalizikia katika makao makuu ya bodi ya mikopo-HESLB..

Tayari mabango yenye jumbe mbalimbali yanaandaliwa katika hostel za mabibo na main campus ili kuweza kutumika siku ya kesho..

MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA.. "SOLIDARITY FOREVER"
 
Kazi ipo.
Au fedha za wanachuo zimekwenda bunge la katiba? au sherehe za miaka 50?
Tatizo HESLB mmekaa kimya sana.
Mzee Nyantega mabango hayo yanakuja.
 
poleni sana, serikali naona hela imemalizia ckukuu ya muungano, bunge la katiba,
komaeni madogo hii
 
Haya haya Ruco. tumaini. mkwawa.Saut.
mzumbe. ifm. kiu. waungeni wenzenu mkono. umoja n nguvu.
 
...loh shemeji alikubali mwenyewe kuitwa hivyo...
 
Bila shaka selikali itakuwa imefulia maana hata mishahara ya mwezi jana italipwa tarehe 38!
 
Wanafunzi wawe watulivu, fedha huenda zinatumika ktk ziara ya kinana, Miaka 50 ya muungano na ziara mpya ya kujibu mapigo ya ukawa. Tanzania bila ccm haiwezi kuendelea ni vita tu zitashamiri. UVCCM chuoni zimeni hili sio kubwabwaja tu majukwani.
 
Hiyo imetulia kama walikubali na mkaingia nao mkataba BODI YA MIKOPO lazima hili liwahusu na walimalize wenyewe. Haiingii akili wakaka kimya muda wote bila ya kuwajulisha Wanafunzi kuwa nn kinaendelea. Feedback zingetoka mapema sidhani kama haya yote yangetokea. GOD bless liberity..forever.
 
Last edited by a moderator:
Vyuo vyote ni ukata mtupu, hata wanafunzi wa udakyari bingwa wanaofadhiliwa na wizara ya afya katika vyuo mbalimbali hawajapata hela zao, walilipwa hela hadi December 2012 basi.
 
Hela zinahifadhiwa kulipa siku 60 za nyongeza ya bunge la katiba. Chezea shemeji wewe!
 
Kumbe watu wanapenda migomo na maandamano eeeee!!!!! Hamna mtu humu aliyeuliza ni lini wangepaswa wapewe fedha zao au wamecheleweshwa kwa muda gani.

Mimi uhakika nilio nao ni kwamba bodi ya mikopo wametoa fedha za baadhi ya vyuo ikiwemo UDSM ingawa siyo wote. Swali, hao wanafunzi watuambie humu kama walivyojaza form na kufuatilia mpaka wakapata mkopo je juhudi gani wamefanya kufuatilia boom la nne? Tuache kupenda mapambano kabla ya mipangao. Mipango ndiyo huzaa matunda mema.

Mwisho nakumbuka miaka miwili iliyopita nilitoa ushauri humu nikapata matusi ya kutosha lakini mwisho kina kijicho, alshabab, alphonse emeka, na silayo wanaweza kusimulia yaliyowakuta. Wengine wamerudi chuo kwa magoti kuomba radhi na kukiri kuwa waliwachapa viboko wenzao haohao wako behind this deal. Nawashauri kuwa watafuatana na important letter ndipo watakapojitambua zaidi.

Kuandamana ni kwema ila tunaandamanaje ndipo ngoma ilipo. Kama kweli mnachotaka ni boom, tuanzie maandamano yetu nnje ya geti la bodi ya mikopo tuzame ndani, maana kuanzia chuo hamtafika popote zaidi ya geti maji au geti ardhi na siye wengine tutajionea kwenye TV jioni baada ya kutoka makazini au humu humu kwa waleta habari wetu.
 
Pambaneni makamanda haki haiombwi inapiganiwa
Nyie Chadema ndiyo mnawadanganya hawa wanafunzi wafanye maandamano.

Mnawaita makamanda haya ngoja jumatatu tuone makamanda watakavyopambana FFU.

Tanzania hakuna maandamano yaliyofanikiwa.

Nawashauri wanafunzi watumie njia za kawaida kudai pesa zenu hamna uwezo wa kufanya maandamo kuishinikiza serikali, wameshindwa Chadema mtaweza nyie.

Mtaishia kupigwa na kufukuzwa vyuoni na mwisho kulalamika polisi wametumia nguvu nyingi kuzima maandamano.
 
Wachote za Bunge la Katiba wawape,Katiba mpya tutasubiri .
 
Kumbe watu wanapenda migomo na maandamano eeeee!!!!! Hamna mtu humu aliyeuliza ni lini wangepaswa wapewe fedha zao au wamecheleweshwa kwa muda gani.

Mimi uhakika nilio nao ni kwamba bodi ya mikopo wametoa fedha za baadhi ya vyuo ikiwemo UDSM ingawa siyo wote. Swali, hao wanafunzi watuambie humu kama walivyojaza form na kufuatilia mpaka wakapata mkopo je juhudi gani wamefanya kufuatilia boom la nne? Tuache kupenda mapambano kabla ya mipangao. Mipango ndiyo huzaa matunda mema.

Mwisho nakumbuka miaka miwili iliyopita nilitoa ushauri humu nikapata matusi ya kutosha lakini mwisho kina kijicho, alshabab, alphonse emeka, na silayo wanaweza kusimulia yaliyowakuta. Wengine wamerudi chuo kwa magoti kuomba radhi na kukiri kuwa waliwachapa viboko wenzao haohao wako behind this deal. Nawashauri kuwa watafuatana na important letter ndipo watakapojitambua zaidi.

Kuandamana ni kwema ila tunaandamanaje ndipo ngoma ilipo. Kama kweli mnachotaka ni boom, tuanzie maandamano yetu nnje ya geti la bodi ya mikopo tuzame ndani, maana kuanzia chuo hamtafika popote zaidi ya geti maji au geti ardhi na siye wengine tutajionea kwenye TV jioni baada ya kutoka makazini au humu humu kwa waleta habari wetu.

Wewe acha upuuzi wako aisee
 
Back
Top Bottom