Wanafunzi wa Kampala waandamana hadi TCU

Void ab initio

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2015
Posts
5,720
Reaction score
5,659
Wanafunzi zaidi ya 200 wa chuo cha Kampala wameandamana hadi ofisi za TCU wakitaka kujua hatma yao ya kielimu.

Chanzo: ITV
 
Yan hcho chuo ni majanga tu maana mi mwenywe nipo pale nasoma bachelor ya pharmacy ila mpaka leo hakuna na maana
 
Hiki chuo kuna mkono mrefu sana!!
 
Siwatetei ila sidhani kama wanafunzi wengi huwa tunafanya tafiti za kina
pale tunapotaka kujiunga na vyuo na taasisi mbalimbali za elimu ya juu
sidhani kama wengi huwa tunazingatia kufatilia usajili wa hivi vyuo na hata
usajili wa kozi mbalimbali sababu laiti kama tungekuwa tunaangalia hivi vitu
mapema hivi vyuo hakika visingekuwa miongoni mwa machaguo yetu kabisa
na hizi shida saiv zisingekuwepo hii nchi imeshavurugika umakini na jitihada
zako ndo unaweza kukufanya usipate taabu hili tatizo sio la kutatuliwa leo
kutokana na mazoea ya serikali yetu laiti hawa wanafunzi wangekuwa makini
hii shida isingekuwepo hili ni funzo kwa wanaojiandaa kuingia vyuoni mwaka huu
na walio shuleni wasome kwa bidii ili wasije chaguliwa vyuo visivyo kidhi mahitaji ya mitaala
na kozi wazipendazo kusoma katika Elimu ya juu
 
kuna vitu mpaka kesho havitakuja jibiwa..ni ilikuaje wanafunzi wakapelekwa kwenye chuo ambacho hakijasajiliwa???inakuaje wamepewa mikopo??ilikuaje kamati ya bunge iliona chuo hakina usajiri wa kudumu..leo prof anadai kina full registration toka 2012!!!!??nani kadanganya umma kati yao...
 
Ila kwel bro kutokujua ndio kunatusababishia matatizo haya lakini TCU kama serikali kwn halilijui tatizo LA Kampala? Coz hili tatizo ni la mda mrfu cnc mwezi wa nne kumekuwa na mgomo hapa chuon
 
We acha 2 ila hii dhambi cku moja lazima itamtafuna coz wazaz wetu huko vijijin wanahangaika kutulipia ada af watu wachache wanachezea maisha yetu inauma we acha 2
 
TCU wana kazi gani kama kila mtu itabidi afatilie usajili na ubora wa vyuo??!! Yaani ndio maana Tanzania haiwezi kuendelea kirahisi, yaani watu wamefanya uzembe hadi wanafunzi kujiunga na chuo kisicho na usajili wewe unataka kulaumu wanafunzi??!!

Hao wahusika ilitakiwa wawe jela kwa kucheza na vichwa vya watu ila kwa kuwa ni Bongo hata wewe huoni kama ni kosa kwa upande wa TCU.
 
we unaongea ujinga kwani bodi husika ambayo ni Tcu iliwekwa kwajili gani na na kwanini nao pia wamekiweka kwenye guide book yao inamaana utasema ni kosa letu tumia akili akati unajibu hoja humu
 
Hiki sio chuo...ni genge linalotengeneza fedha kwa walaji tu. Mwaka Jana PHD takriban 56 zilifutwa uko Uganda kwa kuto kidhi vigezo.
Aidha Kenya walitangaza kufuta degrees za chuo hiki kwa kipindi chote cha miaka kumi ilopita. Hazitambuliwi.

Sudan kusini pia wamechukua hatua hiyo mwaka Jana. Tanzania ndo bado tunalega legaaa. Kama kagame anavyobsema Rushwa ya kitanzania ndo tatizo.
 
Kweli bongo sanaaa zimezidi mpaka kwenye elimu,sasa waziri wa elimu na afya wamekubali kuzitambua izo kozi leo tena vijana wamegoma kwa iyo Yale yalikua maneno ya kuwapoza tu vijana,Poleni sana vijana,ila tatizo mnachodai sasa ivi kigumu mnataka muamishwe mtaenda wapi?komaeni mpate usajili vijana acheni kudanki danki.
 

Mkuu nakubaliana na mawazo yako ila naomba nikurekebishe kidogo.
1. Mwanafunzi anapochagua chuo anapewa nafasi tano (5 Choices) za kuchagua chuo au kozi anazotaka kusoma
2. TCU haimpangii mwanafunzi chuo au kozi nje ya zile 5 selections za mwanafunzi alizojaza kwenye profile yake kupitia CAS

3. Kuna TRansfer pia - wanafunzi wengi walioko KIU waliingia pale baada ya kutemwa kwenye CAS sababu ya ushindani. baada ya nafasi kwenye vyuo vingi vya afya kujaa KIU ilikuwa ina nafasi nyingi tu kwenye mtandao wa TCU. wengi waliomba nafasi za afya KIU waliingia kwa mfumo huo.

4. Transfer za ndani - (internal Transfer) wanafunzi wengi wa KIU wapo walioomba kozi tofauti kabisa mfano BSc Computer Science na kisha kufanya internal transfer wao wenyewe chuoni kwa ridhaa yao na kukubaliwa na chuo.

5. TCU sidhani kama wanawachagulia watu programme au kozi za kusoma bila ridhaa yao.

6. Ushindani wa wanafunzi kwenye kada ya afya kwa mwaka 2014/15 ulikuwa mkubwa sana kiasi ambacho wengi waliiomba kada za afya waliishia kukosa kutokana na ushindani mkubwa.

baada ya huo ufafanuzi hapo juu naomba uelewe kuwa uchaguzi upo kwa mwanafunzi mwenye na kitu kikubwa ni ufaulu wake ndio utakao mpeleka kwenye chuo kizuri na kozi nzuri anayoitaka.

Tuepuke lawama kuwatupia TCU wakati sisi wenyewe wanafunzi ndio chanzo cha matatizo yote
 
Mimi nafikiri kuna harufu ya rushwa kwenye mchakato wa kukisajiri chuo hicho ndio maana wanalaumiana bila kupata ufumbuzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…