Hivi jiulize huyo msichana aliitwa kupeleka usiku huo hiyo barua au alitaka kumkomesha prof wa watu?
Mkuu! the only source of information ambayo tunayo basi ni hii thread yako na ndio maana tunaibua masuali kutokana na thread inavyojieleza. Na kuhusu hapo red, Hilo tatizo kweli lipo lakini kisheria kila tatizo linahukumiwa kipekee kulingana na ushahidi unaowasilishwa, (hakuna ushahidi wa kwamba wengi wanafanya..... katika mahakama). All in all kwa habari ilivyowasilishwa basi nakuhakikishia huyo mwanafunzi kibao kitamgeukia tu, labda waje na masimulizi mapya.
Suala langu muhimu ni: Kwanini aliamua (rejea thread yako) kuwasilisha maelezo usiku tena nyumbani kwa mkufunzi?
Asingemfungulia kama anafata maadili, walitakiwa wamalizane mchana ofisini, kifo kilikuwa kinamwitayote yawezekana sema marehemu hana haki
ila na walimu hasa wa elimu ya juu wanapenda sana vya kunyea kaaaaaaaaaaaaaaaaa
wewe mtu anagonga mlango karibu mpaka ndani
...Let me stick here! Umeona mbali MTMTuelewavyo sisi, ni kwamba hii kitu ilisukwa na ina mtu mwingine ambaye si mwanafunzi ana atajulikana very soon
Au walipanga na wanafunzi wenzake mkisikia kelele mje mbio tumkomeshe ticha mnoko, ila mwanafunzi mmoja akampiga kimakosa kichwani...Let me stick here! Umeona mbali MTM
Hatujajua bado kama ni mchongo au ni ukware kweliThis should be a lesson for wale wakware wote!
<br /><font size="3"><img src="http://ippmedia.com/images/frontend/headline_bullet.jpg" border="0" alt="" /> <b>Adaiwa kutaka kumbaka mwenzao</b></font><br />
<font size="3"><img src="http://ippmedia.com/images/frontend/headline_bullet.jpg" border="0" alt="" /> <b>Ni mwalimu wao wa nidhamu</b></font><br />
<br />
<font size="3">Wanafunzi wa Chuo cha Uuguzi cha Bulongwa kilichoko Wilaya ya Makete mkoani Iringa, wamemuua kwa kumshambulia kichwani mkufunzi wa chuo hicho, <b><font color="red">Dk.</font></b> Jumbe Mafingo, kwa madai ya kupinga jaribio lake la kutaka kumbaka mwanafunzi mwenzao.</font><br />
<font size="3"><br />
Taarifa za awali za makachero wa polisi zilieleza kuwa mkufunzi huyo aliuawa baada ya kutuhumiwa kwamba alitaka kumdhalilisha kijinsia mwanafunzi wa kike, Jean Laison Mwakabuta kwa kutaka kumbaka.</font><br />
<font size="3">Tukio hilo la kuuawa kinyama kwa mkufunzi huyo ambaye ni mwalimu wa nidhamu chuoni hapo, lilitokea juzi usiku nyumbani kwake mjini hapa.</font><br />
<font size="3"><br />
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Evarist Mangalla, <b><font color="red">Dk</font></b>. Mafingo alifikwa na umauti baada ya mwanafunzi huyo kuamua kwenda nyumbani kwake usiku ili kumkabidhi maelezo yake ya kimaandishi kuhusu sababu zilizomfanya alale nje ya chuo.</font><br />
<font size="3"><br />
Ilielezwa kuwa muda mfupi baada ya kuingia kwenye nyumba ya mwalimu huyo, mwanafunzi huyo alianza kupiga kelele kuwa anabakwa.</font><br />
<font size="3"><br />
Alisema kufuatia kelele hizo, wanachuo wengine waliamka katika vyumba vyao na kwenda hadi eneo la tukio na kuanza kumshambulia kichwani mkufunzi huyo hadi kumuua.</font><br />
<font size="3"><br />
Kamanda Mangalla alisema <b><font color="red">Dk</font></b>. Mafingo aliuawa kwa kushambuliwa na kitu kizito kichwani.</font><br />
<font size="3">Huyu Jean Laison Mwakabuta, aliambiwa na <b><font color="red">Dk</font></b>. Mafingo ambaye ni mwalimu wa nidhamu chuoni hapo, aandike maelezo ya maandishi kwa sababu gani alilala nje ya chuo,...baada ya kuandika maelezo hayo, aliamua kuyapeleka nyumbani kwa mkufunzi huyo usiku, sasa baada ya kugonga mlango na hatimaye akaruhusiwa kuingia, alianza kupiga kelele kwamba anabakwa na ndipo wanafunzi wenzake waliposikia kelele wakaamka na kukimbilia eneo hilo na kumshambulia mkufunzi huyo hadi kufa, alisema Kamanda Mangalla.</font><br />
<font size="3"><br />
Ilidaiwa kuwa siku moja kabla ya tukio hilo, uongozi wa chuo hicho cha Bulongwa ulitoa ridhaa kwa wanachuo wote kwenda kutembea nje ya chuo kwa lengo la kuwapunguzia msongo wa mawazo ya masomo na Jean Laison Mwakabuta hakurejea chuoni hadi siku iliyofuata.</font><br />
<font size="3"><br />
Kamanda Mangalla, alisema wanachuo wanne akiwamo mwanafunzi Jean, wametiwa mbaroni kuhusiana na mauaji hayo.</font><br />
<br />
CHANZO: NIPASHE <br />
<br />
<br />
<b>maoni:</b> hivi watu wanashindwa kuoa wake zao wa halali, naona kina dada nao wameshituka sasa
<br />
<br />
Waue2 mimi mwenyewe mwl ndo alinifukuzisha shule,kwa kusimamia kesi ya mwanafunzi mwenzangu ambaye ni mpenzi wake pia.ni funzo zuri.
<br />DUH hii yako kali ilikuwaje mkuu
kwa mie sioni hata sababu moja ya kumtetea mwanafunzi,na pia sioni pia kosa lolote la mkufunzi hii ni kwa sababu zifuatazo;
Mwanafunz wa chuo ni mtu mzima kabisa
kwa maana hii mkufunzi kutembelewa na mwanafunzi usiku alafu usifungue mlango au kumwambia asiingie ndani sidhani kama ni kosa kwake wala mtu mwingine yeyote, kwa desturi ya mwanadamu mtu anapokuja kwako bila kujua nia ya ujion wake lazima utamkaribisha ndani na kumsikiliza aliyojia., tunaweza tusijue hasa kilichojiri but pengine mpaka mwanafunzi kufunguliwa na kuingia ndani kulikuwa na maelezo ya ziada toka kwa mwanafunzi na sio maandishi tu,ndipo alipokaribishwa ndani
kwa maana hii basi hakukuwa na udhalilishwaji wa kijinsia bali ni kujidhalilisha kwa mwanafunzi mwenyewe kwa kwenda kwa mwalimu usiku
Hao Mabinti wamtafute Lawyer mzuri la sivyo wataozea jela...
Hii ni kweli na kwanini alikwenda pekee yake wakati anajua fika mwl anaishi pekeyake?Hii inaonyeshaa ulikuwa mpango wa kumkomesha Dr.tumempoteza mtaalamu.RIP DrDu hii kali.kikawaida haileti maana,kwanini apelekee barua nyumbani kwa mwalimu?kwanini aipelekee usiku?haiwezekani aingie tu alafu mzee ajaribu kumbaaka bila hata ya kumzingua kwa maneno kwanza..huyo dada ana kesi kubwa hapo
mimi bado nasimama kweli suhala kwamba walimu wanamchezo wa kupata ngono kwa kutmia ofisi kutoka kwa wanafunzi
hasa hawa wa nidhamu, sina hakika kama yeye alikuwa kundi hilo maana sikuwa kwenye eneno la tukio lakini , kama mwalimu angelikuwa sio mtu wa totozi
sidhani kama hata mwanafunzi angepeleka barua nyumbani usiku,
madaktari na totozi ndio zao BANA mtu dada anakwenda hospitali na jipu chini ya goti anaambiwa atoe nguo zote.
waliliza hapa wanasema.
hii inaweza kuwa kokote kuna shida.
kwanza kwa nini alimkalibisha ndani ?
mkuu barua za kiofisi na nyumbani kwa DR usiku wapi na wapi?
kunamchezo wa kuwatumia dada zetu wasio na ujasiri wa maisha na ina dalili zote
yawezekana katika ili tukio hakuna kitu lakini kama kanuni zingefuatwa sidhani kama haya yangetokea
Ilikuwaje huyo dada apeleke barua nyumbani kwa mkufunzi tena usiku?na je,hao wanafunzi waliompiga wana uhakika gani kama kweli alitaka kumbaka?na je hawakuona njia nyingine ya kutumia zaidi ya kumpiga?hapo pana mushkhel kidogo?