<font size="3"><img src="http://ippmedia.com/images/frontend/headline_bullet.jpg" border="0" alt="" /> <b>Adaiwa kutaka kumbaka mwenzao</b></font><br />
<font size="3"><img src="http://ippmedia.com/images/frontend/headline_bullet.jpg" border="0" alt="" /> <b>Ni mwalimu wao wa nidhamu</b></font><br />
<br />
<font size="3">Wanafunzi wa Chuo cha Uuguzi cha Bulongwa kilichoko Wilaya ya Makete mkoani Iringa, wamemuua kwa kumshambulia kichwani mkufunzi wa chuo hicho, <b><font color="red">Dk.</font></b> Jumbe Mafingo, kwa madai ya kupinga jaribio lake la kutaka kumbaka mwanafunzi mwenzao.</font><br />
<font size="3"><br />
Taarifa za awali za makachero wa polisi zilieleza kuwa mkufunzi huyo aliuawa baada ya kutuhumiwa kwamba alitaka kumdhalilisha kijinsia mwanafunzi wa kike, Jean Laison Mwakabuta kwa kutaka kumbaka.</font><br />
<font size="3">Tukio hilo la kuuawa kinyama kwa mkufunzi huyo ambaye ni mwalimu wa nidhamu chuoni hapo, lilitokea juzi usiku nyumbani kwake mjini hapa.</font><br />
<font size="3"><br />
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Evarist Mangalla, <b><font color="red">Dk</font></b>. Mafingo alifikwa na umauti baada ya mwanafunzi huyo kuamua kwenda nyumbani kwake usiku ili kumkabidhi maelezo yake ya kimaandishi kuhusu sababu zilizomfanya alale nje ya chuo.</font><br />
<font size="3"><br />
Ilielezwa kuwa muda mfupi baada ya kuingia kwenye nyumba ya mwalimu huyo, mwanafunzi huyo alianza kupiga kelele kuwa anabakwa.</font><br />
<font size="3"><br />
Alisema kufuatia kelele hizo, wanachuo wengine waliamka katika vyumba vyao na kwenda hadi eneo la tukio na kuanza kumshambulia kichwani mkufunzi huyo hadi kumuua.</font><br />
<font size="3"><br />
Kamanda Mangalla alisema <b><font color="red">Dk</font></b>. Mafingo aliuawa kwa kushambuliwa na kitu kizito kichwani.</font><br />
<font size="3">Huyu Jean Laison Mwakabuta, aliambiwa na <b><font color="red">Dk</font></b>. Mafingo ambaye ni mwalimu wa nidhamu chuoni hapo, aandike maelezo ya maandishi kwa sababu gani alilala nje ya chuo,...baada ya kuandika maelezo hayo, aliamua kuyapeleka nyumbani kwa mkufunzi huyo usiku, sasa baada ya kugonga mlango na hatimaye akaruhusiwa kuingia, alianza kupiga kelele kwamba anabakwa
na ndipo wanafunzi wenzake waliposikia kelele wakaamka na kukimbilia eneo hilo na kumshambulia mkufunzi huyo hadi kufa, alisema Kamanda Mangalla.</font><br />
<font size="3"><br />
Ilidaiwa kuwa siku moja kabla ya tukio hilo, uongozi wa chuo hicho cha Bulongwa ulitoa ridhaa kwa wanachuo wote kwenda kutembea nje ya chuo kwa lengo la kuwapunguzia msongo wa mawazo ya masomo na Jean Laison Mwakabuta hakurejea chuoni hadi siku iliyofuata.</font><br />
<font size="3"><br />
Kamanda Mangalla, alisema wanachuo wanne akiwamo mwanafunzi Jean, wametiwa mbaroni kuhusiana na mauaji hayo.</font><br />
<br />
CHANZO: NIPASHE <br />
<br />
<br />
<b>maoni:</b> hivi watu wanashindwa kuoa wake zao wa halali, naona kina dada nao wameshituka sasa