Wayahudi wote wafundisha ya kwamba sheria zote za Sabato zaweza kuvunjwa kama maisha ya kibinadamu yako hatarini.
Kwa muda mrefu Jumapili iliheshimiwa kama siku ya ibada ya kikristo lakini bila masharti ya kuacha kazi. Sharti hili lilikaziwa tu katika nchi za Ulaya tangu karne ya 18 na 19. Maandishi haya nimeyapata kwenye wikipedia hii inamaanisha kwamba sabato ni siku ya mayahudi na wala sio siku ya manasara (wakristo), pia siku yeyote kati ya Jumamosi au Jumapili muumini anaweza kufanya kazi pindi kama maisha yake yako hatarini; swali jee kukosa mtihani (kwa kishingizio cha sabato) hakuhatarishi maisha ya mwanafunzi husika..????? angusha points hapo mwanangu..???
Unaweza kufaulu bila kumtegemea/kumcha Mungu?
NADHANI HAPA KULIKUA NA MALIZE TU, NASIKIA WALIOTANGULIA WALIKUA WANAFANYA JUMAPILI kama kawa...........
Kwa uelewa wangu mtihani haupo katika vilivyozuiliwa kufanya siku ya saba. mna-complicate tu imani yenu safi ya sabato na kuonekana kama ni tatizo.. Ile mijikazi ya nguvu inayokufanya hata unavua shati kwa mijasho ndio iliyokatazwa.
kuna kitu hukijui, jumapili sio siku ya ibada ya wakrito. Ni mfalme constantino aliyeipitisha rasmi kama siku ya ibada kwa wakristo. Biblia au yesu mwenyewe hajabadili siku ya ibada kutoka sabato kwenda jumapili. Jumapili yaani sunday ilikuwa ni siku wapagani walikuwa wanaabudu jua. Wakati yesu yupo duniani mpaka anaondoka na kuwaacha wanafunzi wake muda wote huo walikuwa wanaadhimisha siku ya sabato kama siku ya ibada. Na hawa wote walikuwa wakristo, ambao walipitia mateso makali chini ya utawala wa kirumi ambao baadae walifanya muafaka kuwa wakristo wataendelea na sabato lakini inapofika jumapili waende makanisani. Historia ni ndefu, ukitaka nikujuze zaidi nitakujuza. Swala la wengi wanasali jumapili sio la kuangalia bali mwenyezi mungu anasema nini.
hili swali nililitegemea sana lakn kuna andiko linasema pasipo mimi ninyi hamuwezi kufanya lolote....hivi unajua hata majambazi/mafisadi/wezi wapo wanaomtegemea mungu na wanatoa zaka na sadaka? Seuse wewe? Ama badu wapo wanaomuomba mungu na wanatumia madesa bado..hii ni mada nyinginekwani wote wanaofaulu wanamcha mungu?
umesomeka, sasa toa ushauri wako kuhusu hawa wanafunzibinafsi, nimefuatilia sana majibu ya wadau wengi sana kwenye mjadala huu wa sabato. Na inayvyoonekana, wachangiaji wengi sana, hawaelewi maana ya sabato, chanzo cha sabato, umuhimu wa sabato na hatima ya sabato kwa muumini. Hilo ndilo tatizo la wengi hapa jamiiforum(nazungumzia wale tu waliojirusha kuchangia kwenye mjadala huu wa wanafunzi wasabato).
Aidha, wengine wamediriki hadi kuwatolea matusi wasabato hawa, jambo ambalo binafsi limenihuzunisha sana. Na wengi wana ushabiki tu usio na maana wa kimadhehebu na kidini wakitetea hoja mfu. Mungu si mwanadamu, hafikiri kama tunavyofikiri, wala hatendi kama tunavyotenda sisi. Ni mungu (yehova) asiyechunguzika kabisa.
Sabato siyo ya wayahudi, wala sabato haikuanzia kwa wayahudi wala mlimani sinai kama wengi wanavyofikiri. Sabato ndiyo ndilo pumziko takatifu la ibada kwa mungu, tangu hata milele zote. Pumziko hilo limetajwa tangu mwanzo hadi ufunuo.
Mtu yeyote anayewabishia wasabato ambao ndio watu pekee wanaoifuata biblia, na atuonyeshe ni wapi siku ya ibada ni jumapili au iujumaa au jumanne nk. Aende hadi kwenye biblia na quran asome akiona kuwa kuwa ijumaa, au jumapili ni ibada ya pumziko takatifu la m/mungu, aje, nitamzawadia milioni mbili za bure.
Tofauti na hapo, acheni na hampaswi kuwatukana na kwakejeli wasabato, maana hao ndio wanaoifuata biblia. Wengine ni wajasiliamali wa dini tu.
aisee, naona unahoji mamlaka za juu mno mkuu.......tufike mahala watu waelimishwe namna ya matumizi bora ya muda.fikiria uanze kuimba kuanzia ijumaa saa 12 jioni mpaka j2 tena saa 12jioni.je huo muda utatoka wapi katika ulimwengu huu wenye fursa adimu zinazoendana na muda?.
NADHANI HAPA KULIKUA NA MALIZE TU, NASIKIA WALIOTANGULIA WALIKUA WANAFANYA JUMAPILI kama kawa...........
angalau unaanza kusomeka kiushauri, lakn wamekata rufaa Baraza la Chuo limewatosa, waende wapi zaidi?chuo kimeugua kichaa, what is sunday anyway? wakate rufaa kwa kutumia sababu zinazofanya chuo kisifanye mitihani jumapili ndio hizo hizo zinazowazuia wao kufanya mtihani jumamosi.
angalau unaanza kusomeka kiushauri, lakn wamekata rufaa baraza la chuo limewatosa, waende wapi zaidi?