Wanafunzi wa Kisabato Wafukuzwa TEKU kwa Kukataa Kufanya Mitihani Siku ya Sabato naomba muongozo wa kisheria

Wanafunzi wa Kisabato Wafukuzwa TEKU kwa Kukataa Kufanya Mitihani Siku ya Sabato naomba muongozo wa kisheria

Umesema kweli kabisa Belinda, ila kuwa msabato si tiketi ya kwenda mbinguni, hili ndio wasabato wengi tunalisahau na kujiona tumesimama. Usengenyaji, uzinzi na uasherati vimetawala kwetu kama ambavyo vimetawala sehemu zingne......Ni kwa neema tu tuzidi kuombeana.

Atleast wewe umekuwa muwazi...Hebu waelimishe na wengine bana..
 
Watu tumefanya mitihani na presentation siku za pasaka na jumapili kwanini wasiwe wao? ngoja wajaribu kupima kipi kinawagharimu kati ya kuwepo mtaani sababu ya sabato na kufanya mtihani siku ya sabato. Jibu watalipata.
 
Watu tumefanya mitihani na presentation siku za pasaka na jumapili kwanini wasiwe wao? ngoja wajaribu kupima kipi kinawagharimu kati ya kuwepo mtaani sababu ya sabato na kufanya mtihani siku ya sabato. Jibu watalipata.

Ndugu yangu G.
Kwanza tambua kuwa Tanzania sio nchi ya kidini, imesaini mkataba wa UN wa haki za binadamu, kila mtu ana uhuru wa kufuata imani yake pasipo kubugudhiwa, kama Wasabato kwao siku ya Sabato ni siku takatifu na wanaamini hivyo kwanini kuwalazimisha iwe tofauti??? Hicho chuo kinavunja haki ya kuabudu ya binadamu.
Katika kuheshimu imani za watu wengine ndivyo tunavyofanya na wao kuheshimu imani zetu pia, huwezi kumlazimisha Msabato afanye mtihani siku yake takatifu ya Sabato kwa kuwa wewe huamini kama ni siku yake takatifu ya ibada hali kadhalika huwezi kumlazimisha Muislam ale nguruwe(kitimoto) ambayo kwake ni haramu ilihali kwako wewe huoni kama ni tabu.
Lazima tujue kuvumuliana kiimani ili tujenge jamii yenye furaha na kupenda nchi yao.
 
Umesema kweli kabisa Belinda, ila kuwa msabato si tiketi ya kwenda mbinguni, hili ndio wasabato wengi tunalisahau na kujiona tumesimama. Usengenyaji, uzinzi na uasherati vimetawala kwetu kama ambavyo vimetawala sehemu zingne......Ni kwa neema tu tuzidi kuombeana.

Tatizo kubwa kwenye usabato,ni kukataa kupokea roho mtakatifu.Ishara za kumpokea kama zilivyotajwa na maandiko,ni marufuku au si za muhimu kabisa kwa wasabato,hapo ndipo matatizo mengi yanaanzia.Kuna uigizaji mwingi kanisani na hasa kuiga wazungu!jinsi ya kuimba,muziki,kuvaa,na wakati mwingine hata kuongea lakini mioyoni watu wamejaa kiburi,majivuno,na kujiinua juu ya imani nyingine bila kutambua kwamba Mungu huliangalia kanisa lake kama mtu mmoja mmoja na siyo kikundi cha watu kilichosajiliwa marekani!Wengi wamedanganyika kuwa Mungu analitambua kanisa lake kwa jina la SDA!Lakini ukiangalia kwa umakini na kicho,utagundua si sahihi kuamini hivyo.Ila tangu Yohana mbatizaji hadi sasa,ufalme wa Mungu hupatikana kwa nguvu(roho mtakatifu)na wenye nguvu ndio watakaouteka!Soma maandiko,upate maarifa.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Kumbukumbu la Torati 5

1 Musa akawaita Israeli wote, akawaambia, Enyi Israeli, zisikieni amri na hukumu ninenazo masikioni mwenu leo, mpate kujifunza na kuangalia kuzitenda.
2 Bwana, Mungu wetu, alifanya agano nasi katika Horebu.
3 Bwana hakufanya agano hili na baba zetu, bali na sisi, yaani, sisi sote tuliopo hapa, tu hai.
4 Bwana alisema nanyi uso kwa uso mlimani, toka kati ya moto;

Mimi najiuliza hawa vijana wa TEKU walikuwa Hai siku agano hili linafanywa kama mstari wa tatu (3) na wanne (4) inavyoeleza?
 
Tatizo kubwa kwenye usabato,ni kukataa kupokea roho mtakatifu.Ishara za kumpokea kama zilivyotajwa na maandiko,ni marufuku au si za muhimu kabisa kwa wasabato,hapo ndipo matatizo mengi yanaanzia.Kuna uigizaji mwingi kanisani na hasa kuiga wazungu!jinsi ya kuimba,muziki,kuvaa,na wakati mwingine hata kuongea lakini mioyoni watu wamejaa kiburi,majivuno,na kujiinua juu ya imani nyingine bila kutambua kwamba Mungu huliangalia kanisa lake kama mtu mmoja mmoja na siyo kikundi cha watu kilichosajiliwa marekani!Wengi wamedanganyika kuwa Mungu analitambua kanisa lake kwa jina la SDA!Lakini ukiangalia kwa umakini na kicho,utagundua si sahihi kuamini hivyo.Ila tangu Yohana mbatizaji hadi sasa,ufalme wa Mungu hupatikana kwa nguvu(roho mtakatifu)na wenye nguvu ndio watakaouteka!Soma maandiko,upate maarifa.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums

Nina imani kuna siri kubwa kwenye sabato, ILA niko wazi kuufungua moyo wangu ili Mungu azidi kunifunulia kupitia roho wake ya nini hasa ni sahihi......Hata wewe kama huna kiburi cha uzima unaonaje ukiufungua moyo wako kuendelea kujifunza???
 
Wagalatia 3:23-29

Kabla ya kujaliwa imani, Sheria ilitufanya wafungwa mpaka imani hiyo iliyokuwa inakuja ifunuliwe. 24 Basi, hiyo Sheria ilikuwa kama mlezi wetu mpaka alipokuja Kristo, ili kwa njia ya imani, tukubaliwe kuwa waadilifu. 25 Tangu kufika kwa hiyo imani, Sheria si mlezi wetu tena. 26 Kwa njia ya imani, ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika kuungana na Kristo. 27 Ninyi nyote mliobatizwa mkaungana na Kristo ni kama vile mmemvaa Kristo. 28 Hivyo, hakuna tena tofauti kati ya Myahudi na Mgiriki, mtumwa na mtu huru, mwanamume na mwanamke. Nyote ni kitu kimoja katika kuungana na Kristo Yesu. 29 Ikiwa ninyi ni wa Kristo, basi ni wazawa wa Abrahamu, na mtapokea yale aliyoahidi Mungu.
 
[h=1]Luka 16 : 16[/h]16.16 "Sheria na maandishi ya manabii vilikuweko mpaka wakati wa Yohane mbatizaji. Tangu hapo, Ufalme wa Mungu unahubiriwa, na kila mmoja anauingia kwa nguvu
 
[h=1]2 Wakorintho 3: 12-16[/h]12 nasi si kama Musa alivyotia utaji juu ya uso wake, ili kwamba Waisraeli wasitazame sana mwisho wa ile iliyokuwa ikibatilika; 13 ila fikira zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi, wakati lisomwapo Agano la Kale, utaji uo huo wakaa; yaani, haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo;
14 ila hata leo, torati ya Musa isomwapo, utaji huikalia mioyo yao.
15 Lakini wakati wo wote watakapomgeukia Bwana, ule utaji huondolewa.
16 Basi <Bwana> ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru.
 
MAMBO YA KUTUNZA SABATO NI MAMBO YA KIZAMANI SANA.....Jumamosi ni siku kama siku nyingine:
Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku; mwinginie aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe. Yeye aadhimishaye siku huiadhimisha kwa Bwana" (Warumi 14:5-6a). "Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena? Mnashika siku, na miezi, na nyaktati, na miaka" (Wagalatia 4:9-10).

Waebrania 4: 4......
Kwa maana ameinena siku ya saba mahali fulani hivi, Mungu alistarehe siku ya saba, akaziacha kazi zake zote; - 5 na hapa napo, Hawataingia rahani mwangu. - 6 Basi, kwa kuwa neno hili limebaki kwamba wako watu watakaoingia humo, na wale waliohubiriwa habari ile zamani walikosa kuingia kwa sababu ya kuasi kwao, 7 aweka tena siku fulani, akisema katika Daudi baada ya muda mwingi namna hii, Leo; kama ilivyonenwa tangu zamani,
Leo, kama mtaisikia sauti yake,
Msifanye migumu mioyo yenu. -
8 Maana kama Yoshua angaliwapa raha, asingaliinena siku nyingine baadaye
 
Mengi ya ajabu kama yapi?..Nadhani ni bora kuziheshimu iqmbi na dini za wengine pia, maana kupitia "uajabu" huo watu wanaimani.

Yesu aliivyunjilia mbali sabato, alisema yeye ndio Sabato. kumfuata na kutenda anayofundisha kila siku ni sabato tosha. Sio siku moja kwa wiki bali ni kila siku
 
Yesu aliivyunjilia mbali sabato, alisema yeye ndio Sabato. kumfuata na kutenda anayofundisha kila siku ni sabato tosha. Sio siku moja kwa wiki bali ni kila siku

Sijjaelewa vizuri mkuu, kwa kusema "Mwana wa Adamu ndiye BWANA wa Sabato" ni kuivunja?..
Maana sijaona kwa ufahamu mdogo nilionao sijaona sehemu katika Maandiko isemavyo aliivunja(kama si tafsiri binafsi) mkuu.

Maana ndiye huyu huyu YESU aliyesema hakuja kubadilisha amri yeyote bali kuitimiliza, Wakayi fulani akisema "....chukua msalaba wako unifuate" akimwambia kikana tajiri..Sidhani kama akimaanisha kunifuata kila siku ndiyo Sabato.

Nasema hivi mkuu, maana ni amri MOJA tu inayoanza na neno IKUMBUKE (REMEMBER), na ndiyo nadhani inasahauliwa! Na hapa inasema siku sita fanya kazi (yaani kusiwe na kisingizio kwa siku sita za juma kuwa Tunamfuata MUNGU tu na hatuwezi kufanya "mambo" yetu mengine! ila katika siku saba ile siku moja iliyopewa UTUKUFU, KUBARIKIWA, KUTAKASWA kutufanya tuwe;
1. Karibu zaidi na MUNGU.
2. Kutukumbusha tumetoka wapi na dunia ni ya nani.
3. Kupata pumziko pia la kimwili kutoka kazi za siku sita.
 
Sichanganyi hata kidogo ila wewe ndiye naona unachanganya. Usisahau adui mkubwa wa msabato ni Mkatoliki..... Nikupe hiyo tena!

Nadhani, kama kuna Wasabato watakuwa wanaamini hivyo watakuwa wanakosea, nijuavyo ni kuwa YESU alisema kuwa "...na kondoo wengine ninao, si wa zizi hili, saa ikifika wataisikia sauti yangu, nao watanifuata na kuwa kundi moja..""..ikiwa regatdless of who takes to be right, some other point wapo wengi tuwafikirio kuwa "siyo" na hivyo macho na taswira zetu za kibinadamu huwa husema "yule akienda Mbinguni na mimi nitaenda" n.k. Lakini we (as human beings) are not in a position to judge.

Na mwisho, hao ambao wana UADUI na watu wa imani nyingine ni wenye matatizo maana shida ilikuwa/ni utawala wa Rumi na si wafuasi, pili hata kama ni "maadaui" basi watajuwa wanakosea, maana YESU alisema, ".. wapendeni adui zenu, na watendeeni mema wale wanaowaudhi.."
 
MaxShimba weye sio msabato...?? mbona unakula kitimoto
 
Last edited by a moderator:
Yesu aliivyunjilia mbali sabato, alisema yeye ndio Sabato. kumfuata na kutenda anayofundisha kila siku ni sabato tosha. Sio siku moja kwa wiki bali ni kila siku

Ni wagumu kulewa hao...Ndo maana huwa nawaita Mafarisayo..
 
Back
Top Bottom