Wanafunzi wa Kitanzania Ukraine waruhusiwa kuvuka mpaka wa Russia

Wanafunzi wa Kitanzania Ukraine waruhusiwa kuvuka mpaka wa Russia

Naipendatz

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2011
Posts
5,096
Reaction score
8,234
Wanafunzi wa Kitanzania walio katika mji wa Sumy nchini Ukraine wameruhusiwa kutoka nchini humo kupitia mpaka wa Russia baada ya mazungumzo ya kidiplomasia kufanyika na Serikali ya Russia kuridhia.

Kwa mujibu wa taarifa ya pamoja iliyotolewa leo Machi 4, 2022 na Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden na Ubalozi wa Tanzania nchini Urusi, shughuli ya kuwatoa wanafunzi wote kutoka Sumy hadi kwenye mpaka wa Russia, litaratibiwa na Serikali hiyo na tayari imeanza mipango ya utekelezaji.

“Wanafunzi hao watakapofika mpakani, Ubalozi wa Tanzania nchini Russia utawapokea kwa taratibu nyingine za kurejea nyumbani,” inaeleza taarifa hiyo ya Balozi hizo.

Taarifa hiyo inaeleza kwamba wakati shughuli ya kuwatoa wanafunzi walioko Sumy ikiendelea kuratibiwa, Balozi zinaomba wanafunzi hao pamoja na wazazi kuwa wavumilivu ili kuhakikisha wanatoka kwa usalama nchini Ukraine.

Mwananchi

My take:

Huu ndio uzuri wa kutofungamana na upande wowote, tungejifanya kiherehere hawa vijana wangepata shida sana. Huu mji wa Sumy upo mpakani wa Russia na Ukraine, ni mbali sana kuyafikia mataifa ambayo yanapokea wakimbizi wa Ukraine.
 
Kwa huyo kama tungekuwa tunafungamana na upande mmoja wapo ndio wangeamua kumalizia hasira zao kwa wananchi wake? mbona sijasikia wenyeji wa mataifa mengine ya ulaya magharibi wakinyanyaswa kwa sababu ya misimamo ya nchi zao?
 
Wanafunzi wa Kitanzania walio katika mji wa Sumy nchini Ukraine wameruhusiwa kutoka nchini humo kupitia mpaka wa Russia baada ya mazungumzo ya kidiplomasia kufanyika na Serikali ya Russia kuridhia.

Kwa mujibu wa taarifa ya pamoja iliyotolewa leo Machi 4, 2022 na Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden na Ubalozi wa Tanzania nchini Urusi, shughuli ya kuwatoa wanafunzi wote kutoka Sumy hadi kwenye mpaka wa Russia, litaratibiwa na Serikali hiyo na tayari imeanza mipango ya utekelezaji.

“Wanafunzi hao watakapofika mpakani, Ubalozi wa Tanzania nchini Russia utawapokea kwa taratibu nyingine za kurejea nyumbani,” inaeleza taarifa hiyo ya Balozi hizo.

Taarifa hiyo inaeleza kwamba wakati shughuli ya kuwatoa wanafunzi walioko Sumy ikiendelea kuratibiwa, Balozi zinaomba wanafunzi hao pamoja na wazazi kuwa wavumilivu ili kuhakikisha wanatoka kwa usalama nchini Ukraine.

Mwananchi

My take:

Huu ndio uzuri wa kutofungamana na upande wowote, tungejifanya kiherehere hawa vijana wangepata shida sana. Huu mji wa Sumy upo mpakani wa Russia na Ukraine, ni mbali sana kuyafikia mataifa ambayo yanapokea wakimbizi wa Ukraine.
Umewahi kusika kitu kinaitwa "Geneva Conventions"?
 
Umewahi kusika kitu kinaitwa "Geneva Conventions"?
Yap Chief, Vipi hiyo "Geneva Conventions" inasaidia chochote kwa mtu kichwa ngumu kama Putin? Mtu kama analikazia Baraza la Usalama la UN, hiyo Geneva ni nini kwake?
 
Kwa huyo kama tungekuwa tunafungamana na upande mmoja wapo ndio wangeamua kumalizia hasira zao kwa wananchi wake? mbona sijasikia wenyeji wa mataifa mengine ya ulaya magharibi wakinyanyaswa kwa sababu ya misimamo ya nchi zao?
Kunyanyaswa kwenye scenario ipi?
 
take:

Huu ndio uzuri wa kutofungamana na upande wowote, tungejifanya kiherehere hawa vijana wangepata shida sana. Huu mji wa Sumy upo mpakani wa Russia na Ukraine, ni mbali sana kuyafikia mataifa ambayo yanapokea wakimbizi wa Ukraine.
Kabisa kabisa
 
Back
Top Bottom