Wanafunzi wa sekondari kutoruhusiwa kuwa na simu shuleni ni sahihi?

Wanafunzi wa sekondari kutoruhusiwa kuwa na simu shuleni ni sahihi?

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Nimesoma uzi wa wanafunzi flani huko Singida wampata msala wa kukamatwa na Jeshi la Polisi baada ya kuchoma moto pikipiki ya mwalimu na kufyeka shamba la mwalimu huyo baada ya kumpa adhabu mwanafunzi mmoja aliyekutwa na simu.

Mwanafunsi huyo ni wa sekondari, binafsi hata mimi siungi mkono mchongo waliofanya hao wanafunzi, mimi nauita ni usela feki wa ujanani.

Lakini hoja ya msingi wadau tujadiline, hivi ni sahihi kweli kwa levo ya sekondari wanafunzi kutoruhusiwa kuwa na simu?

Dunia ya sasa kweli simu inazuilika? Nimewaza kwa nini simu wawe nazo lakini kuwe na masharti maaluma ya kutumia mfano kutotumika darasani au wakakti wa shughuli za shule, au labda wawe wanaenda nazo shuleni kisha zinakabidhiwa kwa uongozi wakati wa wikiendi wanakabidhiwa ili wawe wana focus na masomo siku za katikati ya wiki.

Mnaonaje hili wadau......
 
Wazee wa kutongoza watoto zetu naona mnataka simu wakae nazo bwenini sio?
 
Zama za teknolojia, sisi bado tuko gizani kwenye ujima….. simu ni kitu cha anasa.
 
Nimesoma uzi wa wanafunzi flani huko Singida wampata msala wa kukamatwa na Jeshi la Polisi baada ya kuchoma moto pikipiki ya mwalimu na kufyeka shamba la mwalimu huyo baada ya kumpa adhabu mwanafunzi mmoja aliyekutwa na simu.

Mwanafunsi huyo ni wa sekondari, binafsi hata mimi siungi mkono mchongo waliofanya hao wanafunzi, mimi nauita ni usela feki wa ujanani.

Lakini hoja ya msingi wadau tujadiline, hivi ni sahihi kweli kwa levo ya sekondari wanafunzi kutoruhusiwa kuwa na simu?

Dunia ya sasa kweli simu inazuilika? Nimewaza kwa nini simu wawe nazo lakini kuwe na masharti maaluma ya kutumia mfano kutotumika darasani au wakakti wa shughuli za shule, au labda wawe wanaenda nazo shuleni kisha zinakabidhiwa kwa uongozi wakati wa wikiendi wanakabidhiwa ili wawe wana focus na masomo siku za katikati ya wiki.

Mnaonaje hili wadau......
wazuiewe
waache watoto wasome, sisi wenyewe watu wazima zinatuchanganya
 
Ni sahihi, Sheria inaendana na Mtaala wa elimu ya Tanzania kwani elimu yetu inatuhitaji tuweze kukariri Sasa mtu akiwa na simu hahitaji kukariri Bali kuelewa
 
Mleta mada hebu tuwekane sawa hapa n chi gani ya dunia ya kwanza ambayo inaruhusu mwanafunz wa sekondar kumiliki simu shuleni?

Hata hao waliotuzid kiteknolojia bado wameweka wigo kati ya mtoto na matumiz ya simu hasa mazingira ya shule
 
Sahihi la sivyo bullying za kurekodiana wazi wazi zitaongezeka
 
Back
Top Bottom