Wanafunzi waliofaulu kidato cha kwanza Dar kusoma kwa zamu

Wanafunzi waliofaulu kidato cha kwanza Dar kusoma kwa zamu

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge leo Jumanne Januari 5 amesema wanafunzi waliofaulu kuingia kidato cha kwanza mwaka huu watasoma kwa zamu kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa katika mkoa huo.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya shule kwa ajili ya wanafunzi hao, Kunenge amesema wamefikia hatua,ili wengine wasibaki nyumbani na itakapofika Februari 28,2021 wataendelea na utaratibu wa kawaida.

"Tayari Mkoa umeomba kibali wanafunzi wetu wote waende shule japo kwa shift kutokana na uhaba wa madarasa ambapo wataanza Januari 11, 2021.

"Ila itakapofika Februari 28 ambapo ni agizo la Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuwa madarasa yawe yamekamilika na wanafunzi awamu ya pili wawe wameingia darasani wataendelea na utaratibu wa kawaida wa kwenda wote asubuhi," amefafanua Kunenge.
 
Baada ya kutafuta sifa ya kufaulisha tu ionekane awamu ya 5 ufaulu unapanda kila mwaka madhara yake ndio hayo, hapo kuna watoto kibao hawana sifa za kwenda kidato cha Kwanza na miongoni mwao Hawajui kusoma wala kuandika ila kikubwa waeenda kidato cha Kwanza.
 
Kwani swala la kuongezeka kwa wanafunzi ni la ghafla!? Mbona tunafanywa mazuzu kiasi hiki!?
 
Haya mambo yanachekesha sana, hivi serikail uwa inafail wapi. Idadi ya wanafunzi kila mkoa watakaomaliza inakuwaga nayo, sasa sijui kwanini uwa wanasubiri wazime moto.
Wazazi wanatotoa kila siku huwezi pia huwezi Kujua idadi ya watakaofaulu mitihani sababu kufaulu sio predictable
 
Wazazi wanatotoa kila siku huwezi pia huwezi Kujua idadi ya watakaofaulu mitihani sababu kufaulu sio predictable
Mkuu mbona tunaambiwa na takwimu tunapewa kwamba ufaulu unaongezeka kila mwaka sasa kwanini usiwe na makadirio ya juu ya mwaka unaofuata ili kuendana na takwimu.
 
Hivi hizi sarakasi ni za kiku** sana!? Kwani swala la kuongezeka kwa wanafunzi ni la ghafla!? Mbona tunafanywa mazuzu kiasi hiki!?
Fomu one mtu anatakiwa afaulu mtihani wewe tupe takwimu mtihani ujao wa darasa la saba wangapi watafaulu?ufaulu utaongexeka au utashuka au utakuwa constant?

Pili kuna wengine pamoja na kufaulu hawataenda kuripoti shule za serikali wazazi wao watawapeleka shule za sekondari za private tupe takwimu za mwakani wewe Watoto wangapi watapelekwa private na wazazi wao na watakaobaki kuripoti shule za serikali ni wangapi?
 
Kuna wilaya na mikoa mengine watoto wamefaulu kwa wastani wa 'C' wamepata shule (selection). Bado hapa Dar Kuna watoto wamepata wastani wa 'B' Tena wengi hawajachaguliwa (selection) shule yeyote. Yeye anaongelea hao tu waliochaguliwa. Je hawa waliofaulu?

Aache uzemb* apambane kama Bashite.
 
Halafu still mnawaambia wazaliane kumbe hata huduma za jamii kama Elimu ,afya hata majengo tu hamna. Nchi haina mipango hii kutwa kuropoka tu.
Nchi zenye manilionea wakubwa duniani zina population kubwa

Watu wakiwa wengi fikiria muuxs uniform atakavyopiga pesa muuxs stationery muuza vitabu vya shule

Muuxs nguo za Watoto atapiga pesa ndefu sana watu wakizalians sana

Muuza vyakula kama Azam anauza sana sababu ya population kubwa

Biashara ziwe za daladala bodaboda zinaongezeka population ikiongezeka nk

Population kuongexeka sio tatizo inategemea unatizama kupitia angle ipi?ya utajiri au maskini angle yako unayoongelea wewe ni ya kimaskini
 
Mkuu mbona tunaambiwa na takwimu tunapewa kwamba ufaulu unaongezeka kila mwaka sasa kwanini usiwe na makadirio ya juu ya mwaka unaofuata ili kuendana na takwimu.
Uko sahihi kabisa mkuu.
 
Kwani swala la kuongezeka kwa wanafunzi ni la ghafla!? Mbona tunafanywa mazuzu kiasi hiki!?
Ndiyo ni la ghafla,
Wanafunzi Wanapoingia Darasa la saba,huwa wanaomgezeka Kama matone ya mvua!
 
Wazazi wanatotoa kila siku huwezi pia huwezi Kujua idadi ya watakaofaulu mitihani sababu kufaulu sio predictable
Siku hizi ufaulu unakuwa wa juu kuliko wanaofail inabidi watumie mbinu za statistics, kutabiri matokeo. Mbona mbinu hizo hizo zinatumika katika kubashiri ongezeko la watu, magari, vifo na kadhalika.
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge leo Jumanne Januari 5 amesema wanafunzi waliofaulu kuingia kidato cha kwanza mwaka huu watasoma kwa zamu kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa katika mkoa huo.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya shule kwa ajili ya wanafunzi hao, Kunenge amesema wamefikia hatua,ili wengine wasibaki nyumbani na itakapofika Februari 28,2021 wataendelea na utaratibu wa kawaida.

"Tayari Mkoa umeomba kibali wanafunzi wetu wote waende shule japo kwa shift kutokana na uhaba wa madarasa ambapo wataanza Januari 11, 2021.

"Ila itakapofika Februari 28 ambapo ni agizo la Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa kuwa madarasa yawe yamekamilika na wanafunzi awamu ya pili wawe wameingia darasani wataendelea na utaratibu wa kawaida wa kwenda wote asubuhi," amefafanua Kunenge.
Mitano tenaaaaaa
 
Nchi zenye manilionea wakubwa duniani zina population kubwa

Watu wakiwa wengi fikiria muuxs uniform atakavyopiga pesa muuxs stationery muuza vitabu vya shule

Muuxs nguo za Watoto atapiga pesa ndefu sana watu wakizalians sana

Muuza vyakula kama Azam anauza sana sababu ya population kubwa

Biashara ziwe za daladala bodaboda zinaongezeka population ikiongezeka nk

Population kuongexeka sio tatizo inategemea unatizama kupitia angle ipi?ya utajiri au maskini angle yako unayoongelea wewe ni ya kimaskini
Stupid idea. Kama hao population ni masikini unategemea nini?Vicious cycle siyo ?
 
Back
Top Bottom