Wanafunzi waliofaulu kidato cha kwanza Dar kusoma kwa zamu

Hivi yule mama kigezo gani kimesaidia walau kumrudisha kwenye Wizara ya Elimu!?
 
Kujilipa mishahara posho kutembelea ma veiteee na sio kuwahudumia wapuuzi masikini kama wewe
😁😁😁😁😁 Tanzania ni nchi yangu..

Mkuu niko geto mwenyewe nimecheka sana kwa majibu yako!
 
Kujilipa mishahara posho kutembelea ma veiteee na sio kuwahudumia wapuuzi masikini kama wewe
Daaah machozi yamenitoka.Kila mtu asali kwa imani yake labda na sisi tunaweza kuyaendesha kwa Mungu
 
Hivi yule mama kigezo gani kimesaidia walau kumrudisha kwenye Wizara ya Elimu!?
Mimi nilishajiuliza maswali mengi sana angalau hata angepewa kitila mkumbo au January Makamba wako Creative huyu mama amna kitu kabisa
 
Yeye anafanya nini?! Katika wizara yake?! Yupo yupo tuuuu hajui anasimamia nini.
 
Suala la Madarasa wanaotakiwa kushutumiwa Ni viongozi wote wanaohusika na kujengwa hayo madarasa waliokuwepo kipindi hao madogo wanamaliza darasa la Saba,
 
Hili tatizo la upungufu wa madarasa tulizoee
Tutakuwa halo now and then
 
Wanafunzi wanaongezeka na madarasa yanaongezwa ingawa kwa kusuasua.Swali ni je, ongezeko hili linaenda sambamba na kuongeza idadi ya walimu na vifaa vya kufundishia?

Kama una uwezo, mwanao mmepeleke private.
 
Acheni Kumsukumizia lawama Waziri Profesa Ndalichako leo hii na ukweli ni kwamba Elimu ya Tanzania ipo Kaburini tokea mwaka 2005 hadi sasa.
 
Chuo Shift! Secondary shift! Tuko vizuri 5 tena
 
Lakini serikali na jamii haiamini kabisa kwa walimu
Ni sawa na kutafuta house girl ambae hana akili sawasawa halafu unampa akuletee mwanao
Sijui nani anakuwa hana akili hapo
 
Mimi najiuliza hivi:

Wizara ya Elimu ina

1. Maafisa Elimu Mkoa

2. Maafisa Elimu Wilaya

Ambao kazi yao kubwa ni Ku coordinate Maswala yote ya Elimu.

Ongezeko la Watoto kwa mfano kwa mwaka huu lilijulikana tokea Enrollment yao wakiwa Darasa la Kwanza; Mtihani wa kuvuka Darasa la 4.

Sasa hawa Maafisa Elimu walikuwa wapi ku oversee na Kumitigate hili Tatizo.

Mpaka Waziri Mkuu na Waziri wa TAMISEMI kuamua kuingilia Kati.

Ina maana kila Mwaka hali itakua ndio hivi hivi?

Ingekua ni kwenye Financial Institutions ambazo zenyewe ni Matokeo ni Faida au Hasara ( Profit or Loss) ina maana Makampuni karibu yote yangeshapata Hasara kubwa sana kutokana na kushindwa kwa Managers ku forecast and Ku-Mitigate Risks!!!

Kila Mwaka Sekta ya Elimu ( Msingi na Sekondari) zimekua na Matatizo ya Zimamoto katika
1. Upungufu wa Vyumba vya Madarasa
2. Upungufu wa Viti vya Kukalia
Ni wakati umefika Wahusika kujirekebisha kwa mapungufu yao.
Kama tatizo ni Wakurugenzi wa Manispaa na Halmashauri basi ikiwezekana idara za Elimu zirudishwe katika Wizara Husika kama Miaka ya Zamani.
 
Wazazi wanatotoa kila siku huwezi pia huwezi Kujua idadi ya watakaofaulu mitihani sababu kufaulu sio predictable
Hapo tunadanganyana ndugu,unaweza kupredict Ila maafisa takwimu wavivu tu, kwa mfano

Afisa elimu kata anajua katani kwake Kuna sekondari ngapi na wakimaliza kidato Cha nne November kutakua na nafasi ngapi,pia anajua Ana shule ngapi za msingi katani kwake na Kila shule Ina darasa la Saba wangapi, akiweka 80 asilimia watafaulu, akalinganisha na nafasi za kidato Cha kwanza hajapata jibu, automatically atakua anajua wangapi watakosa nafasi katani kwake,na Hilo wanalipeleka kwenye kikao Cha maendeleo ya kata kujadiliwa.

Peke yangu nikiwezeshwa usafiri naweza fanya prediction 2021 kwa DSM au mkoa wowote standard seven watafaulu wangapi na nafasi ziko ngapi na wangapi watakosa madarasa.

The problem,watendaji wa Chini hawako seriously,hawawasaidii presidaa,w mkuu na makamo wa rais,
 
Wazazi wanatotoa kila siku huwezi pia huwezi Kujua idadi ya watakaofaulu mitihani sababu kufaulu sio predictable
Tunafuata tamko la rais, tunafyatuana kweli kweli. Au ninasema uongo ndugu zangu?
 
Hapo tunadanganyana ndugu,unaweza kupredict Ila maafisa takwimu wavivu tu, kwa mfano...
Hufai kabisa kuwa afisa takwimu huyo afisa elimu kata hana uwezo huo Watoto wakifaulu hawapangiwi shule za secondary za kama yake tuhupangiwa me hata ya kama zao au hata za Bweni mikoa mingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…