Wanafunzi waliokosa mkopo ina maana pesa hazipo? Mnakubali hivi hivi tuu... Wadau mnaonaje?

Hii ndio tanzania..pesa wanakula wenyewe,..wanafunzi wa chuo dodoma walinyimwa ela zao na field hivo hivo.
 
hili ni jukwaa huru ambalo kila mtu ana uhuru wa kutoa mawazo yake.................kama wewe ni great thinker ,usitegemee kuungwa mkono kwa kila unachokisema.budget constraints ni kitu cha kawaida kabisa,labda suala la msingi ni kujiuliza kwamba ni kweli wote walioomba mkopo wana uhitaji wa mkopo?tunaweza kujadili kwa kina vigezo vya kutoa mkopo,je ni sahihi au la?vigezo husika vimefuatwa?wanufaika wa mikopo hiyo ya elimu ya juu wanawajibika(accountable)kulipa ili wengine wafaidike?na vitu kama hivyo.lakini pia unaweza kujiuliza idadi ya wanafunzi wanaochaguliwa kwenda kusoma shule za serikali(wakati mwingine hata sio shule za kata)wanaoamua kuachia nafasi zao na kwenda kusoma shule za binafsi ambazo ada zake ni kubwa mara nyingine hata kuliko gharama za kusoma chuo.watu hawa wakifika chuo wanasema hawana uwezo,je ni sawa?hili sio tatizo?labda utaniambia wanafuata ubora wa elimu kwenye shule binafsi,sikatai,basi pia wajiandae kwa kwa gharama za kusoma chuo................naomba kuwasilisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…