kibogo
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 9,739
- 4,742
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo amesema kufeli kwa baadhi ya wanafunzi hakutokani na walimu kutokamilisha mitaala bali kutokana na uzembe wa wanafunzi wenyewe, waziri alitoa kauli hiyo jana 04.10.2012 jijini Dar alipokuwa akitoa taarifa kuhusu mtihani wa kidato cha nne na mtihani wa maarifa inayotarajiwa kuanza Oct 8 25.
Kwa kauli yake amesema wanafunzi wanaotoa madai hayo wengi wao ni wale waliokuwa wakishindwa kuwasikiliza walimu wakati wakifundisha darasani na alisema kwa kawaida mfa maji aachi kutapatapa hivyo hao wanaosema kwamba walimu hawamalizi mitaala mara nyingi ni wale waliokuwa wakipata sifuri tangu awali.
My Take.
1. Hivi huyu naibu waziri anajua anachokisema au anaonge kwa sababu watoto wao hawasomi shule za mchangani?
2. Tumeshuhudia mgomo wa walimu ambao serikali imeshindwa kutekeleza madai yao ya msingi, hivyo walimu watakuwa wanafanya kazi ipasavyo? Kama sio je watamaliza mitaala katika kufundisha hata kama watamaliza je watafundisha ili mwanafunzi aelewe au bora kipindi kiishe?
3. Tumeshuhudia matokea ya Form 4 mwaka jana 89% karibia na 90% walifeli inamaanisha amekwisha sahau matokeo hayo na je serikali inajua sababu ya kufeli huko kwa hao wanafunzi?
4. Shule nyingi za kata zimejengwa lakini nyingi zina walimu wasiozidi 3 je wanaweza kufundisha ipasavyo? Na anashindwa kuelewa kwamba hicho ndo chanzo cha wanafunzi wengi kufeli
5. Na je kama mwanafunzi alikuwa anapata sifuri tangu awali kwa nini wameufuta mtihani wa kidato cha pili ambao ulikuwa ni muhimu kwa ajili ya kumpima mtoto kabla ajavuka kwenda kidato cha tatu?
6. Na bado tumeshuhudia kuboronga kwa wizara hii kwa kuweka maswali ya multiple choice ya hesabu kwa mtihani wa Darasa la saba waliomaliza hivi karibuni hapo tusitegemee kuboresha somo la hesabu kwani mtoto anaweza kuwa hajui hesabu lakini akabuni nakubahatisha akaongoza kitaifa.
**Chanzo cha habari hii ni Tanzania Daima**
Kwa kauli yake amesema wanafunzi wanaotoa madai hayo wengi wao ni wale waliokuwa wakishindwa kuwasikiliza walimu wakati wakifundisha darasani na alisema kwa kawaida mfa maji aachi kutapatapa hivyo hao wanaosema kwamba walimu hawamalizi mitaala mara nyingi ni wale waliokuwa wakipata sifuri tangu awali.
My Take.
1. Hivi huyu naibu waziri anajua anachokisema au anaonge kwa sababu watoto wao hawasomi shule za mchangani?
2. Tumeshuhudia mgomo wa walimu ambao serikali imeshindwa kutekeleza madai yao ya msingi, hivyo walimu watakuwa wanafanya kazi ipasavyo? Kama sio je watamaliza mitaala katika kufundisha hata kama watamaliza je watafundisha ili mwanafunzi aelewe au bora kipindi kiishe?
3. Tumeshuhudia matokea ya Form 4 mwaka jana 89% karibia na 90% walifeli inamaanisha amekwisha sahau matokeo hayo na je serikali inajua sababu ya kufeli huko kwa hao wanafunzi?
4. Shule nyingi za kata zimejengwa lakini nyingi zina walimu wasiozidi 3 je wanaweza kufundisha ipasavyo? Na anashindwa kuelewa kwamba hicho ndo chanzo cha wanafunzi wengi kufeli
5. Na je kama mwanafunzi alikuwa anapata sifuri tangu awali kwa nini wameufuta mtihani wa kidato cha pili ambao ulikuwa ni muhimu kwa ajili ya kumpima mtoto kabla ajavuka kwenda kidato cha tatu?
6. Na bado tumeshuhudia kuboronga kwa wizara hii kwa kuweka maswali ya multiple choice ya hesabu kwa mtihani wa Darasa la saba waliomaliza hivi karibuni hapo tusitegemee kuboresha somo la hesabu kwani mtoto anaweza kuwa hajui hesabu lakini akabuni nakubahatisha akaongoza kitaifa.
**Chanzo cha habari hii ni Tanzania Daima**