Wanafunzi wanaosoma shule msingi Msimba Mikumi wanatembea umbali mrefu sana kwenda shule. Serikali waonee huruma Watanzania hawa

Wanafunzi wanaosoma shule msingi Msimba Mikumi wanatembea umbali mrefu sana kwenda shule. Serikali waonee huruma Watanzania hawa

Kyambamasimbi

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
762
Reaction score
1,597
Habari wanaJF.

Jamani, nimeexperience mara kadhaa nikiwa nasafiri barabara ya Iringa kutoka Morogoro, huwa naona watoto wadogo wa shule ya msingi Msimba wakitembea umbali mrefu kufuata shule iliko. Mbaya zaidi, wakati wa masika huwa wanatia huruma sana watoto hawa, na huwa wananyooka wakitembea pembezoni mwa barabara kuu yenye malori na mabasi.

Jamani, mwenzenu huwa naumia moyo juu ya watoto wale. Kuna siku nilimuomba dereva awabebe, na nilivyowashusha walifurahi na kushukuru kwa kupiga magoti. Jamani, kimoyomoyo niliwaombea, "Eeeeeee Mungu, wakumbatie watoto wako."

Serikali, wasogezee watoto hawa shule angalau wafarijike wajione ni sehemu ya Watanzania. Jamani, huwa naumia sana sijui kwa sababu nimekulia shida?

Naomba kuwasilisha.
 
Waachwe hivohivo hao ndio watakuja kusaidia taifa kwa baadae maana watakua wakakamavu na wenye machungU
 
Nakuelewa Mkuu, watu wenye huruma tupo hivyo. Hapo utakuwa unawawazia sana. Bahati mbaya Serikali ya chura kiziwi, sasa hivi iko na bodaboda, wasanii. Kampeni wamezianza. Shule hizo labda wananchi tuchangishane, watoto waondokane na hiyo kadhia.
 
Nakuelewa Mkuu, watu wenye huruma tupo hivyo. Hapo utakuwa unawawazia sana. Bahati mbaya Serikali ya chura kiziwi, sasa hivi iko na bodaboda, wasanii. Kampeni wamezianza. Shule hizo labda wananchi tuchangishane, watoto waondokane na hiyo kadhia.
Hakika mkuu roho inauma mkuu
 
Waendesha pikipiki za kijani watakwambia, Mama anaupiga mwingi.

Nadhani mpaka sasa kimoyoni, Yule mzee mwenye gwanda anajuta kuwakatalia wale walotaka kupindua katiba na kumweka mtu mwingine..

Tumeona madhara ya urithi..
 
Habar wanjf. Jamani nmexperience mara kadhaa nikiwa nasafiri Barbara ya Iringa kutoka Morogoro huwa naona watoto wadogo wa shule ya msingi Msimba wakitembea umbali mrefu kufuata shule iliko. Mbaya zaidi wakati wa masika huwa wanatia huruma watoto Hawa, na huwa wananyooka wakitembea pembezoni mwa Barbara kuu yenye malori na mabasi. Jamani mwenzenu huwa naumia moyo juu ya watoto wale. Kuna nilimuomba dereva awabebe nivyowashusha walifurahi na kushukuru kwa kupiga magoti jamani.......... Kimoyomoyo niliwaombea Eeeeeee Mungu Wakumbatie watoto wako. Serikali wasogezee watoto Hawa shule angalau wafarijike wajione ni sehemu ya watanzania. Jamani huwa naumia sijui kwa Sababu nimekulia shida?? Naomba kuwasilisha.
Akina Juniors acheni kudeka, Kizazi cha 1920-1980s tulisoma shule za umbali wa km 26 na tulikomaa kiumeni bila kulia lia, mnakwama wapi?

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
 
Habar wanjf. Jamani nmexperience mara kadhaa nikiwa nasafiri Barbara ya Iringa kutoka Morogoro huwa naona watoto wadogo wa shule ya msingi Msimba wakitembea umbali mrefu kufuata shule iliko. Mbaya zaidi wakati wa masika huwa wanatia huruma watoto Hawa, na huwa wananyooka wakitembea pembezoni mwa Barbara kuu yenye malori na mabasi. Jamani mwenzenu huwa naumia moyo juu ya watoto wale. Kuna nilimuomba dereva awabebe nivyowashusha walifurahi na kushukuru kwa kupiga magoti jamani.......... Kimoyomoyo niliwaombea Eeeeeee Mungu Wakumbatie watoto wako. Serikali wasogezee watoto Hawa shule angalau wafarijike wajione ni sehemu ya watanzania. Jamani huwa naumia sijui kwa Sababu nimekulia shida?? Naomba kuwasilisha.
halmashauri ndiyo iwajibishwe, hivi hawaoni vitu kama hivyo? Unaweza kuta tayari bajeti imewekwa lakini ikatumika kwa mambo mengine.

Hebu weka vizuri ni halmashauri gani hiyo?
 
Binafsi nilikutana na watoto wanatembea maeneo ya barabara ya Iringa maeneo ya Iyovi porini kuelekea shule tena wadogo sanaa.Nashukuru dereva wa basi la ABC Mungu amtunze aliwabeba na kuwasogeza mpaka maeneo ya shule.Hakika ni mbali sana ni zaidi ya km 20 mpaka nikafikiri dereva amesahau kuwashusha hawa watoto.
 
Angesema ni wapi huko.maana kwa sasa serikali ya Rais Samia imejenga shule nyingi sana hadi shikizi maeneo mbalimbali nchini.
Tena wewe Mpuuzi msifia ujinga.wale watoto wanateseka mbwa wewe.unakalia kusifia mama mama.
Wapo Iyovi wanasoma katikati hapa kabla hujafika mikumi njia ya Iringa, ni zaidi ya Km 20 Wale madogo wanatembea.
We kalia kusema mama anatosha unadhambi sana ya unafki wewe.mimi dua zangu usipate uteuzi wala CCm iskukukumbuke ufe maskini nyau wewe.
 
Binafsi nilikutana na watoto wanatembea maeneo ya barabara ya Iringa maeneo ya Iyovi porini kuelekea shule tena wadogo sanaa.Nashukuru dereva wa basi la ABC Mungu amtunze aliwabeba na kuwasogeza mpaka maeneo ya shule.Hakika ni mbali sana ni zaidi ya km 20 mpaka nikafikiri dereva amesahau kuwashusha hawa watoto.
Hakika mkuu mm huwa naumia kweli na sahihi maeneo hayohayo sidhani kama huwa wanaelewa darasani baada ya kuchoka
 
Tena wewe Mpuuzi msifia ujinga.wale watoto wanateseka mbwa wewe.unakalia kusifia mama mama.
Wapo Iyovi wanasoma katikati hapa kabla hujafika mikumi njia ya Iringa, ni zaidi ya Km 20 Wale madogo wanatembea.
We kalia kusema mama anatosha unadhambi sana ya unafki wewe.mimi dua zangu usipate uteuzi wala CCm iskukukumbuke ufe maskini nyau wewe.
Mwambie mkuu yaani huyu jamaa anakera.
 
Hakika mkuu mm huwa naumia kweli na sahihi maeneo hayohayo sidhani kama huwa wanaelewa darasani baada ya kuchoka
Nakumbuka ile siku mama mmoja akaanzisha kuwapa Wale watoto hela ,karibia basi zima tulitoa tulichonacho walau wakanunue maftari.Mbaya zaidi kulikua na manyunyu na ukungu.niliumia sana.
Nikamuangalia binti yangu pembeni nikabaki namshukuru Mungu kwa kidogo anachotupa.Tulikua tunatoka Iringa.
 
Nakumbuka ile siku mama mmoja akaanzisha kuwapa Wale watoto hela ,karibia basi zima tulitoa tulichonacho walau wakanunue maftari.Mbaya zaidi kulikua na manyunyu na ukungu.niliumia sana.
Nikamuangalia binti yangu pembeni nikabaki namshukuru Mungu kwa kidogo anachotupa.Tulikua tunatoka Iringa.
Yaani Mungu aingilie kati awatie nguvu watoto kama huna mtoto unaweza kurahisisha na kuchangizia ujinga kwenye Uzi huu
 
Back
Top Bottom