Eneo hilo ndipo inapopatikana shule analiyotaja mwanzisha mada? -Binafsi nilikutana na watoto wanatembea maeneo ya barabara ya Iringa maeneo ya Iyovi porini kuelekea shule tena wadogo sanaa.Nashukuru dereva wa basi la ABC Mungu amtunze aliwabeba na kuwasogeza mpaka maeneo ya shule.Hakika ni mbali sana ni zaidi ya km 20 mpaka nikafikiri dereva amesahau kuwashusha hawa watoto.
Inasikitisha snNakuelewa Mkuu, watu wenye huruma tupo hivyo. Hapo utakuwa unawawazia sana. Bahati mbaya Serikali ya chura kiziwi, sasa hivi iko na bodaboda, wasanii. Kampeni wamezianza. Shule hizo labda wananchi tuchangishane, watoto waondokane na hiyo kadhia.
Siyo hapo tu, nenda kuanzia Makambako mpaka Chimala hali ni hiyohiyo, Makambako watoto wanatembea kando ya barabara huku wamevaa gauni na suruali ndani pamoja na kofia za kufuma kuzuia baridi kali na upepo mkali wa Makambako utawahurumia.Habari wanaJF.
Jamani, nimeexperience mara kadhaa nikiwa nasafiri barabara ya Iringa kutoka Morogoro, huwa naona watoto wadogo wa shule ya msingi Msimba wakitembea umbali mrefu kufuata shule iliko. Mbaya zaidi, wakati wa masika huwa wanatia huruma sana watoto hawa, na huwa wananyooka wakitembea pembezoni mwa barabara kuu yenye malori na mabasi.
Jamani, mwenzenu huwa naumia moyo juu ya watoto wale. Kuna siku nilimuomba dereva awabebe, na nilivyowashusha walifurahi na kushukuru kwa kupiga magoti. Jamani, kimoyomoyo niliwaombea, "Eeeeeee Mungu, wakumbatie watoto wako."
Serikali, wasogezee watoto hawa shule angalau wafarijike wajione ni sehemu ya Watanzania. Jamani, huwa naumia sana sijui kwa sababu nimekulia shida?
Naomba kuwasilisha.
Kata hiyo ina shule moja tu mkuu?Hao Wanafunzi nami nimewahi kuwaona mara kadhaa wakiomba hata lift kwenye mabasi ama magari binafsi ili waelekee Shule.
Sisi tuliokua zamani, ilikuwa tunasafiri Umbali kama huo ama zaidi ili kwenda Shule, lakini haifai maisha yale na Vijana wetu wayaishi.
Halmashauri inakusanya mapato, lakini pia hata Serikali KUU ione namna ya kusaidia kumaliza hili tatizo.
Shule inaitwa Msimba Shule ya Msingi, Ipo kwenye Kata ya Mikumi, Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa. Ni Moja wapi ya Shule za zamani zamani kidogo, nahisi kwenye miaka ya 2000 hivi imeanza
DED, Mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na Mbunge wa Jimbo la Mikumi waone namna ya kusaidia kuondoa hili tatizo.
bitimkongwe Lucas Mwashambwa
Kata ya Mikumi ni Moja ya Kata kubwa na kongwe yenye Shule za Msingi zaidi ya 10 kama sikosei.Kata hiyo ina shule moja tu mkuu?
kuna dereva mmoja wa al saedy ya iringa anaitwa mengi kasike huwa anawabeba sana hao watoto anapokutana nao njiani na wanamjua na kumpenda sana dereva yule. nafikiri kuna dereva mwingine am madereva wa mabasi kuwa na moyo kama huu.Habari wanaJF.
Jamani, nimeexperience mara kadhaa nikiwa nasafiri barabara ya Iringa kutoka Morogoro, huwa naona watoto wadogo wa shule ya msingi Msimba wakitembea umbali mrefu kufuata shule iliko. Mbaya zaidi, wakati wa masika huwa wanatia huruma sana watoto hawa, na huwa wananyooka wakitembea pembezoni mwa barabara kuu yenye malori na mabasi.
Jamani, mwenzenu huwa naumia moyo juu ya watoto wale. Kuna siku nilimuomba dereva awabebe, na nilivyowashusha walifurahi na kushukuru kwa kupiga magoti. Jamani, kimoyomoyo niliwaombea, "Eeeeeee Mungu, wakumbatie watoto wako."
Serikali, wasogezee watoto hawa shule angalau wafarijike wajione ni sehemu ya Watanzania. Jamani, huwa naumia sana sijui kwa sababu nimekulia shida?
Naomba kuwasilisha.
Habari wanaJF.
Jamani, nimeexperience mara kadhaa nikiwa nasafiri barabara ya Iringa kutoka Morogoro, huwa naona watoto wadogo wa shule ya msingi Msimba wakitembea umbali mrefu kufuata shule iliko. Mbaya zaidi, wakati wa masika huwa wanatia huruma sana watoto hawa, na huwa wananyooka wakitembea pembezoni mwa barabara kuu yenye malori na mabasi.
Jamani, mwenzenu huwa naumia moyo juu ya watoto wale. Kuna siku nilimuomba dereva awabebe, na nilivyowashusha walifurahi na kushukuru kwa kupiga magoti. Jamani, kimoyomoyo niliwaombea, "Eeeeeee Mungu, wakumbatie watoto wako."
Serikali, wasogezee watoto hawa shule angalau wafarijike wajione ni sehemu ya Watanzania. Jamani, huwa naumia sana sijui kwa sababu nimekulia shida?
Naomba kuwasilisha. Hayo yapo sehemu nyingi hapa Tanganyika
Umesema vizuri kabisa, hii nchi wanajijali watawala waishi vizuri na kifahari, kuliko wananchi. Fikiria tu mbunge anakuwa ndiyo tajiri anaowawakilisha ni masikini wa kupindukia.Hivi serikali hua inashindwa kununua magari maalum Kwa ajili ya kubeba hawa watoto wanaosafiri umbali mrefu kufuata shule, mbona magari yao ya million 300 wanaweza kuyanunua
Mikoa mingi tu hali ipo hivi, Lindi kuna vijiji watoto wanavuka na mitumbwi kila siku kwenda shule lakini hakuna kiongozi anaeshituka labda mpaka yatokee maafa
Matendo yetu watu weusi yanafikirisha sana