Filosofia ya Rorya
JF-Expert Member
- Sep 20, 2021
- 3,211
- 3,611
Kumekuwa na mkanganyiko kuhusu mimba mashuleni ambapo tafsiri na mitazamo huelemea wanafunzi wa kike wanaopewa mimba na watu (wakiwemo Walimu) huku wanafunzi wa kiume wanaotia mimba Walimu wao wa kike wakiachwa nje ya tafsiri na mitazamo hiyo.
Zipo jamii katika nchi za Tanzania na Kenya ambapo kwa mujibu wa mila zao e.g. Wakurya, unakuta mwanafunzi wa kiume ameoa Mwalimu wake na anaendelea na masomo kama kawaida.
Aidha, nimewahi kushuhudia kesi ambapo wazazi wanapinga kufukuzwa shule mtoto wao wa kiume kwa kosa la kumtia Mwalimu wake mimba; wakidai kwamba Mwalimu ndiye afukuzwe kazi badala ya mwanafunzi kwamba utovu wa nidhamu hauko kwa mwanafunzi bali kwa Mwalimu wake huyo.
Waraka wa Waziri wa Elimu (hivi karibuni) kuhusu wanafunzi wenye mimba kuendelea na masomo haukujibu maswali ya tafsiri na mitazamo hiyo.
Taswira kwa hisani ya google
Zipo jamii katika nchi za Tanzania na Kenya ambapo kwa mujibu wa mila zao e.g. Wakurya, unakuta mwanafunzi wa kiume ameoa Mwalimu wake na anaendelea na masomo kama kawaida.
Aidha, nimewahi kushuhudia kesi ambapo wazazi wanapinga kufukuzwa shule mtoto wao wa kiume kwa kosa la kumtia Mwalimu wake mimba; wakidai kwamba Mwalimu ndiye afukuzwe kazi badala ya mwanafunzi kwamba utovu wa nidhamu hauko kwa mwanafunzi bali kwa Mwalimu wake huyo.
Waraka wa Waziri wa Elimu (hivi karibuni) kuhusu wanafunzi wenye mimba kuendelea na masomo haukujibu maswali ya tafsiri na mitazamo hiyo.
Taswira kwa hisani ya google