Wanafunzi wenye UKIMWI Kibaha wawekewa Label!

Mwalimu mkuu naye apigwe lebo, make kazi zimemzidia ndo mana hawezi kufikiria vizuri.
 
This is wrong.ninafanya kazi shule,kuna vitu vinatakiwa kuwa confidential.inatakiwa walimu,wajue medical history za wanafunzi na sio kwa kuruhusu wazazi wao waweke lebo,zitawekwa lebo ngapi?unajua mambo ya shule,kuna kutaniwa,jee mwanafunzi atajisikiaje?hao walimu nao ni wavivu wa kutambua huyu ana tatizo gani la kiafya.basi na wao wajiweke hizo lebo.huku ninakofanya kazi,kuna kitabu cha wanafunzi wenye chronic illness,na inakuwa siri yako,ila inasaidia pale mwanafunzi anapokuwa na tatizo,ujue vya kumsaidia
 

Huko unakofanya kazi kuna ratio gani ya walimu kwa wanafunzi?
 
pumbafu kabisa, kabla ya kuwawekea lebo kwanza wakapime wao wenyewe wajue afya zao, shenzitype, kwani magonjwa yanayouwa ni ukimwi tu, halafu huyo mwalimu anaesema ni maamuzi ya wazazi nae pia ni kilaza kama nainihii wetu huyu, yaani sasa alienda shule kusoma ili iweje kama yeye anatekeleza matakwa ya wazazi, ameidhalilisha taaluma yetu ya uwalimu na lazimi nimchukulie hatua, ujue ni li-voda fasta hili, walimu wa awamu ya nne. pumbafu kabisa
 
Samahani ila unaweza ukaskia mtu akisema " hao walipoata ukimwi ni kiherehere chao wenyewe" ....kweli kuna watu wana mtindio wa ubongo wa kijutakia yaani huyu mwalimu ana akili kweli??
 
Dah! Sio mpango mzuri hata kidogo. Wachukuliwe hatua hao.
 
Huko unakofanya kazi kuna ratio gani ya walimu kwa wanafunzi?
siwezi ku compare shule hizo mbili.utaratibu wao ni mwingi ni tofauti na nilivyosoma mimi,ila kuna mabo mengine walimu wanafaa wawe na uelewa,kwani mwanafunzi ni sawa sawa na mlezi wako.
 
Samahani ila unaweza ukaskia mtu akisema " hao walipoata ukimwi ni kiherehere chao wenyewe" ....kweli kuna watu wana mtindio wa ubongo wa kijutakia yaani huyu mwalimu ana akili kweli??


aaahahahahahahahaaaaaah!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Unanikumbusha kuna mjamaa alisema hadharani baada ya kuishiwa Point ya hoja kuwa " WANAFUNZI WA KIKE WANAOPATA MIMBA NI KIHEREHERE CHAO"

DUUUUUUUUUUUUUUUU!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

kweli anaweza kuibuka mkuu akasema hadharani kuwa tuliopata UKIMWI ni kiherehere chetu!!! AAAAAHAHAHAHAHAHAHAHAAAAAAA!!!!!



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 

Si kila anaetwa MWALIMU ana TAALUMA YA UALIMU! Nashauri huyo mwalimu achunguzwe kuanzia AKILI HADI CV ZAKE.HANA HAIBA YA UALIMU.He/She has LOW THINKING CAPACITY
 
Me cjaipenda sana wakuu! ubaguz huu wazaz nyie vp!
 

Naelewa yote hayo, ndiyo maana ukifuatilia thread utaona namulika dichotomy ya kukubali tunayoletewa na western world au kuamua wenyewe?

Ndiyo maana hiyo "child labor" nime i qualify kwamba "kuna wengine watasema" kwa kujua kwamba katika context ya kitanzania mtoto kufundishwa kazi ni wajibu kama ulivyosema hapo juu.

Katika context ya kiTanzania, ugonjwa si kitu cha kuonewa aibu (UKIMWI/HIV ni ugonjwa mpya na kama alivyosema Mwinyi "umekaa pabaya" kwa hiyo una anomalous stigma), na privacy hatuijuhi kama wanavyoijua hao watu wa West.

Kwa hiyo kuna a separate line of thinking inayokuja hapa, kwamba, jamii ya Kitanzania inawezekana in a dilapidated way, in it's own context,imeendelea sana kupita hao watu wa magharibi kiasi cha ku prioritize kitu muhimu kabisa, afya na maisha ya mtoto, kuliko kitu ambacho katika jamii ya kitanzania hakina umuhimu mkubwa, privacy.

Inawezekana hawa watoto wanajulikana tayari kwamba ni HIV positive kijiji kizima kwa sababu kila mtu anajua walizaliwa wakati wazazi wao wana HIV. Kwa mtoto kama huyu, kitu muhimu ni nini, privacy au protection?

Ni swali gumu kwa sababu jamii zetu ziko nyuma kiuchumi kiasi kwamba tunaona hata tamaduni zetu ziko nyuma, na inawezekana nyingine zipo nyuma.

Lakini je, hili linamaanisha Waswede Wamarekani na Waingereza ambao tamaduni zao zina expectations zaprivacy level iliyo unrealistic kwetu wana haki ya kututaka tuwe na privacy kama yao?

Wwana haki ya kusema privacy expectations za tamaduni zao ndio ziwe standards za dunia?

Wengine wanaweza kusema tukitaka kufuatisha sana standards za west tutafikia point mtu ana mgonjwa mahututi, ambulance limekuja kumchukua kumpeleka hospitali, tunakataa kumpandisha mgonjwa mahututi kwenye ambulance kwa sababu halina reflective sticker au halijafanyiwa inspection katika miezi 6 iliyopita kama kinavyosema kitabu cha code za ambulance maintenance cha California, huku sie tuko Malampaka.

Hii epidemic inaweza ku warrant exceptions kwa watu wanaoamua kusema mie privacy kwangu si muhimu kama kupata nafasi ya kutofagia na kuchokoza magonjwa zaidi?

Hii aproach ya kibongobongo, hata kama ni serendipitously, inaweza kuondoa stigma juu ya UKIMWI/HIV kwa kuonyesha kwamba UKIMWI ni ugonjwa kama asthma tu? Na kama tunaweza kuwapa exception watoto wenye asthma, tunaweza kuwapa wenye UKIMWI pia (labda tuwavishe wagonjwa/ waathirika wote label, tuna solve tatizo la kuwanyanyapaa wenye UKIMWI tu)

Lakini hata ukiwawekea label wagonjwa wote, bado watu wenye values za kimagharibi watasema mnanyanyasa wagonjwa fundamentally, despite the practical reasons.

Hivi bongo kama jamii tuna value privacy kihivyo? Mtu mwingine ukimsalimia na kumjulia hali rhetorically tu ataanza kukuelezea mgongo unavyomuuma na kukupa his entire medical history, mtu kama huyu ukimwambia unarisk mtoto apate magonjwa kwa sababu ya privacy atakuelewa?
 
Wagojwa wa UKIMWI jamanii ni binadamu wenzetu tusiwatenge tutasababisha mengine kama kijinyonga kwa baadhi ya wenye label.
 
Wagojwa wa UKIMWI jamanii ni binadamu wenzetu tusiwatenge tutasababisha mengine kama kijinyonga kwa baadhi ya wenye label.

Kwanza hapa kuna suala la uathirika na virusi na ugonjwa, kuathirika si lazima uwe mgonjwa.

Pili Mwalimu kasema kwamba hawatengwi, wazazi wa watoto hawa wanaomba watoto watambulike kama wagonjwa/ waathirika wengine ili wasipewe kazi zitakazoathiri afya zao.

Kuna wengine wanaweza kusema kwamba kuwakatalia kujulikana kama waathirika ndio kunaweza kuwatenga zaidi. Maana wameathirika halafu wananyimwa nafasi ya kujulikana kama waathirika ili jamii iwafanyie kama waathirika wanavyotakiwa kufanyiwa.

Sitetei hii habari, lakini pia sitaki kukataa labelling kwa sababu wazungu wamesema hivyo tu. Najaribu kuangalia practical situation katika jamii yetu.

Mzazi kaja kasema mwanae ana virusi anataka watu wote wajue ili anapokula ashikirimu wasimuombe, kwa sababu wanaweza kumuomba na yeye akajisahau akawapa, katika kuwapa ashikirimu ikawa na mate, wengine wakaambukizwa.

Au anasema mtoto akifagia anaweza ku trigger viral infections ambazo kwa mtu mwenye VVU zinaweza kuwa deadly. Mzazi hajali lofty privacy ideals from a distant Ivy league tower, anajali afya ya mtoto on the ground. Anasema yeye hataki kila mtoto mwenye VVU awekewe label, yeye anataka mwanawe tu.

Tutamwambiaje mzazi huyu?
 

Hii imenikumbusha freshman orientation yangu.

Director wa international programs alituambia kabisa huku Unyamwezini mtu akikuulizia hali yako haina maana uanze kumuwambia yote yanayokusumbua, sijui mwanao kaamka na homa, mara baba mkwe sijui nini....hapana...it's not like that.

Ukiulizwa 'how is it going'?....ukijibu 'not too bad, yourself'?, imetosha and you keep it moving.

Cultural differences!!!
 
Bado mi naona waathirika wawe fair, kunyanyapaliwa kutaisha itakapozoeleka.Jamaa hawa wanaambukiza mbaya.Mi kwanza hata dawa za kuongeza masiku sioni dili yake.Nadhani wangeleta za kufupisha zaidi ingekuwa deal, kwani kwa muda mfupi wangeisha. Watu wanaambukizwa saana. Mbona hamsemi kitu, watu wenye v**udu vidogo wanavyonyanyapaliwa, hamjasema wenye sura fulani wanavyokosa wenzi, kuna wengi wananyanyapaliwa, hamkasema jamaa wanavyosema Jamaa wa kaskazini wasahau kuongoza nchi, mnasema wakati mnaowalinda wanaua wengine. Basi hakuna haja ya kampeni za ukimwi wakati mnawaficha wagonjwa tena wenye hisia. Juzi tuu kuna sis mmoja mumewe kapita long time, katumia dawa na kuhudhuria makanisa ya fasta akadai kapona kwa watu wanaomjua, na kwa wasiomjua hakuwa akiwaambia.kaolewa na watu wawili,tofauti, wa mwisho alikuwa king`ang`anizi hadi wife kafariki.Hayo matukio yapo sana huku uswazi.watu watazoea kuwaona na kuwakubali km wazungu walivyojifunza wakubali weusi ktk mpira na maisha ya kawaida.
 
Schoolchildren in Tanzania are being made to wear a red ribbon on their uniforms to show that they are HIV positive.

Photo: Reuters




By Aislinn Laing, Johannesburg

8:29AM GMT 18 Mar 2012



The headmaster of one of the schools, in the northwest district of Kibaha, said the unusual move was done at the parents' request to ensure ill pupils were not made to undertake tasks that might affect their health.

But campaigners say that revealing another person's HIV status is illegal under Tanzanian law and punishable by up to three years imprisonment.

Around five per cent of the population – some 1.4m people – have HIV in Tanzania. While the rate is no higher than in most East African countries, the infection rate for women is higher than for men and it is often transmitted to children.

Mohammed Lukema, head of Kibaha Primary School, said parents had asked for their children to wear red ribbons if they were infected so they could be excused from strenuous duties at the rural school, such as sweeping the compound and fetching and carrying water.

He insisted that they were not judged as a result. "Our school has pupils who are suffering from various diseases," he told the BBC.

"The school and the society at large have decided to label pupils' uniforms."
When contacted by The Daily Telegraph for comment after the row broke, he declined to comment, saying it was a matter for the district's Director of Education.

Msafiri Thomas was leading an HIV/Aids community awareness scheme in the area when the practice of putting ribbon on pupils emerged in a focus group.

"It was raised by parents, teachers and school leavers and seems to have been happening for some time," he told The Daily Telegraph. "The general feeling was that it wasn't a good thing because life is hard enough for students living with HIV without making life harder for them at school.


"Students wearing these ribbons are sometimes shunned by other pupils who don't want to share or be near them because they fear they will be infected. There must be another well to help these children." Rebecca Mshumbusi, chairperson of the Kibaha Association of People Living with HIV/Aids, said that forcing children to reveal their status was not only unethical but illegal.


In 2008, a law was passed which makes it illegal to discriminate against someone with HIV or Aids, or to reveal another's status.
 
This time the Government went too far; Is this really necessary? to post# Young Kids? do U think it is discrimination?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…