Wanahabari hawakubaliani na tozo japo wanaandaa vipindi vinavyotetea tozo

Wanahabari hawakubaliani na tozo japo wanaandaa vipindi vinavyotetea tozo

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Mmoja wa wadau katika warsha ya uandaaji wa maudhui ya ndani iliyoandaliwa na TCRA alionesha masikito yake kuwa analazimika kuandaa vipindi vinavyotetea tozo japo yeye binafsi hakubaliani na tozo za kwenye miamala ya fedha kwenye simu na benki.

Mdau huyo amesema " Nazungumza uongo mbele ya 'Audience' yangu, nafanya kipindi kuhusu tozo, tozo yenyewe mimi inaniumiza maana mimi mshahara wangu unakatwa na ukienda benki unakatwa tena halafu nalazimika kusema tozo ni nzuri" Alisema mdau huyo kwenye warsha.

Serikali ilianzisha kukusanya kiasi cha pesa kwenye miamala yoyote ya kutuma na kutoa fedha kwa njia simu na benki ambayo imeibua mjadala mkubwa kwa wananchi ambao hawajaridhishwa na uwepo wa tozo huku wengi wakitaka tozo hizo kuondolewa na Serikali.
 
Mmoja wa wadau katika warsha ya uandaaji wa maudhui ya ndani iliyoandaliwa na TCRA alionesha masikito yake kuwa analazimika kuandaa vipindi vinavyotetea tozo japo yeye binafsi hakubaliani na tozo za kwenye miamala ya fedha kwenye simu na benki.

Mdau huyo amesema " Nazungumza uongo mbele ya 'Audience' yangu, nafanya kipindi kuhusu tozo, tozo yenyewe mimi inaniumiza maana mimi mshahara wangu unakatwa na ukienda benki unakatwa tena halafu nalazimika kusema tozo ni nzuri" Alisema mdau huyo kwenye warsha.

Serikali ilianzisha kukusanya kiasi cha pesa kwenye miamala yoyote ya kutuma na kutoa fedha kwa njia simu na benki ambayo imeibua mjadala mkubwa kwa wananchi ambao hawajaridhishwa na uwepo wa tozo huku wengi wakitaka tozo hizo kuondolewa na Serikali.
Ni kama waliomsifia mfalme amevaa suti amependeza sana wakati kengele ipo nje
 
Kama taifa tumekosa ushirikiano kati yetu ndio maana CCM wanaendelea kututawala kwa urahisi.

Ni rahisi sana miongoni mwetu, kwa yule atakayepewa "bahasha" akawasahau wenzake aliokuwa nao kwenye mapambano.

Hili halipo kwa waandishi pekee, lipo hata kwa wanasiasa, tumeona vile wakihamia upande wa pili wanavyoanza kuupamba, mpaka pale wakiondolewa ulaji ndio akili zinawarudi.

Wasomi pia, wengi huacha kufuata taaluma zao wanapopata ulaji kwenye siasa, mpaka pale wanapotoswa siasani, ndipo hurudi kujikumbusha yaliyoandikwa kwenye vitabu vyao.

Hata kwa wapiga kura, wapo wale wanaolalamika miaka mitano hali ngumu, lakini ukifika wakati wa kampeni wakahongwa t shirt na kanga za kijani, nao wanahama kambi.

Hatujielewi.
 
Kama taifa tumekosa ushirikiano kati yetu ndio maana CCM wanaendelea kututawala kwa urahisi.
Its a fact CCM itatawala milele kwasababu Watanzania wanaipenda, wanaikubali na wataendelea kuipigia kura na kuipatia ushindi wa kishindo.
Ni rahisi sana miongoni mwetu, kwa yule atakayepewa "bahasha" akawasahau wenzake aliokuwa nao kwenye mapambano.
Duh...!.
Hili halipo kwa waandishi pekee, lipo hata kwa wanasiasa, tumeona vile wakihamia upande wa pili wanavyoanza kuupamba, mpaka pale wakiondolewa ulaji ndio akili zinawarudi.
Ni kweli!.
Wasomi pia, wengi huacha kufuata taaluma zao wanapopata ulaji kwenye siasa, mpaka pale wanapotoswa siasani, ndipo hurudi kujikumbusha yaliyoandikwa kwenye vitabu vyao.
Ni kweli, wakiwemo ma profesa wetu!.
Hata kwa wapiga kura, wapo wale wanaolalamika miaka mitano hali ngumu, lakini ukifika wakati wa kampeni wakahongwa t shirt na kanga za kijani, nao wanahama kambi.
Ni kweli!.
Hatujielewi.
Sii wote hawajielewi, kuna wengine wanajielewa kabisa ila wamejikuta ni wazalendo tuu zaidi kwa taifa lao kwasababu there is no choice to choose from any other options, hivyo they have to choose the one and only devil they know!. CCM ni ... likujualo!.
Watanzania tutaendelea kulichagua hili ... tulijualo kwa miaka mingi ijayo and probably milele kama China na Korea Kaskazini!.
P
 
Back
Top Bottom