pwilo
JF-Expert Member
- May 27, 2015
- 10,913
- 13,876
1. Ali kiba
Moja kati ya wasanii ambao wamejaaliwa kipaji na sauti nzuri ila jamaa anajiamini kupita kiasi na ili akubali ushauri au idea ya kuendeleza kipaji chake nguvu kubwa sana inahitajika. Kilichotokea kati yake na Davido pamoja na MI wa aje ni ushahidi wa ninachokiongea na hata aliye mshauri idea ya team samatta na team kiba alifanya kazi kubwa sana mpaka akakubali wazo hilo.
2. Ruby
Mwanadada mwenye sauti murua ya kumtoa nyoka pangoni hakusita kuwagomea ma boss wake kwa kudai pesa aliyokuwa amepewa ni kidogo hivyo hatashiriki kwenye tamasha lao na kuingia katika mgogoro mkubwa ulio isha siku za karibuni.
3.Barak da prince
Moja kati ya wasanii ambao walikuja vizuri sana kipindi cha mwanzoni na kufanya vizuri na nyimbo yake ya SIACHANI NAWE na baada ya hapo ni ngoma Kali mfululizo ila jamaa ni jeuri sana kitu kinacho fanya baadhi ya media kumpotezea.
4.Timbulo
Kinacho muangusha huyu jamaa kwanza sio mtu wa kujichanganya sana anaishi maisha tofauti na wasanii wenzake baada ya kugombana na media ambayo bila wao kimziki huwezi kutoboa kutokana na maslahi yake na wakaamua kumpotezea.
5. Young killer (msodoki)
Huyu jamaa tatizo lake anajisifia sana
Na kuwadharau baadhi ya wasanii wenzake wakiwemo wakongwe (weusi) na kudai kuwa kuna baadhi Yao wana bebwa na media ila hawana uwezo wowote kulinganisha na yeye kama janjaro na young Dee hivyo kufanya baadhi ya media na wasanii wenzake kumpotezea.
Wapo wengi ila hao ni wachache tu kati Yao kama wakiacha hizo Tabia walizo nazo na kuweka juhudi kwenye mziki wao wangefika mbali sana ila ndo hivyo kipato huleta majivuno.
Moja kati ya wasanii ambao wamejaaliwa kipaji na sauti nzuri ila jamaa anajiamini kupita kiasi na ili akubali ushauri au idea ya kuendeleza kipaji chake nguvu kubwa sana inahitajika. Kilichotokea kati yake na Davido pamoja na MI wa aje ni ushahidi wa ninachokiongea na hata aliye mshauri idea ya team samatta na team kiba alifanya kazi kubwa sana mpaka akakubali wazo hilo.
2. Ruby
Mwanadada mwenye sauti murua ya kumtoa nyoka pangoni hakusita kuwagomea ma boss wake kwa kudai pesa aliyokuwa amepewa ni kidogo hivyo hatashiriki kwenye tamasha lao na kuingia katika mgogoro mkubwa ulio isha siku za karibuni.
3.Barak da prince
Moja kati ya wasanii ambao walikuja vizuri sana kipindi cha mwanzoni na kufanya vizuri na nyimbo yake ya SIACHANI NAWE na baada ya hapo ni ngoma Kali mfululizo ila jamaa ni jeuri sana kitu kinacho fanya baadhi ya media kumpotezea.
4.Timbulo
Kinacho muangusha huyu jamaa kwanza sio mtu wa kujichanganya sana anaishi maisha tofauti na wasanii wenzake baada ya kugombana na media ambayo bila wao kimziki huwezi kutoboa kutokana na maslahi yake na wakaamua kumpotezea.
5. Young killer (msodoki)
Huyu jamaa tatizo lake anajisifia sana
Na kuwadharau baadhi ya wasanii wenzake wakiwemo wakongwe (weusi) na kudai kuwa kuna baadhi Yao wana bebwa na media ila hawana uwezo wowote kulinganisha na yeye kama janjaro na young Dee hivyo kufanya baadhi ya media na wasanii wenzake kumpotezea.
Wapo wengi ila hao ni wachache tu kati Yao kama wakiacha hizo Tabia walizo nazo na kuweka juhudi kwenye mziki wao wangefika mbali sana ila ndo hivyo kipato huleta majivuno.