Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 8,870
- 14,258
Mmoja wa waliothirika na hama hama ndani ya Gazi ni mzee Yasser Alsharafa ambaye alipohojiwa kuhusiana na matamshi ya hivi karibu kutoka kwa raisi wa Marekani, amesema hatishiki na maneno hayo kwani kwa sasa hana chochote cha kuhofia kukipoteza.
Kwa sasa mzee huyo anashughulika na kuuza pipi kwenye rafu alizozisimamisha barabarani. Kabla ya vita kuanza anasema alikuwa na duka kubwa la nguo na kumiliki jengo la Ghorofa pamoja na gari. Aliporudi hivi karibuni kutoka kusini ya Gaza alikokimbilia amekuta jengo lake hilo limebaki ni kifusi tu na kila kitu alichomiliki kimepotea.
Mawazo kama hayo yametolewa na wananchi kadhaa waliohojiwa kuhusiana na kitisho cha Donald Trump pale aliposema wananchi wanaowashikilia mateka wawatoe mara moja kinyume cha hivyo wote wajihesabu wameshakufa.
Kwa sasa mzee huyo anashughulika na kuuza pipi kwenye rafu alizozisimamisha barabarani. Kabla ya vita kuanza anasema alikuwa na duka kubwa la nguo na kumiliki jengo la Ghorofa pamoja na gari. Aliporudi hivi karibuni kutoka kusini ya Gaza alikokimbilia amekuta jengo lake hilo limebaki ni kifusi tu na kila kitu alichomiliki kimepotea.
Mawazo kama hayo yametolewa na wananchi kadhaa waliohojiwa kuhusiana na kitisho cha Donald Trump pale aliposema wananchi wanaowashikilia mateka wawatoe mara moja kinyume cha hivyo wote wajihesabu wameshakufa.