Kinoamiguu
JF-Expert Member
- Nov 29, 2018
- 11,936
- 15,196
Wandugu,
Hali ni mbaya Mikoa ya kusini, Pwani, Lindi na Mtwara. Zao la KOROSHO siyo mkombozi wao tena. Ikumbukwe hapo mwishoni mwa mwaka 2017 serikali ilitangaza ununuzi wa zao la KOROSHO kwa kisingizio cha kukomesha unyonyaji kwa WAKULIMA wa zao hilo.
Kwa mujibu wa wakazi wa huko tangu wakati huo hali haijatengemaa mpaka sasa ni vilio.
Huu ni wakati wa kuandaa mashamba. Kabla ya uporaji ule wananchi walikuwa wana namna zao za kukopeshana. Mfano unapewa salpher utakuja kurudisha KOROSHO ilikuwa kawaida. Mabenk nayo hayakuwa nyuma, unakopeshwa ukija kulipwa pesa unapita bank wanakata cha kwao maisha yanaenda. Baada ya serikali ya bwana mkubwa kuingilia sasa kila kitu kimekwama. Wakopeshaji hawatoi mikopo tena kwani wanaogopa kuambiwa waoneshe mashamba tena na wanaishi wenye magwanda.
Zao la KOROSHO ambalo lilikuwa mkombozi Mikoa ya kusini sasa limegeuka shubir halina soko tena. Wapo waliouza kg 50 lakini analipwa kilo mbili mbili. Wakamdai nani? Siyo vyama vya ushirikiano AMCOS wala nini vyenye lakusema juu ya malipo yao! Wasemeje nae mchumi mkuu wa taifa ameshaamua.
Siyo KOROSHO tu. Kabla ya 2015 kusini kulikuwa na mazao matatu. Mbaazi kwisha kazi, kazi, korosho na ufuta yote kwisha kazi.
KUONESHA KWAMBA AMEHARIBU NA KUKERA WATU 2021 HAJAENDA KUPIGA KAMPENI HUKO KUSINI.
Je. Wakusini waendelee kuimba hapa kazi tu? Wamevuna walichopanda? Ni kivuli na majivuno ya mtawala?
Hali ni mbaya Mikoa ya kusini, Pwani, Lindi na Mtwara. Zao la KOROSHO siyo mkombozi wao tena. Ikumbukwe hapo mwishoni mwa mwaka 2017 serikali ilitangaza ununuzi wa zao la KOROSHO kwa kisingizio cha kukomesha unyonyaji kwa WAKULIMA wa zao hilo.
Kwa mujibu wa wakazi wa huko tangu wakati huo hali haijatengemaa mpaka sasa ni vilio.
Huu ni wakati wa kuandaa mashamba. Kabla ya uporaji ule wananchi walikuwa wana namna zao za kukopeshana. Mfano unapewa salpher utakuja kurudisha KOROSHO ilikuwa kawaida. Mabenk nayo hayakuwa nyuma, unakopeshwa ukija kulipwa pesa unapita bank wanakata cha kwao maisha yanaenda. Baada ya serikali ya bwana mkubwa kuingilia sasa kila kitu kimekwama. Wakopeshaji hawatoi mikopo tena kwani wanaogopa kuambiwa waoneshe mashamba tena na wanaishi wenye magwanda.
Zao la KOROSHO ambalo lilikuwa mkombozi Mikoa ya kusini sasa limegeuka shubir halina soko tena. Wapo waliouza kg 50 lakini analipwa kilo mbili mbili. Wakamdai nani? Siyo vyama vya ushirikiano AMCOS wala nini vyenye lakusema juu ya malipo yao! Wasemeje nae mchumi mkuu wa taifa ameshaamua.
Siyo KOROSHO tu. Kabla ya 2015 kusini kulikuwa na mazao matatu. Mbaazi kwisha kazi, kazi, korosho na ufuta yote kwisha kazi.
KUONESHA KWAMBA AMEHARIBU NA KUKERA WATU 2021 HAJAENDA KUPIGA KAMPENI HUKO KUSINI.
Je. Wakusini waendelee kuimba hapa kazi tu? Wamevuna walichopanda? Ni kivuli na majivuno ya mtawala?