Pre GE2025 Wananchi na Viongozi wa Upinzani kukaa kimya kunatoa mwanya kwa watekaji kuendelea kupoteza watu nchini

Pre GE2025 Wananchi na Viongozi wa Upinzani kukaa kimya kunatoa mwanya kwa watekaji kuendelea kupoteza watu nchini

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Hawa watekaji walianza kuwateka wanaharakati. Kwa kawaida wanaharakati huwa hawana wafuasi rasmi. Watekaji walifanya hivyo kupima mwamko na nguvu ya wananchi pale inapotokea mmoja wao anafanyiwa uharamia. Wakataka kuona, Watamzania watafanya nini dhidi yao.

Matokeo: Watanzania, kama nyumbu wanapomwona mwenzao amekamatwa na simba, wao hupumua wakiamini kuwa sasa wapo salama, bila kujua kuwa njaa ya simba haitamalizwa na kumla yule nyumbu mmoja, kesho itabidi akamatwe mwingine, na kadiri wanavyozidi kukamatwa wenzako, zamu yako inazidi kukaribia.

2) Watekaji walipojiridhisha kuwa kumbe Watanzania, kama walivyo nyumbu, hawaumizwi na madhira ya mwananchi mwenzao mmoja, wakaamua waende kwa waliokusudia, huku wakijua kuwa wananchi hawatafanya lolote.

3) Wakawateka viongozi wa ngazi za chini wa CHADEMA. Watekaji wanajua kuwa CHADEMA ina wanachama, wafuasi na wapenzi. Walifanya hivyo ili kuona, je hao wanachama, wapenzi na wafuasi wa chama watafanya nini?

Matokeo: Nao wakakaa kimya, wakafanya kama nyumbu wafanyavyo. Hapo watekaji wakajipa uhakika kuwa wanaweza kuendelea kuteka na kuwaua viongozi wa ngazi za chini wa CHADEMA, bila bugdha yoyote. Lakini wakawa hawana uhakika wakiwagusa viongozi wa kitaifa.

3) Jaribio lao la kwanza wamemteka na kisha kumwua msaidizi wa katibu mkuu wa CHADEMA Taifa. Wanasubiria kuona kama kutakuwa na reaction kutoka kwa wanachama, wapenzi na wafuasi wa CHADEMA, halikadhalika kutoka kwa wananchi. Hili likipita kimya, watakuwa na uhakika wa kumteka au hata kumwua Mbowe, Lisu, Mnyika au kiongozi mwingine yeyote bila ya kuwa na hofu yoyote.

NB: Lakini wanachama wa vyama vingine, viongozi wa vyama vingine vya upinzani, na hata ndani ya CCM, kwa ujinga nao wanafanya kama nyumbu. Wakiamini kuwa wanaotafutwa ni CHADEMA pekee, wakati kiuhalisia tukilikubali hili, huu ndio utageuka na kuwa utamaduni mpya wa utawala nchini Tanzania. Hata ukiwa ndani ya CCM, ukakosoa kama alivyofanya Mpina, ujue utekaji na kisha mauaji vinakuhusu. Hata ukiwa kwenye Serikali ya umoja Zanzibar, ukakosoa chochote, ujue utekaji na mauaji vinakuhusu. Hata ukiwa ndani ya Serikali, ukaonekana ni tishio kwa watu fulani, ujue utekaji na mauaji vinakuhus.

Pia soma: Ally Mohamed Kibao auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

WITO:
Kama wewe mwenyewe hutaki kutekwa, hutaki ndugu na mwanafamilia wako kutekwa na kuuawa, wakati wa kuzuia ni huu wa sasa ambao bado unapumua. Ukishatekwa, umeuawa, huna nafasi ya kuuzuia utekaji na mauaji holela yanayoendelea nchini mwetu sasa, na yanayozidi kuota mizizi.

Viongozi wa dini, walio wengi wapo kimya dhidi ya uovu huo, yawezekana na wao wamekuwa kama nyumbu, wakiamini huo uharamia utaishia kwa CHADEMA. Lakini wajue kuwa utaratibu huu unaoendelea kuota mizizi, watekaji hawataona shida kumteka na hata kumwua kiongozi yeyote wa dini atakayejaribu kukosoa chochote.

Wananchi tujue kuwa kila kitu huanza kwa udhaifu, kisipobugudhiwa au kukataliwa, kadiri siku zinavyoenda, kitazidi kukua na kujiimarisha. Utaratibu huu mpya wa kuwateka na wakati mwingine kuwaua wakosoaji, ulianza kidogo kidogo, pengine utasikia tukio 1 kwa mwaka, lakini siku ziendavyo, matukio yanazidi kuongezeka, hii ni kudhihirisha kuwa watekaji na mfumo wa utekaji na mauaji, vinazidi kujijenga na kujiimarisha. Siku za huko nyuma, wakosoaji walikuwa wanakamatwa na kufunguliwa kesi za kubambikizwa. Sasa wakosoaji wanatekwa, kisha kuuawa mafichoni. Itakuja wakati, wakosoaji watakuwa wanauawa mbele ya macho ya wananchi wote, na sisi, kama nyumbu, tutabakia tunatizama kusubiria siku ya kwetu.

Tunamwomba Mungu utusaidie Watanzania, tuache unafiki, tuuheshimu na kuulinda uhai wetu na wa wenzetu kwa gharama yoyote ipasayo huku Mkono wako wenye nguvu ukitupatia ujasiri na ushidi dhidi ya uovu na waovu.
 
Liwalo na liwe ifike wakati sasa tusiruhusu huu ujinga kuendelea, tumeona watu wanatekwa na kumalizwa

Halafu mtu unakuja kushushwa unakubali, potelea pote usikubali na kama kumalizwa hakikisha unamalizwa hapo hapo

Ndio maana yule bosi wa Tarime aliwatandika risasi, hawa ukiwazoeza wanakuzoea


Ipo siku mmoja atasimama na kuonesha mfano kuwa mna haki ya kukamata na na kuna haki ya kukamatwa lakini kwa kufuata utaratibu maalum na sio kiholela holela tu, kisha mtu unakutwa umetupwa mahali
 
Kwa mtazamo wa kiusalama.. hili jambo miaka ya mbeleni litaleta machafuko makubwa kwa sababu ya kisasi
Yap hao wanaoguswa direct na haya wanakusanya nguvu, they will come back and this time hawatotumia siasa, itakuwa ni jino kwa jino ndipo machafuko yatakapozuka
 
Hawa watekaji walianza kuwateka wanaharakati. Kwa kawaida wanaharakati huwa hawana wafuasi rasmi. Watekaji walifanya hivyo kupima mwamko na nguvu ya wananchi pale inapotokea mmoja wao anafanyiwa uharamia. Wakataka kuona, Watamzania watafanya nini dhidi yao.

Matokeo: Watanzania, kama nyumbu wanapomwona mwenzao amekamatwa na simba, wao hupumua wakiamini kuwa sasa wapo salama, bila kujua kuwa njaa ya simba haitamalizwa na kumla yule nyumbu mmoja, kesho itabidi akamatwe mwingine, na kadiri wanavyozidi kukamatwa wenzako, zamu yako inazidi kukaribia.

2) Watekaji walipojiridhisha kuwa kumbe Watanzania, kama walivyo nyumbu, hawaumizwi na madhira ya mwananchi mwenzao mmoja, wakaamua waende kwa waliokusudia, huku wakijua kuwa wananchi hawatafanya lolote.
3) Wakawateka viongozi wa ngazi za chini wa CHADEMA. Watekaji wanajua kuwa CHADEMA ina wanachama, wafuasi na wapenzi. Walifanya hivyo ili kuona, je hao wanachama, wapenzi na wafuasi wa chama watafanya nini?
Matokeo: Nao wakakaa kimya, wakafanya kama nyumbu wafanyavyo. Hapo watekaji wakajipa uhakika kuwa wanaweza kuendelea kuteka na kuwaua viongozi wa ngazi za chini wa CHADEMA, bila bugdha yoyote. Lakini wakawa hawana uhakika wakiwagusa viongozi wa kitaifa.

3) Jaribio lao la kwanza wamemteka na kisha kumwua msaidizi wa katibu mkuu wa CHADEMA Taifa. Wanasubiria kuona kama kutakuwa na reaction kutoka kwa wanachama, wapenzi na wafuasi wa CHADEMA, halikadhalika kutoka kwa wananchi. Hili likipita kimya, watakuwa na uhakika wa kumteka au hata kumwua Mbowe, Lisu, Mnyika au kiongozi mwingine yeyote bila ya kuwa na hofu yoyote.

NB: Lakini wanachama wa vyama vingine, viongozi wa vyama vingine vya upinzani, na hata ndani ya CCM, kwa ujinga nao wanafanya kama nyumbu. Wakiamini kuwa wanaotafutwa ni CHADEMA pekee, wakati kiuhalisia tukilikubali hili, huu ndio utageuka na kuwa utamaduni mpya wa utawala nchini Tanzania. Hata ukiwa ndani ya CCM, ukakosoa kama alivyofanya Mpina, ujue utekaji na kisha mauaji vinakuhusu. Hata ukiwa kwenye Serikali ya umoja Zanzibar, ukakosoa chochote, ujue utekaji na mauaji vinakuhusu. Hata ukiwa ndani ya Serikali, ukaonekana ni tishio kwa watu fulani, ujue utekaji na mauaji vinakuhus.

WITO:
Kama wewe mwenyewe hutaki kutekwa, hutaki ndugu na mwanafamilia wako kutekwa na kuuawa, wakati wa kuzuia ni huu wa sasa ambao bado unapumua. Ukishatekwa, umeuawa, huna nafasi ya kuuzuia utekaji na mauaji holela yanayoendelea nchini mwetu sasa, na yanayozidi kuota mizizi.

Viongozi wa dini, walio wengi wapo kimya dhidi ya uovu huo, yawezekana na wao wamekuwa kama nyumbu, wakiamini huo uharamia utaishia kwa CHADEMA. Lakini wajue kuwa utaratibu huu unaoendelea kuota mizizi, watekaji hawataona shida kumteka na hata kumwua kiongozi yeyote wa dini atakayejaribu kukosoa chochote.

Wananchi tujue kuwa kila kitu huanza kwa udhaifu, kisipobugudhiwa au kukataliwa, kadiri siku zinavyoenda, kitazidi kukua na kujiimarisha. Utaratibu huu mpya wa kuwateka na wakati mwingine kuwaua wakosoaji, ulianza kidogo kidogo, pengine utasikia tukio 1 kwa mwaka, lakini siku ziendavyo, matukio yanazidi kuongezeka, hii ni kudhihirisha kuwa watekaji na mfumo wa utekaji na mauaji, vinazidi kujijenga na kujiimarisha. Siku za huko nyuma, wakosoaji walikuwa wanakamatwa na kufunguliwa kesi za kubambikizwa. Sasa wakosoaji wanatekwa, kisha kuuawa mafichoni. Itakuja wakati, wakosoaji watakuwa wanauawa mbele ya macho ya wananchi wote, na sisi, kama nyumbu, tutabakia tunatizama kusubiria siku ya kwetu.

Tunamwomba Mungu utusaidie Watanzania, tuache unafiki, tuuheshimu na kuulinda uhai wetu na wa wenzetu kwa gharama yoyote ipasayo huku Mkono wako wenye nguvu ukitupatia ujasiri na ushidi dhidi ya uovu na waovu.
Haya mambo ni mageni tu huku Tanzania Bara ila wenzetu wa Zanzibar wameshayasahau haya madhila hata huku ifafika mahali yataisha.
 
Huyu mkizimkazi ametuletea utamaduni wa kutoka nchini kwake. Kule kwao kulikuwa na kundi la Mazombi ambalo lilikuwa likipita mitaani na kuwateka ama kuwaua wapinzani..

Shida yote hii inaletwa na tamaa ya Kizimkazi ya kutaka kuendelea kuwa rais 2025
 
Ifike wakati hao wanaowatuma na waanze kuwa walengwa huku mitaani.
Kama lingeweza kufanyika hilo, hakika huu ushetani ungekoma.

Kule Mwanza, wakati Masha akiwa waziri wa Mambo ya ndani, baada ya uchaguzi mkuu, ikajulikana wazi kuwa mgombea wa upinzani ameshinda lakini mkurugenzi, polisi na CCM, walikiwa wanashirikiana kuchakachua matokeo. Baadhi ya vijana walikwenda kuizunguka ofisi ya CCM (ikiwa na baadhi ya watendaji ndani) na nyumba ya Baba yake Masha (mzee Masha) akiwa ndani wakazimwagia peteol kuzunguka nyumba, wakamwambia mzee Masha kuwa ampigie simu mwanae kuwa wamtangaze kuwa ndiye mshindi ila yeye atakuwa kafara wa huo ushindi bandia. Kilichofuatia, ni mkurugenzi kutoka nje na kuwatangazia wananchi kuwa mgombea wa CHADEMA alikuwa ameshinda. Lakini kwa siku 3 alikuwa amegoma kutangaza matokeo akisubiria maelekezo ya Mwenyekitiwa CCM.

Kuna wakati ni muhimu kwenda na lugha ambayo hao maharamia nao wataielewa.
 
Huyu mkizimkazi ametuletea utamaduni wa kutoka nchini kwake. Kule kwao kulikuwa na kundi la Mazombi ambalo lilikuwa likipita mitaani na kuwateka ama kuwaua wapinzani..

Shida yote hii inaletwa na tamaa ya Kizimkazi ya kutaka kuendelea kuwa rais 2025
Halafu tunayo mapunguani humu yanayompigia debe, huku watanganyika wenzetu wanazidi kupoteza uhai wao.
 
HAlafu tu ayo mapunguani humu yanayompigia debe, huku watanganyika wenzetu wanazidi kupoteza uhai wao.
Wahuni wanafurahia. Wao wanaona ni sifa kwa kupewa kazi ya kuwaua ndugu zao kwa ujira mdogo.
 
Kama mwenye mamlaka anawafumbia macho mimi raia nitasema nini?
Kwani samia hana macho,haoni?
labda anawatuma?
 
Binafsi simkubali Samia kabisa ikimpendeza asigombee 2025.

Lakini kwenye huu utekaji nakataa kabisa kuna mkono wake au wa serikali.

In this instance siafiki huu uhuni wa ‘means justifies the end’.

CDM waache kuumiza wanachama wao, hawana huo ushawishi wa kushinda chaguzi.
 
Hawa watekaji walianza kuwateka wanaharakati. Kwa kawaida wanaharakati huwa hawana wafuasi rasmi. Watekaji walifanya hivyo kupima mwamko na nguvu ya wananchi pale inapotokea mmoja wao anafanyiwa uharamia. Wakataka kuona, Watamzania watafanya nini dhidi yao.

Matokeo: Watanzania, kama nyumbu wanapomwona mwenzao amekamatwa na simba, wao hupumua wakiamini kuwa sasa wapo salama, bila kujua kuwa njaa ya simba haitamalizwa na kumla yule nyumbu mmoja, kesho itabidi akamatwe mwingine, na kadiri wanavyozidi kukamatwa wenzako, zamu yako inazidi kukaribia.

2) Watekaji walipojiridhisha kuwa kumbe Watanzania, kama walivyo nyumbu, hawaumizwi na madhira ya mwananchi mwenzao mmoja, wakaamua waende kwa waliokusudia, huku wakijua kuwa wananchi hawatafanya lolote.

3) Wakawateka viongozi wa ngazi za chini wa CHADEMA. Watekaji wanajua kuwa CHADEMA ina wanachama, wafuasi na wapenzi. Walifanya hivyo ili kuona, je hao wanachama, wapenzi na wafuasi wa chama watafanya nini?

Matokeo: Nao wakakaa kimya, wakafanya kama nyumbu wafanyavyo. Hapo watekaji wakajipa uhakika kuwa wanaweza kuendelea kuteka na kuwaua viongozi wa ngazi za chini wa CHADEMA, bila bugdha yoyote. Lakini wakawa hawana uhakika wakiwagusa viongozi wa kitaifa.

3) Jaribio lao la kwanza wamemteka na kisha kumwua msaidizi wa katibu mkuu wa CHADEMA Taifa. Wanasubiria kuona kama kutakuwa na reaction kutoka kwa wanachama, wapenzi na wafuasi wa CHADEMA, halikadhalika kutoka kwa wananchi. Hili likipita kimya, watakuwa na uhakika wa kumteka au hata kumwua Mbowe, Lisu, Mnyika au kiongozi mwingine yeyote bila ya kuwa na hofu yoyote.

NB: Lakini wanachama wa vyama vingine, viongozi wa vyama vingine vya upinzani, na hata ndani ya CCM, kwa ujinga nao wanafanya kama nyumbu. Wakiamini kuwa wanaotafutwa ni CHADEMA pekee, wakati kiuhalisia tukilikubali hili, huu ndio utageuka na kuwa utamaduni mpya wa utawala nchini Tanzania. Hata ukiwa ndani ya CCM, ukakosoa kama alivyofanya Mpina, ujue utekaji na kisha mauaji vinakuhusu. Hata ukiwa kwenye Serikali ya umoja Zanzibar, ukakosoa chochote, ujue utekaji na mauaji vinakuhusu. Hata ukiwa ndani ya Serikali, ukaonekana ni tishio kwa watu fulani, ujue utekaji na mauaji vinakuhus.

Pia soma: Ally Mohamed Kibao auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

WITO:
Kama wewe mwenyewe hutaki kutekwa, hutaki ndugu na mwanafamilia wako kutekwa na kuuawa, wakati wa kuzuia ni huu wa sasa ambao bado unapumua. Ukishatekwa, umeuawa, huna nafasi ya kuuzuia utekaji na mauaji holela yanayoendelea nchini mwetu sasa, na yanayozidi kuota mizizi.

Viongozi wa dini, walio wengi wapo kimya dhidi ya uovu huo, yawezekana na wao wamekuwa kama nyumbu, wakiamini huo uharamia utaishia kwa CHADEMA. Lakini wajue kuwa utaratibu huu unaoendelea kuota mizizi, watekaji hawataona shida kumteka na hata kumwua kiongozi yeyote wa dini atakayejaribu kukosoa chochote.

Wananchi tujue kuwa kila kitu huanza kwa udhaifu, kisipobugudhiwa au kukataliwa, kadiri siku zinavyoenda, kitazidi kukua na kujiimarisha. Utaratibu huu mpya wa kuwateka na wakati mwingine kuwaua wakosoaji, ulianza kidogo kidogo, pengine utasikia tukio 1 kwa mwaka, lakini siku ziendavyo, matukio yanazidi kuongezeka, hii ni kudhihirisha kuwa watekaji na mfumo wa utekaji na mauaji, vinazidi kujijenga na kujiimarisha. Siku za huko nyuma, wakosoaji walikuwa wanakamatwa na kufunguliwa kesi za kubambikizwa. Sasa wakosoaji wanatekwa, kisha kuuawa mafichoni. Itakuja wakati, wakosoaji watakuwa wanauawa mbele ya macho ya wananchi wote, na sisi, kama nyumbu, tutabakia tunatizama kusubiria siku ya kwetu.

Tunamwomba Mungu utusaidie Watanzania, tuache unafiki, tuuheshimu na kuulinda uhai wetu na wa wenzetu kwa gharama yoyote ipasayo huku Mkono wako wenye nguvu ukitupatia ujasiri na ushidi dhidi ya uovu na waovu.
Ipo siku namba za waliotekwa ndugu zao, baba zao nk mioyo itachoka na maumivu, hapo ndio utakuwa mwanzo wa majuto. Tukumbuke ni damu ya mtu inathamani kuliko kuupata ulimwengu wote.
Binadamu akichoka hakuna kitu cha kumzuia.
 
Kama mwenye mamlaka anawafumbia macho mimi raia nitasema nini?
Kwani samia hana macho,haoni?
labda anawatuma?
Nakubaliana nawe. Maana wakati wote Rais Samia ameonekana wazi kabisa kusimama upande wa watekaji. Alidiriki kusema wazi kabisa kuwa eti hakuna utekaji. Sijui huu ambao sisi tunauona ni utekaji, yeye kwake ni kitu gani!!
 
Ipo siku namba za waliotekwa ndugu zao, baba zao nk mioyo itachoka na maumivu, hapo ndio utakuwa mwanzo wa majuto. Tukumbuke ni damu ya mtu inathamani kuliko kuupata ulimwengu wote.
Binadamu akichoka hakuna kitu cha kumzuia.
Amina, na iwe hivyo.
Mungu atujalie ujasiri, ili tusikubali mashetani yawe juu yetu. Mashetani, kwao ni jehanamu wala si miongoni mwa wanadamu wema.
 
Hawa watekaji walianza kuwateka wanaharakati. Kwa kawaida wanaharakati huwa hawana wafuasi rasmi. Watekaji walifanya hivyo kupima mwamko na nguvu ya wananchi pale inapotokea mmoja wao anafanyiwa uharamia. Wakataka kuona, Watamzania watafanya nini dhidi yao.

Matokeo: Watanzania, kama nyumbu wanapomwona mwenzao amekamatwa na simba, wao hupumua wakiamini kuwa sasa wapo salama, bila kujua kuwa njaa ya simba haitamalizwa na kumla yule nyumbu mmoja, kesho itabidi akamatwe mwingine, na kadiri wanavyozidi kukamatwa wenzako, zamu yako inazidi kukaribia.

2) Watekaji walipojiridhisha kuwa kumbe Watanzania, kama walivyo nyumbu, hawaumizwi na madhira ya mwananchi mwenzao mmoja, wakaamua waende kwa waliokusudia, huku wakijua kuwa wananchi hawatafanya lolote.

3) Wakawateka viongozi wa ngazi za chini wa CHADEMA. Watekaji wanajua kuwa CHADEMA ina wanachama, wafuasi na wapenzi. Walifanya hivyo ili kuona, je hao wanachama, wapenzi na wafuasi wa chama watafanya nini?

Matokeo: Nao wakakaa kimya, wakafanya kama nyumbu wafanyavyo. Hapo watekaji wakajipa uhakika kuwa wanaweza kuendelea kuteka na kuwaua viongozi wa ngazi za chini wa CHADEMA, bila bugdha yoyote. Lakini wakawa hawana uhakika wakiwagusa viongozi wa kitaifa.

3) Jaribio lao la kwanza wamemteka na kisha kumwua msaidizi wa katibu mkuu wa CHADEMA Taifa. Wanasubiria kuona kama kutakuwa na reaction kutoka kwa wanachama, wapenzi na wafuasi wa CHADEMA, halikadhalika kutoka kwa wananchi. Hili likipita kimya, watakuwa na uhakika wa kumteka au hata kumwua Mbowe, Lisu, Mnyika au kiongozi mwingine yeyote bila ya kuwa na hofu yoyote.

NB: Lakini wanachama wa vyama vingine, viongozi wa vyama vingine vya upinzani, na hata ndani ya CCM, kwa ujinga nao wanafanya kama nyumbu. Wakiamini kuwa wanaotafutwa ni CHADEMA pekee, wakati kiuhalisia tukilikubali hili, huu ndio utageuka na kuwa utamaduni mpya wa utawala nchini Tanzania. Hata ukiwa ndani ya CCM, ukakosoa kama alivyofanya Mpina, ujue utekaji na kisha mauaji vinakuhusu. Hata ukiwa kwenye Serikali ya umoja Zanzibar, ukakosoa chochote, ujue utekaji na mauaji vinakuhusu. Hata ukiwa ndani ya Serikali, ukaonekana ni tishio kwa watu fulani, ujue utekaji na mauaji vinakuhus.

Pia soma: Ally Mohamed Kibao auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

WITO:
Kama wewe mwenyewe hutaki kutekwa, hutaki ndugu na mwanafamilia wako kutekwa na kuuawa, wakati wa kuzuia ni huu wa sasa ambao bado unapumua. Ukishatekwa, umeuawa, huna nafasi ya kuuzuia utekaji na mauaji holela yanayoendelea nchini mwetu sasa, na yanayozidi kuota mizizi.

Viongozi wa dini, walio wengi wapo kimya dhidi ya uovu huo, yawezekana na wao wamekuwa kama nyumbu, wakiamini huo uharamia utaishia kwa CHADEMA. Lakini wajue kuwa utaratibu huu unaoendelea kuota mizizi, watekaji hawataona shida kumteka na hata kumwua kiongozi yeyote wa dini atakayejaribu kukosoa chochote.

Wananchi tujue kuwa kila kitu huanza kwa udhaifu, kisipobugudhiwa au kukataliwa, kadiri siku zinavyoenda, kitazidi kukua na kujiimarisha. Utaratibu huu mpya wa kuwateka na wakati mwingine kuwaua wakosoaji, ulianza kidogo kidogo, pengine utasikia tukio 1 kwa mwaka, lakini siku ziendavyo, matukio yanazidi kuongezeka, hii ni kudhihirisha kuwa watekaji na mfumo wa utekaji na mauaji, vinazidi kujijenga na kujiimarisha. Siku za huko nyuma, wakosoaji walikuwa wanakamatwa na kufunguliwa kesi za kubambikizwa. Sasa wakosoaji wanatekwa, kisha kuuawa mafichoni. Itakuja wakati, wakosoaji watakuwa wanauawa mbele ya macho ya wananchi wote, na sisi, kama nyumbu, tutabakia tunatizama kusubiria siku ya kwetu.

Tunamwomba Mungu utusaidie Watanzania, tuache unafiki, tuuheshimu na kuulinda uhai wetu na wa wenzetu kwa gharama yoyote ipasayo huku Mkono wako wenye nguvu ukitupatia ujasiri na ushidi dhidi ya uovu na waovu.
Umeandika vizuri ila wewe sio Mtanzania? Nilitegemea hadi sasa uwe mbele huko na mabango kupinga ukatili huu, sio kujificha huku. Ila bado inasikitisha yaani kuna watu wanafurahia binadamu anapokufa loh.
 
Hakuna mtu Muoga kama Mtanzania, hata mimi ni muoga sana 🤣🤣.


Chadema muelekeze nguvu kwenye majeshi ili wanajeshi wawaunge mkono. Sisi raia tutaongea mitaani na mitandaoni tu.

Sisi ni waoga mno hata mimi ni muoga
 
Tunalifanya hili jambo la CDM pekeyao ndio maana linaendelea, ni juzi hapo Mbeya hao hao CDM walipigwa wote wakawa hoi, hakuna aliyewasemea zaidi sana baadhi ya mbumbumbu waliwamock.

CCM na watekaji wanachekea chooni kwa hii divide and rule waliyofanikiwa kuifanya!
 
Nakubaliana nawe. Maana wakati wote Rais Samia ameonekana wazi kabisa kusimama upande wa watekaji. Alidiriki kusema wazi kabisa kuwa eti hakuna utekaji. Sijui huu ambao sisi tunauona ni utekaji, yeye kwake ni kitu gani!!
Sio yeye tu hata bungeni pia wanatetea utekaji.
Kambwa kalikuwa kadogo sasa kamekuwa kakubwa na kuwa mbwa mwitu.
 
Back
Top Bottom