SI KWELI Wananchi Ukerewe waanza kutozwa kodi ya mifugo tena

SI KWELI Wananchi Ukerewe waanza kutozwa kodi ya mifugo tena

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
Taarifa zinadai kuwa kuna zoezi la ukusanyaji wa kodi ya mifugo linaendelea wilayani Ukerewe. Inadaiwa kuwa Mbuzi na Ng'ombe sasa wanalipiwa kodi. Yaonekana, kuna kodi nyingi zinarudishwa.

1667312348984.png
 
Tunachokijua
JamiiForums imefanya mawasiliano na viongozi wa Wilaya ya Ukerewe ili kupata ukweli wa madai haya ambao wameeleza yafuatayo:

Mkuu wa Wilaya, Kanali Denis Mwila anasema “Suala hilo mtafute Mkurugenzi ndiye atalizungumzia japokuwa ninavyojua hakuna tozo mpya ni zilezile zilizopo ambazo hazitungwi na Mkuu wa Wilaya wala Mkurugenzi."

“Zinatungwa na Serikali na wao ngazi ya chini wanatekeleza tu, lakini zungumza naye atakufafanulia.”


kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe bwana Emmanuel Luponya Sherembi anasema “Hakuna Tozo ni masuala ya herein, hilo ndilo linaloendelea na linafanyika kwa mujibu wa Sheria n ani maelekezo ya Serikali ili kupata utambuzi wa mifugo.

“Kuhusu kiasi cha malipo siwezi kukitaja kwa sasa kwa kuwa sina hizo takwimu lakini majibu ni hayo na linafanyika Nchi nzima.”
Huo usajili wa kila mfugo na inafanyika kwa tozo toka kwa mfugaji ni nini kama sio kodi?
 
Back
Top Bottom