Wananchi wakiwajibika kujiletea maendeleo wenyewe kwa mtindo huu, jukumu la serikali kitakuwa lipi na suala la kodi na mapato mengine ya taifa (misaada, mikopo) yatashughulikiwaje?Safi kabisaa. Hiyo ndio dhana halisi za siasa ya ujamaa na kujitegemea. Naimba mfano huu uchukuliwe kwa watanzania wote, wajue maendeleo watajiletea wenyewee.
Changamoto ya ubovu wa miundombinu ya barabara katika eneo la Kiruweni, Kata ya Mwika Kusini, Wilaya ya Moshi, imewalazimu wananchi wa eneo hilo waishio maeneo mbalimbali nchini kuchangishana fedha na kuanza ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 72 kwa kiwango cha changarawe.
Eneo hilo ambalo wananchi wake wanajishughulisha na uzalishaji wa ndizi na kilimo cha mazao mbalimbali, limekuwa na changamoto kubwa ya miundombinu ya barabara.
Hali hii imewalazimisha kusafirisha mizigo kwa kichwa hadi sokoni, hivyo kushindwa kufikia ndoto zao za kujikwamua kiuchumi.
Chimbuko la wazo la ujenzi wa barabara lilianzia katika Usharika wa Kiruweni wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), baada ya mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa Machi na Aprili, 2024.
Mvua hizo zimesababisha barabara hizo zishindwe kupitika kwa vyombo vya usafiri, zikiwamo pikipiki.
Akizungumza kuhusu ujenzi huo, Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Kiruweni, Joram Mamuya amesema barabara hizo zimefikia hatua mbaya na kufanya wananchi kushindwa kutumia vyombo vya usafiri na hivyo kulazimika kubeba mazao yao kichwani kuyapeleka sokoni, huku wakitembea umbali mrefu.
Shughuli ya kupanua moja ya barabara zilizoko Kijiji cha Kiruweni Wilaya ya Moshi, ambazo zinajengwa kwa nguvu za wananchi wa eneo hilo ikiendelea ili waweze kuondokana na adha ya kusafirisha mazao kichwani.
Changamoto ya ubovu wa miundombinu ya barabara katika eneo la Kiruweni, Kata ya Mwika Kusini, Wilaya ya Moshi, imewalazimu wananchi wa eneo hilo waishio maeneo mbalimbali nchini kuchangishana fedha na kuanza ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 72 kwa kiwango cha changarawe.
Eneo hilo ambalo wananchi wake wanajishughulisha na uzalishaji wa ndizi na kilimo cha mazao mbalimbali, limekuwa na changamoto kubwa ya miundombinu ya barabara.
Hali hii imewalazimisha kusafirisha mizigo kwa kichwa hadi sokoni, hivyo kushindwa kufikia ndoto zao za kujikwamua kiuchumi.
Chimbuko la wazo la ujenzi wa barabara lilianzia katika Usharika wa Kiruweni wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), baada ya mvua kubwa zilizonyesha mwishoni mwa Machi na Aprili, 2024.
Mtambo wa kushindilia barabara ukiendelea na kazi ya kushindilia moja ya barabara katika kijiji cha Kiruweni, Wilaya ya Moshi,mkoani Kilimanjaro, ambazo zinajengwa kwa nguvu za wananchi.
Akizungumza kuhusu ujenzi huo, Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Kiruweni, Joram Mamuya amesema barabara hizo zimefikia hatua mbaya na kufanya wananchi kushindwa kutumia vyombo vya usafiri na hivyo kulazimika kubeba mazao yao kichwani kuyapeleka sokoni, huku wakitembea umbali mrefu.
"Barabara zetu zilikuwa zimefikia hatua mbaya na hazikuwa zinapitika. Mwaka huu mvua zilinyesha nyingi, barabara zimeharibika zaidi kiasi kwamba hata wananchi wanashindwa kupeleka ndizi sokoni," amesema Mchungaji Mamuya na kuongeza:
Aidha, amesema kufuatia hali hiyo walilazimika kuwatangazia waamini na wananchi kwa ujumla kuona ni namna gani kutengeneza barabara hizo, ili kurahisisha shughuli za usafiri na kuchochea ukuaji wa uchumi wa eneo hilo.
"Tunamshukuru Mungu, wananchi wetu wanaoishi nje ya hapa waliokuja kusherekea Sikukuu ya Pasaka, ambao walikuwa ibadani siku hiyo, nao waliona changamoto hiyo na wakaamua kuchangia. Aprili 7, 2024 tulianza kuchangia kanisani na kuhamasisha kazi hiyo.
"Tuliwaomba Tarura wakafika, wakakagua barabara na kutupa ushauri namna bora ya kuzifanyia kazi. Sisi kwa pamoja tukaona tuanzie hapo. Gharama walizotupa zilikuwa kubwa, zaidi ya Sh180 milioni, lakini haikutukatisha tamaa. Tuliungana kwa pamoja kama jamii na kuanza kazi hii,” amesema mchungaji huyo.
Mtambo wa kumwagilia maji barabara ukiendelea na kazi hiyo katika moja ya barabara katika kijiji cha Kiruweni, Wilaya ya Moshi,mkoani Kilimanjaro, ambazo zinajengwa kwa nguvu za wananchi.
Wananchi wafunguka
Wakizungumza baadhi ya wananchi wa kijiji hicho, wamesema ujenzi wa barabara hizo utawawezesha kusafirisha mizigo yao kwa urahisi kutoka nyumbani hadi sokoni na kuchochea ukuaji wa uchumi katika eneo hilo.
John Tarimo, amesema barabara hizo walizoea kuzitengeneza kwa majembe ya mkono kupitia msaragambo wa kijiji, lakini kwa sasa hilo lilishindikana kutokana na mvua ambazo ziliharibu zaidi barabara hizo.
Anasema baadhi zilijifunga na nyingine kuwa na mashimo makubwa ambayo yalifanya zisipitike.
"Barabara zetu tumekuwa tukizitengeneza kwa majembe ya mikono na mbaya zaidi kwa sasa kijijini huku hakuna vijana, ni wazee ambao hawawezi kutoka msaragambo kutengeneza barabara, hali iliyosababisha barabara kuharibika na kutopitika kabisa. Hii imechangiwa zaidi na mvua nyingi zilizonyesha mwaka huu,” amesema.
Moja ya barabara zinazoendelea kutengenezwa katika kijiji cha Kiruweni, Wilaya ya Moshi, mkoani Kilimanjaro. Picha na Omben Daniel
Tarimo amesema Aprili walivyokwenda kijijini huko, barabara zilikuwa hazipitiki. Kupitia uongozi wa kanisa, wananchi wa eneo hili walijichangisha na kuwashirikisha Wana-Kiruweni wanaoishi maeneo mbalimbali nchini. “Tukashirikishana changamoto hiyo na hivyo tukakubaliana kuchangishana, ili kufungua barabara zote za kijiji hiki ambazo mtandao wake ni kilometa 72,” amesema Tarimo.
Amesema asilimia kubwa ya wakazi wa kijiji hicho ni wakulima, wanahitaji mazao yao yasafirishwe kupeleka sokoni, hali iliyowafanya wengi kuyabeba kichwani kufikia soko kutokana na ubovu wa barabara.
Amesema kutokana na Serikali kukabiliwa na mambo mengi, anatoa wito kwa wananchi katika maeneo mbalimbali kuanza kuchukua hatua ya kutatua changamoto zinazowakabili watu waishio vijijini.
“Tusisubiri kila kitu kifanywe na Serikali. Pale wanapoweza kufanya waunganishe nguvu kama jamii na kufanya jambo, wajitokeze na kufanya. Watu wanapotoka vijijini na kwenda mijini, wakifanikiwa wasisahau nyumbani. Warudi nyumbani kuboresha mazingira ya kwao,” amesisitiza Tarimo.
Shicha Mmbando, mkazi wa kijiji hicho, amesema wameamua kutoa sehemu ya mashamba yao na nguvu kazi, ili kuhakikisha miundombinu ya barabara inapitika kwa urahisi wakati wote wa mvua na kiangazi.
"Barabara zilikuwa ni changamoto. Tunatembea zaidi ya kilometa 10 na mizigo kichwani tukitoa mazao shambani maeneo ya Riata na Holili. Tunapeleka mizigo kichwani kwa sababu magari hayawezi kupita, tunashukuru zikikamilika sasa maisha yatakuwa rahisi," amesema.
Basi hata kodi wasamehewe, ili hiyo pesa ambayo wangetoa kodi, wawe wanaamua waitumie kwa kazi gani kwenye maeneo yao.Safi kabisaa. Hiyo ndio dhana halisi za siasa ya ujamaa na kujitegemea. Naimba mfano huu uchukuliwe kwa watanzania wote, wajue maendeleo watajiletea wenyewee.
Hiyo barabara ni kwa hitaji lao, so wastop bevause kodi zinakwenda kwingine? Nope?
Ni ijungaa bado nasisitiza kodi zunatumika wapi?; haya yakiendelea kuna siku Raia wataambiwa wachangishane wawalipe watumishi wa umma mishahara.Huu ni ujinga kodi zijenge Barabara haiwezekani.
Ndio maana nimekwambia huo ni uongo, kama ni kweli tuambie ni kijiji gani huko Mwanza wananchi waliojichanga kutengeneza barabara za mawe kijiji kizima?Uongo wanini? Nimekwambia mmechelewa sana, Mwanza wameanza zamani sana, tena kiwango cha mawe, unabisha hilo nikuwekee ushahidi?
Na sisi tunapenda wenye fedha wajenge miundombinu ya umaa. Mungu awabariki matajiriiUjamaa gani wakati hao ni capitalists wenye biashara kubwa? Ingekua ujamaa wasingekuwa na fedha ya kujenga barabara
Lini wagomee kulipa kodi na lini waanze kuchangishana?Kwanza wagomee kulipa kodi kwa maana haiwasaidii zaidi ya kugharamia anasa za watawala. Baada ya hapo ndiyo walistahili kuanza kuchangishana.
Jukumu la serikali kwa wananchi ni maeneo mengi saana, mfano, amani, ajira, kupandisha madaraja watumishi, kujenga vituo vya afya na kusambaza huduma mbalimbali katika jamiii, kama vile umeme shule n.k, n.kWananchi wakiwajibika kujiletea maendeleo wenyewe kwa mtindo huu, jukumu la serikali kitakuwa lipi na suala la kodi na mapato mengine ya taifa (misaada, mikopo) yatashughulikiwaje?
Na waganga, wauguzi, walimu, wanajeshi n.k n.k watalipwa na nini sasa ndugu yanguu??Basi hata kodi wasamehewe, ili hiyo pesa ambayo wangetoa kodi, wawe wanaamua waitumie kwa kazi gani kwenye maeneo yao.
Barabara nyingi za Same na Mwanga za Vijijini ni za vumbi, zilianza kuchimbwa kwa kuchoronga mlima na miamba na wananchi wenyewe (kwa zana duni za mikono) kabla ya Uhuru na bara bara hizo zinakwenda milimani ndani ndani, zinapitika mwaka mzima na zipo mpaka leo hii. Hii ni asili yao kupitia utamaduni wao maarufu wa Msalagambo. Ndio utamaduni uliozalisha maendeleo ya kijamii ya kudumu. Hii inapaswa kupongezwa na kuigwa...asilimia 60% ya mkoa wa Kilimanjaro ni wilaya za Same na Mwanga. Je, hali ya maeneo hayo kimiundombinu ikoje?
Nakwambia hao jamaa wa huko Kilimanjaro ni akili kubwa sana, ungewaelewa usiandike hayo.Wananchi wakiwajibika kujiletea maendeleo wenyewe kwa mtindo huu, jukumu la serikali kitakuwa lipi na suala la kodi na mapato mengine ya taifa (misaada, mikopo) yatashughulikiwaje?
Huyu aliyesambaza hiyo 'sumu' amefanikiwa sana kwasababu inaonekana ni kweli..Watz wengi wameaminishwa kwamba Kilimanjaro "imependelewa" kwa miundombinu ya kila aina. Hata ukisoma mijadala mbalimbali hapa JF utakutana na hoja za namna hiyo.
Barabara nyingi za Same na Mwanga za Vijijini ni za vumbi, zilianza kuchimbwa kwa kuchoronga mlima na miamba na wananchi wenyewe (kwa zana duni za mikono) kabla ya Uhuru na bara bara hizo zinakwenda milimani ndani ndani, zinapitika mwaka mzima na zipo mpaka leo hii. Hii ni asili yao kupitia utamaduni wao maarufu wa Msalagambo. Ndio utamaduni uliozalisha maendeleo ya kijamii ya kudumu. Hii inapaswa kupongezwa na kuigwa.
Kwa Mwanga, upande wa Usangi na Ugweno (maeneo ya vijiji vya asili vya wapare) wana barabara za lami iliyochipuka katika barabara kuu ya Dar-Moshi, barabara hizo zinafika huko milimani, juu kabisa, ndani ndani kabisa. Hii ni barabara ya upendeleo tu kwa heshima ya wazee wao kina Kisumo, Mgaya, Msuya, Asha-Rose Migiro, Maghembe na utitiri wa Mabregadia wastaafu wa jeshi ambao wameporomosha majumba mazuri na wanaishi huko na kuzikwa huko.
Maeneo ya mjini katika wilaya za Mwanga na Same kiujumla yana lami, ni sawa tu na makao makuu ya wilaya nyingi hapa Tanzania.
Serikali ipo, Mbunge yupo TARURA ipo hizo pesa wanapangiwa zinaenda wapi?Hawalipi Kodi? Yaani Kodu walipe zineende kununua wapinzani, kulipa Bongo Muvi kule Korea then Raia wachangishane kijenga Barabara. Wachaga wamenza ufala
Excellent!Barabara nyingi za Same na Mwanga za Vijijini ni za vumbi, zilianza kuchimbwa kwa kuchoronga mlima na miamba na wananchi wenyewe (kwa zana duni za mikono) kabla ya Uhuru na bara bara hizo zinakwenda milimani ndani ndani, zinapitika mwaka mzima na zipo mpaka leo hii. Hii ni asili yao kupitia utamaduni wao maarufu wa Msalagambo. Ndio utamaduni uliozalisha maendeleo ya kijamii ya kudumu. Hii inapaswa kupongezwa na kuigwa.
Wrong!Kwa Mwanga, upande wa Usangi na Ugweno (maeneo ya vijiji vya asili vya wapare) wana barabara za lami iliyochipuka katika barabara kuu ya Dar-Moshi, barabara hizo zinafika huko milimani, juu kabisa, ndani ndani kabisa. Hii ni barabara ya upendeleo tu kwa heshima ya wazee wao kina Kisumo, Mgaya, Msuya, Asha-Rose Migiro, Maghembe na utitiri wa Mabregadia wastaafu wa jeshi ambao wameporomosha majumba mazuri na wanaishi huko na kuzikwa huko.
Wilaya ya Mwanga pale barabarani ni Lami ya barabara kuu hakuna kitu kingine.Maeneo ya mjini katika wilaya za Mwanga na Same kiujumla yana lami, ni sawa tu na makao makuu ya wilaya nyingi hapa Tanzania.
Excellent!
Wrong!
Wilaya ya Mwanga ipo milimani ' Ugweno na Usangi' ambako kuna population kubwa sana na shughuli nyingi sana. Hospitali ya Wilaya ipo Usangi. Shule nyingi za sekondari zipo milimani. Kumbuka kuna kilimo cha ndizi, kahawa, Iliki n.k. Kwa ufupi pale Mwanga unapopaona ni kwasababu ya ''convinience'
Lami kwenda Ugweno na Usangi si upendeleo ni kwasababu ya shughuli za kiuchumi za Wilaya.
Wilaya ya Mwanga pale barabarani ni Lami ya barabara kuu hakuna kitu kingine.
Nimekueleza kwamba Wilaya imewekwa pale Mwanga ili kupunguza umbali na watu wa Bondeni kuanzia Nyumba ya Mungu, kuja Lembeni hadi Same na watu kutoka Lake Jipe hadi Njia panda.
Wilaya ilipaswa kuwa katika maungano ya Usangi na Ugweno lakini pia walizingatia maeneo ya Bondeni ikaamuliwa ijengwe pale Barabara kuu ya Moshi-Arusha
Kuhusu Same, ni Wilaya iliyodumaa kwasababu tangu Mkoloni imekuwa Wilaya na Boma.
Harakati za kupinga kodi '' Kodi ya Mbiru' dhidi ya Wajerumani ilifanyika Boma Same wakati huo ikiwa pamoja na Mwanga. Kwahiyo haikutakiwa iwe kama ilivyo. Same ni sawa na Korogwe , Wilaya Kongwe sana nchini zilizodumaa. Tukipata Uhuru Korogwe ilikuwa ''Town council''