Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Wananchi wa Mtaa wa Tegeta "A" katika Manispaa ya Ubungo, jijini Dar es Salaam, wamejitokeza kwa wingi na kuelekea ofisi za Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa huo wakipaza sauti zao kupinga ongezeko la nauli kutoka shilingi 500 hadi 1,000 kwa wanaotumia usafiri wa Daladala na Bajaji za kuchangia.
Wakizungumza kwa hasira, wananchi hao wamesema kupanda kwa nauli kumewaathiri kwa kiasi kikubwa, hasa wafanyakazi wa kipato cha chini na wanafunzi wanaotegemea usafiri huo kila siku.
Akijibu malalamiko yao, Mwenyekiti wa Mtaa huo, Protus Ruwanda, amesema kupanda kwa nauli kumetokana na hali mbovu ya miundombinu, hususan barabara, hali inayoongeza gharama za uendeshaji kwa watoa huduma za usafiri.
Wakizungumza kwa hasira, wananchi hao wamesema kupanda kwa nauli kumewaathiri kwa kiasi kikubwa, hasa wafanyakazi wa kipato cha chini na wanafunzi wanaotegemea usafiri huo kila siku.
Akijibu malalamiko yao, Mwenyekiti wa Mtaa huo, Protus Ruwanda, amesema kupanda kwa nauli kumetokana na hali mbovu ya miundombinu, hususan barabara, hali inayoongeza gharama za uendeshaji kwa watoa huduma za usafiri.