KERO Wananchi wa Ubungo hatuna maji miezi 3 sasa!!

KERO Wananchi wa Ubungo hatuna maji miezi 3 sasa!!

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Ubungo ipi babu acha kugeneralize
Ubungo msewe
Ubungo riverside
Ubungo maji
Ubungo kibangu
Ubungo Tbl pale
Ubungo kule wapemba?
Ubungo relini?
 
Mheshimiwa Rais popote ulipo, na mheshimiwa Awesso, ni miezi mitatu sasa hatujui maji wakazi wa Ubungo Kibangu mtaa wa Kajima tunaomba msaada wenu viongozi wetu hali ni mbaya sana.

Tuna miezi mitatu hatuna maji

Eneo ni kajima (Rivaside juu) mtaa wa Kibangu Ubungo
Eneo hili ni kubwa kuanzia Novo, kwa mdee, kwa mgogo, Kwa mlacha, kilima cha lami, bonde la kajima, na kwa bondia hii mitaa yote hamna maji kabisa

Mfano, Novo magorofani na mpaka kwa mdee wao wa miezi 6 hawajawahi kuona maji.

Maji hayatoki lakini watu wanauza maji na kuleta na magari na kuyauza kwa ndoo 500

Tumelalamika tumechoka inaonekana kuna mfumo wa watu kula hela na kujineemesha

Kipindi cha Magufuli maji yalikua yakitoka

Sio hivyo tu, wameleta matank ya kuuza maji na inadaiwa na miradi ya mheshimiwa fulani hivi

Naombeni mnisaidie namba ya Aweso tumechoka!!
Poleni sana na Mwaka huu mtapata cha moto zaidi maana hakuna mvua ya kutosha

Wakati Serikali inasema watutoze miamala ya simu Ili wajenge maji Vijijini mlikuwa wa kwanza kutukana.

Shida ya miezi 3 tuu mnataka kufa Je sisi wa Vijijini ambao hatujawahi ona Bomba la maji la serikali tusemaje?
 
Back
Top Bottom