Pre GE2025 Wananchi wa Vijiji viwili Jimbo la Namtumbo warudisha t-shirt na fedha za Mbunge wao Vita Kawawa!

Pre GE2025 Wananchi wa Vijiji viwili Jimbo la Namtumbo warudisha t-shirt na fedha za Mbunge wao Vita Kawawa!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607


Nimeona hii clip, wenyeji wa huko tuambieni kama ishu ina ukweli hii?

======================================

Wakizungumza na Wawakilishi wa Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, Vita Rashid Kawawa, Wananchi wa Kijiji cha Mlalamiwa na Matepwende wamedai hawawezi kupokea zawadi za Mbunge wao wakati huduma mbalimbali za Kijamii hazijaimarika.

Viongozi wa Vijiji hivyo walioingia madarakani Novemba 27, 2024 wamesema matumaini yao ni kuwatumikia Wananchi katika matatizo yao ya kijamii yanayowahusu, jambo ambalo pia halijafanywa na Mbunge wao.

Wamesema hayo katika kikao kilichohitishwa na Katibu wa Mbunge Zubery, akishirikiana na Ally Lyuma ambaye ni mpambe wa Kawawa.

Kikao kilifanyika Ijumaa Januari 17, 2025 Saa 1 Jioni katika Kijiji cha Mlalawima, Kata ya Msisima na kuhudhuliwa na Watendaji wa Vijiji vya Matepwende na Mlalawima, Watendaji ni Miraji Haridi na Moyo.

Wenyeviti wa Vijiji ni Kawawa Ally Banda na Athumani Kalumbi Tegi, wengine ni wajumbe wa Serikali za Vijiji hivyo na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM kutoka kwenye matawi.

Viongozi hao wa Serikali za Mtaa wanadai miaka mitano inaenda kukamilisha lakini Mbunge wao hajawatumikia Wananchi wa vijiji hivyo kisha anatuma wawakilishi wake kwenda kutoa zawadi ya jezi na fedha jambo ambalo hawaafikiani nalo.

Wanadai hawana huduma ya maji, madarasa ni machache kiasi kwamba Mwaka 2024 kuna shule wanafunzi walifanya mitihani wakiwa chini ya mti, Barabara ni mbovu na hawana huduma ya maji ambapo watu wanakunywa maji ya kisima wakisea pamoja na mifugo.

Wanadai hali hiyo imesababisha Wananchi kukosa imani na Mbunge wao kutokana na kutohudumia vijiji hivyo viwili.

Majibu ya Mbunge ~
Baada ya Wananchi kugomea t-shirt na fedha za Mbunge, ajitokeza na kusema hizo ni fitna za Kisiasa na kuwa wanaichafua CCM

===================================


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma, Komredi Oddo Mwisho akizungumza na Wanahabari kuhusu masuala ya uongozi leo Januari 23, 2025
 
Siasa zitakuwa ngumu sana mwaka huu kwakuwa watu wamesanuka na kujua hakuna Biashara inalipa Kama siasa.
 
Hapo lazima presha iwe 👆👇👆👇
 
Ndio maana Mwenye Heri JPM alikuwa akiita "CCM ya Magufuli" ambayo iliheshimika hasa.....

Mh. Lissu naomba jinsi ya kupata kadi yangu ya Chadema!
 
Kwa Maafisa Elimu Kata zote, Wakuu wa Shule za Serikali za Msingi na Sekondari, Moshi Manispaa, Kilimanjaro

Mkurugenzi wa Manispaa, Mwajuma Nasombe, kwa mamlaka aliyonayo, anawataka watumishi wote kuchangia fedha kwa ajili ya "Get Together" ya Watumishi Wote wa Moshi Manispaa, ikiwa ni sherehe ya kuukaribisha Mwaka 2025. Sherehe hii itafanyika tarehe 01.02.2025.

Kiwango cha Kuchangia

Wakuu wa Idara na Vitengo, Waratibu Elimu Kata, Wakuu wa Shule za Sekondari, na Walimu Wakuu wa Shule za Msingi: Tsh 50,000/-
Walimu Wote: Tsh 30,000/-
watumishi wengine: Tsh 20,000/-

Mwisho wa kuchangia ni siku ya 26.01.2025 bila kukosa.

Angalizo

Hata hivyo, ni muhimu kuwajulisha watumishi kuhusu baadhi ya masuala yanayohusiana na zoezi hili la kuchangia fedha:

1. Ushirikishwaji: Watumishi wengi hawajashirikishwa kabla ya tangazo hili. Ushirikishwaji wa awali ni muhimu ili kuhakikisha kuwa kila mmoja anafahamu lengo la michango hii.

2. Kamati ya Kuratibu: Hakuna kamati iliyoundwa kwa ajili ya kuratibu zoezi hili. Kukosekana kwa kamati kunaleta hofu miongoni mwa watumishi kuhusu matumizi ya fedha zao.

3. Muda wa Tangazo: Tangazo hili limetolewa muda mfupi sana, kuanzia tarehe 23.01.2025 na mwisho wa kuchangia ni tarehe 25.01.2025. Hii inapunguza nafasi ya watumishi kupanga na kujiandaa kwa michango yao.

4. Mshahara na Madeni: Watumishi wengi wamepokea mshahara wao na tayari wameshatumia kwa kulipa madeni wanayodaiwa. Hali hii inawafanya wengi kuwa na wasiwasi kuhusu kutoa michango zaidi.

5. Kujulishwa kwa Mkuu wa Wilaya: Mkuu wa Wilaya hajajulishwa kuhusu ukusanyaji huu wa fedha za michango, jambo ambalo ni muhimu ili kuweza kufuatilia matumizi ya fedha hizo.

6. *Kuchoshwa na Mkurugenzi:*Watumishi wengi wanasema wanachoshwa na mkurugenzi huyu, kwani mara kwa mara anaitisha michango. Wengi wanahisi kuwa huenda hii ni sehemu ya fedha za kampeni yake kuelekea kwenye uchaguzi wa ubunge.

Ombi

Kwa kuzingatia masuala haya, tunaomba zoezi hili lisitishwe hadi pale ambapo itakapofanyika mabadiliko yanayohitajika ili kuhakikisha kuwa watumishi wanashirikishwa ipasavyo na michango inakusanywa kwa njia ya uwazi na uaminifu.
Hii itasaidia kujenga uhusiano mzuri kati ya watumishi na uongozi wa manispaa.

Tunatumai kuwa maelezo haya yatasaidia katika kueleweka kwa sababu za kutokubali michango hii na kutafutwa kwa suluhisho la kudumu litakalowafaidi watumishi wote wa Moshi Manispaa.

Ahsanteni.
 
Wananchi wakikataa kuburuzwa viongozi watashika adhabu zao tu...asanteni Namtumbo
 
Back
Top Bottom