Wananchi waanza kupata mgawo wa jezi na mipira katika maandalizi ya uchaguzi mkuu; kampeni hi inaitwa mpe mpira na jezi akupe kula

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Kamkeni ya wape mipira na jezi wakupe kula imeanza rasmi mkoani Singida. Wabunge wameanza kampeni hiyo ikiwa ni maandalizi ya uchaguzi mkuu.

Katika kampeni Hii tunategemea kushuhudia wabunge walio ungeni kwa kushirikiana na wale wanaolengwa kugombea Ubunge na udiwani wakifanya mazungumzo na makampuni ya uagizaji vifaa vya michezo waweze kuleta mzigo wa kutosha.

Kampeni hii kama ilivyo kwa miaka ya nyuma itahitimishwa pale waliogombea watakaopewa KULA. Wananchi kupitia michezo wanao uwezo mkubwa mkubwa wakutofathamini mabaya ya kiongozi anayewapa mipira na jezi badala yake kuhesabu kama mtu mwema na anayewajali kwa kuwaleta pamoja kwenye viwanja vya michezo.

Kampeni inaendelea pia huko Kawe, MBEYA mjini na Arusha mjini ambapo wakongwe wa siasa wanaoongoza majimbo hayo wanategemea ushindani mkubwa
 
2024/2025 ndiyo miaka ya mavuno hii kwa wapenda kitonga aka CHAWA.
 
Nawasubiri kwa hamu kwer pesa ntakula na kura sitoi🤣🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…