Vituko haviishi bongo,
Wananchi wilayani Busega mkoani Simiyuwametaka kuondolewa kwa Mwalimu mmoja ambaye jina lake halikupatikana mara moja kwa madai kuwa ni "Freemasons".
Wananchi hao wamefikia hatua hiyo baada ya kutokea "ugonjwa wa ajabu" wa kuanguka anguka kwa wanafunzi katika shule ya sekondari Mwamagisisi.
Wanafunzi wengi katika shule hiyo wameonekana kupata matatizo ya kuanguka ovyo kila wakati jambo ambalo wanachi wamelihusisha na imani za kishirikina huku wakidai kuwa "TV asili" zinaonesha kuwa Mwalimu tajwa ndiye "anayewachezea" wanafunzi hao hadi kupelekea kupata matatizo hayo ya kuanguka ovyo.
Wakizungumza kwenye mkutano maalum wa wazazi na viongozi wa shule juu ya tatizo hilo wananchi wengi walimtuhumu Mwalimu huyo kuwa ni Freemasons na hivyo kutaka aondolewe.
Afisa Elimu wa wilaya hiyo amesema atamwamisha mwalimu huyo ili kuwaridhisha wananchi lakini hakubali kamwe kuwa mwalimu huyo ni freemasons.
Wakielezea sababu za matatizo yanayowapata wanafunzi shuleni hapo, wataalamu wamedai kuwa hiyo inatokana na lishe duni, uchovu na njaa na wala si sababu za ushirikina na u-freemasons kama wananchi hao wanavyoamini.
...Duniani kuna mambo!
Wananchi wilayani Busega mkoani Simiyuwametaka kuondolewa kwa Mwalimu mmoja ambaye jina lake halikupatikana mara moja kwa madai kuwa ni "Freemasons".
Wananchi hao wamefikia hatua hiyo baada ya kutokea "ugonjwa wa ajabu" wa kuanguka anguka kwa wanafunzi katika shule ya sekondari Mwamagisisi.
Wanafunzi wengi katika shule hiyo wameonekana kupata matatizo ya kuanguka ovyo kila wakati jambo ambalo wanachi wamelihusisha na imani za kishirikina huku wakidai kuwa "TV asili" zinaonesha kuwa Mwalimu tajwa ndiye "anayewachezea" wanafunzi hao hadi kupelekea kupata matatizo hayo ya kuanguka ovyo.
Wakizungumza kwenye mkutano maalum wa wazazi na viongozi wa shule juu ya tatizo hilo wananchi wengi walimtuhumu Mwalimu huyo kuwa ni Freemasons na hivyo kutaka aondolewe.
Afisa Elimu wa wilaya hiyo amesema atamwamisha mwalimu huyo ili kuwaridhisha wananchi lakini hakubali kamwe kuwa mwalimu huyo ni freemasons.
Wakielezea sababu za matatizo yanayowapata wanafunzi shuleni hapo, wataalamu wamedai kuwa hiyo inatokana na lishe duni, uchovu na njaa na wala si sababu za ushirikina na u-freemasons kama wananchi hao wanavyoamini.
...Duniani kuna mambo!